Baada ya kumjali na kupigania mafanikio yake, leo nimegeuka kuwa mshamba

Nilimkuta akiwa ana stress za maisha baada ya kumaliza masomo yake katika chuo fulani. Nilimshika mkono, nikamfuta machozi kisha nikampenda na nikamfundisha kunipenda, nikaishi nae kwa zaidi ya miez kumi. sikuhitaji kumuona akiwa katika msongo wa mawazo bali nilitafiti nikagundua shauku yake ilikuwa ni kupata kazi au biashara ainue familia yake na ajenge mustakabali wa maisha yake.

Niliamini katika falsafa ya ushirikiano katika kujenga mustakabali wetu kwani kila mara alionyesha kuwa mimi ni chagua sahihi kwa kauli na matendo. Nilipambana kwa hali na Mali kwa kipato changu cha kawaida na hii exposure ndogo mpaka nikafanikiwa akapata kazi kwenye shirika moja la miradi ya afya hapa nchini akaenda kufanya kazi nje ya mkoa niliopo mimi.

Wiki mbili baada tu ya kuajiriwa alibadilika sana alibadilika sana, ninaweza kumpigia simu nakuta yuko busy kuanzia saa tano mpaka saa saba usiku na anaona simu yangu inaingia hapokei na akimaliza kuongea hanitafuti hata nikimuulza hatak kusema anaongea na nani, akaenda mbali zaid ukimtumia sms anakujib kwa mkato na ikafikia hatua hataki kunitafuta na nikimtafuta hapokei simu.

Nimewahi kwenda huko anakofanyia kazi nimekaa siku tatu yaani muda wote hajiamini na hawez kutoka nje akaongozana na mm. Dharau na kiburi ndio umekuwa mtindo wa maisha yake. Naishia kuitwa mshamba kwa kumfatilia eti nijiamini. Kifupi nimejitoa kwa mengi nikijua huyu atakuwa mke wangu halaf amekuja kunibadilikia ghafla, inauma sana na Niko katika wakati mgumu sana ukizingatia niko naandika tasnifu yangu niweze kumaliza shahada yangu ya uzamili lakini nashindwa hata kusimamia biashara zangu zinanishinda.

Nabaki muda wote ndani nimejifungia tu roho inaniuma sana kila nikiwaza mawazo yangu yananipeleka mbali zaidi ya jinsi ambavyo siwez kuelezea, nimepitia changamoto nyingi katika maisha yangu lakin hili naona linanizidi.. ndugu zangu naona kabisa jahazi linazama.

Mwenye ushauri mzuri utakaonisaidia na kunitoa ktk hii hali naomba aje PM au hapa hadharani anishauri. Jf naona ndio second home yangu naamini ndugu zangu wenye busara zaidi mtanisaidia.
1. Jeepeers and creepers!! Kama nakumbuka vzr ni muvi moja ya kibabe sana..

2. Shahada ya uzamili, hii si ni master degree?

Mapenzi yana nguvu hivi??

All in all, kama ulimpeleka kwa miradi ya afya ya HIV, huko kuna vihela hela vya kununua mboga.
Amekutumia kama daraja, maisha ndivyo yanavyohitaji.. Kila mtu anahitaji daraja la kumfikisha sehemu.

Move on bro.
 
Nenda club, piga bia tafuta mademu visu zaidi yake lakini fanya hit & run tu... Life is too short to make rooms for heart breaks, enjoy it while you still have it... Your happiness lies within your own hands, not from others.
 
unategemea kumaliza shahada yako ya uzamili lakini hujui jinsi ya kuhandle issue za mapenzi? mkuu wewe kweli ni mshamba na inaonekana umejifunzia mapenzi uzeeni, hamna cha kuwashauli watu kama nyinyi.
 
Fanya mambo yako, mpotezee kabsa, japo ni ngumu,ila ni possible. Ukiweza futa namba yake. Muda ni mwalimu mzuri..kuna siku atarudi analia na kujuta kwa nini alkukosea, then na wewe unapotezea mazima
 
Hapo mm ndio huwa nakuwaga tofauti kidogo na wengine. Kama ni wake, basi hataondoka. Kitendo cha kuondoka tu, huyo sio wake. Yani aende huko apelekewe moto weee, mambo yakiwa magumu ndio arudi tena kwa jamaa???
Inashangaza mnoo mkuu yan wanawake akili zao za hovyo mnoo ..Et kama n wake atarud ...
 
unategemea kumaliza shahada yako ya uzamili lakini hujui jinsi ya kuhandle issue za mapenzi? mkuu wewe kweli ni mshamba na inaonekana umejifunzia mapenzi uzeeni, hamna cha kuwashauli watu kama nyinyi.

Naamini katika honesty, humanity, commitment & care kama uwekezaji mzuri katika mahusiano yenye tija kuelekea ndoa. Na kama sio siwezi kuwa prayer, less commited and rude bali sioni busara yake. Kama kuamini katika falsafa hii ni ushamba kwa tafsiri halisi basi nakiri kweli mimi ni mmoja wa hao washamba.
 
Back
Top Bottom