Last emperor
JF-Expert Member
- Mar 22, 2015
- 10,352
- 9,805
Kwa sisi tuliokuwa karibu na mzee kwenye siku zake za mwisho ,kati ya watu alioongea nao kwa muda mrefu ukiwatoa viongozi wa dini na familia yake ni CDF Mabeyo, nadhani alikuwa mtu wa karibu sana kwenye moyo wa mzee.
CDF Mabeyo aliambiwa mambo mazito mno pamoja na dokezo la kwamba iwe mvua au jua likitokea la kutokea ahakikishe ya kwamba makamu wa rais anaapishwa kuwa rais wa sita wa nchi yetu. Kwa mjibu wa dokezo hilo kumbe mzee alikuwa ameshamsoma mama kuwa ni mtu mwenye msimamo mkali usioyumba na ni yeye tu ndiyo atakayeweza kuendeleza na kukamilisha miradi yote kwa manufaa ya watanzania wote. Mama alikuwa mwanafunzi mahiri wa mzee aliyehitimu kozi ya miaka 5 kwa daraja la juu kabisa. Kumbuka miaka 5 ni sawa na kumaliza degree ya udaktari.
Kwa jinsi rais Samia anavyokemea tabia mbaya za wahuni ikiwemo pale alipowaonya wabunge waache kudemka na jinsi ambavyo yuko tayari kubishana hadharani na spika Ndugai basi kuanzia leo nimeamini na kuelewa ni kwa nini CDF Mabeyo aliachiwa dokezo lile.
Acha uongo basi.... kujifanya legacy inaendelea