Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 50,720
- 21,779
Kombani awashukia walimu walevi
na Ghisa Abby, Morogoro
WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Celina Kombani, amewaagiza maofisa wa elimu wa wilaya nchini kuwavua madaraka walimu wakuu wanaoendekeza ulevi na kusababaisha shule zao kufanya vibaya.
Waziri Kombani alitoa agizo hilo wilayani Ulanga, Morogoro wakati wa ziara ya kukagua shughuli za kimaendeleo jimboni kwake ambapo alipokea taarifa ya wilaya hiyo kuhusu mikakati ya elimu ya mwaka 2010 ili kuinua kiwango cha elimu kutoka asilimia 48.2 ya mwaka 2009 na kufikia asilimia 60 katika kipindi cha mwaka huu.
Alisema wapo walimu wengi ambao wametoka vyuoni hivi karibuni na wana sifa za ulevi kama walimu wa zamani nao pia wanapaswa kutolewa katika nafazi zao na kupewa walimu wengine wenye sifa nzuri na wanaofuata maadili.
Akiwakilisha mikakati ya kuinua elimu wilayani humo, Kaimu Mkurugezi wa Halmashauri hiyo Clemence Mgoano, alisema kuwa katika kipindi cha mwaka 2009 walishindwa kufikia malengo ya kuinua taaluma kutokana na sababu mbalimbali.
Alizitaja sababu hizo kuwa ni pamoja na utoro wa walimu, ulevi wa kupindukia kwa wakuu wa shule na hivyo kushindwa kuwajibika hali ambayo imesababisha kiwango cha elimu kushindwa kupanda.
Alisema kuwa katika kipindi cha mwaka huu, halmashauri hiyo imejiwekea mikakati mbalimbali ikiwemo ya kuwapatia ushauri nasaha walimu hao pamoja na kutoa barua za kalipio na onyo kwa walimu wakuu walevi, watoro na wanaoshindwa kuwajibika.
na Ghisa Abby, Morogoro
WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Celina Kombani, amewaagiza maofisa wa elimu wa wilaya nchini kuwavua madaraka walimu wakuu wanaoendekeza ulevi na kusababaisha shule zao kufanya vibaya.
Waziri Kombani alitoa agizo hilo wilayani Ulanga, Morogoro wakati wa ziara ya kukagua shughuli za kimaendeleo jimboni kwake ambapo alipokea taarifa ya wilaya hiyo kuhusu mikakati ya elimu ya mwaka 2010 ili kuinua kiwango cha elimu kutoka asilimia 48.2 ya mwaka 2009 na kufikia asilimia 60 katika kipindi cha mwaka huu.
Alisema wapo walimu wengi ambao wametoka vyuoni hivi karibuni na wana sifa za ulevi kama walimu wa zamani nao pia wanapaswa kutolewa katika nafazi zao na kupewa walimu wengine wenye sifa nzuri na wanaofuata maadili.
Akiwakilisha mikakati ya kuinua elimu wilayani humo, Kaimu Mkurugezi wa Halmashauri hiyo Clemence Mgoano, alisema kuwa katika kipindi cha mwaka 2009 walishindwa kufikia malengo ya kuinua taaluma kutokana na sababu mbalimbali.
Alizitaja sababu hizo kuwa ni pamoja na utoro wa walimu, ulevi wa kupindukia kwa wakuu wa shule na hivyo kushindwa kuwajibika hali ambayo imesababisha kiwango cha elimu kushindwa kupanda.
Alisema kuwa katika kipindi cha mwaka huu, halmashauri hiyo imejiwekea mikakati mbalimbali ikiwemo ya kuwapatia ushauri nasaha walimu hao pamoja na kutoa barua za kalipio na onyo kwa walimu wakuu walevi, watoro na wanaoshindwa kuwajibika.