Baada ya kumshauri huyu mwanamke sasa ananipenda mimi

BioPsychologist

JF-Expert Member
Aug 23, 2017
724
1,014
Hello JF members!

Bila Shaka mu-wazima wa afya!

SIO KUOMBA USHAURI BALI NI KU SHARE CHANGAMOTO NA MITIZAMO MBALIMBALI

Taaluma yangu ni mwanasaikolojia (Psychologist) currently nashauri watu katika nyanja mbalimbali za maisha na mostly case nyingi nazokutana nazo ni za mahusiano ya kimapenzi, kwa kweli sehemu hii kuna shida kubwa sana usione watu barabarani wana furaha kuna mengi wanameza.

Issue kubwa iliyonifanya niandike huu uzi ni kuwa kuna MWANAMKE mmoja alikuwa na mahusiano ya kimapenzi na jamaa ambae amekuwa hampendi na kumnyanyasa sana kwa mda wa miaka miwili,kifupi jamaa hakumpenda kivile huyu Dada but Dada alikuwa amezama sana licha ya kujua kuwa hapendwi lakini alishindwa kujikwamua katika mateso hayo ya kimapenzi, nmemsaidia na sasa kawa poa sana na anaendelea na maisha kama kawaida.

Shida ni kuwa sasa kageuka na kuanza kuni napproach mimi (Mshauri wake) lakini mimi kama mwana taaluma na kutokana na miiko ya kitaaluma (Counselling ethics) sipaswi kujenga mahusiano ya kimapenzi na mteja wangu, nmemweleza lakini haelewi kabisa, kwangu nmejaribu kumwambia nimeoa lakini anasema kafanya uchunguzi na kujua sijaoa offcoz ni kweli sijaoa!

Jamani niombe kwa wale wanaodhani kuwa washauri wote wako perfect hii sio kweli kwa 100% kuna washauri wengi tuu (Counselors) hata wao wanasumbuliwa na mahusiano yao, sisi tuna nafasi ya kitaaluma lakini haifanyi tupoteze udhaifu wa kibinadamu tulioumbwa nao, (still we are human being).

Najiamini kuwa hana uwezo wa kunishawishi, bali nimeona nilifikishe hapa either kupata ABCs na mitizamo ya wengine pia na kama kuna watu wanaotoa huduma kama hizi naomba ku share pia uzoefu wenu katika hili.

Karibu!
 
Hapa mbele ya jamii utatuambia kile unachotaka kukuamini mkuu ila nyuma ya pazia, wanadhiri wa Mungu walishindwa na wanawake. Maaskofu, Mapadri wameshindwa. Labda tu karoho kawe hakajampokea basi lakini mengine, changamsha genge.
 
Ni kweli waswahili husema mganga hajigangi sasa ujue mahusiano Na mtu yeyote hayana formula Kwa maana unakutana Na mke wako popote pale kwan nimeshawahi kusikia mwalimu kaolewa Na mwanafunzi wake Na vitu Kama hvyo Na hata ukirudi kwenye miiko yako Ni kwamba huruhusiwi kujiingiza kwenye mahusiano Na mteja wako ikiwa Na maana kwamba yule mteja wako anapofika kwako anajiweka uchi sasa usije ukatumia udhaifu wake ambao umeujua kumteka kimapenz kwahyo nikirud ktk ishu yako naona hakuna tatizo hapo kwan ww unahitaj mke pia Na suala lake ulishalimaliza sasa yy mwenyewe anakuja kwako cyo ww ndye unaanza kumtongoza mm naona hakuna shida isipokuwa Kama kweli umempenda Na unadhani mwanamke anayekufaa unaweza kuendelea hakuna Dhambi
 
Hapa mbele ya jamii utatuambia kile unachotaka kukuamini mkuu ila nyuma ya pazia, wanadhiri wa Mungu walishindwa na wanawake. Maaskofu, Mapadri wameshindwa. Labda tu karoho kawe hakajampokea basi lakini mengine, changamsha genge.
Hahahaha mkuu nimecheka sana kwamba nichangamshe genge! Aiseee huwezi amini kabisa!

Honestly speaking fani hii INA changamoto sana sasa kila mwanamke atakae kuja nitoke nae hivi nitabaki MTU mkuu???
 
Ni kweli waswahili husema mganga hajigangi sasa ujue mahusiano Na mtu yeyote hayana formula Kwa maana unakutana Na mke wako popote pale kwan nimeshawahi kusikia mwalimu kaolewa Na mwanafunzi wake Na vitu Kama hvyo Na hata ukirudi kwenye miiko yako Ni kwamba huruhusiwi kujiingiza kwenye mahusiano Na mteja wako ikiwa Na maana kwamba yule mteja wako anapofika kwako anajiweka uchi sasa usije ukatumia udhaifu wake ambao umeujua kumteka kimapenz kwahyo nikirud ktk ishu yako naona hakuna tatizo hapo kwan ww unahitaj mke pia Na suala lake ulishalimaliza sasa yy mwenyewe anakuja kwako cyo ww ndye unaanza kumtongoza mm naona hakuna shida isipokuwa Kama kweli umempenda Na unadhani mwanamke anayekufaa unaweza kuendelea hakuna Dhambi
Nimekuellewa vzr lakin kumbuka kuwa sio wote wanapenda kiukweli wengine wanatafuta sehemu ya kupumzikia,,nmekuwa nashauri watu wengi kiasi kuwa wengine wanao lalamika ndiyo wenye makosa, kiukweli sijampenda kabisa Kima mpenzi !!
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom