Baada ya kulazimishwa kujiunga na NSSF nimekuwa na masikitiko makubwa

LICHADI

JF-Expert Member
Feb 4, 2015
4,124
11,114
Nikikaa nikifikiria hela yangu inavyopasuliwa kwenye mshahara wangu ambao ni jasho langu alafu anayechukua hizo hela ananipangia masharti ya kunilipa roho yangu inaniuma sana, Nikiangalia mshahara wangu kiwango nnachokatwa kwenda NSSF ni kikubwa.

Naona sio mafao tena bali ni sadaka hii natoa kwa mipango ya watu fulani na sio kwa manufaa yangu wallahi. Kama kipindi cha Nyerere, Mwinyi, Mkapa, Kikwete watu walichukua pesa zao bila wasiwasi iweje sasa hii mifuko ikatae kuwalipa watu pesa zao wakati ni majasho ya watu.

Nawaambieni hili swala lilianza polepole kuwakumba watu wa sekta binafsi wenye mikataba mifupi, wale waliopo serikalini ambao wana mikataba ya kudumu wakajiona wapo salama kwa kuwa wanauhakika wakula mshahara hadi umri wa kustaafu na wakazoa mafao yao yote.

Lakini mda ulivyozidi kwenda kibao kikageuka tena yani sasa hata mzee mwenye miaka 55 analazimika kupewa mafao yake kwa 25% tu, mengine atapewa eti kidogo kidogo eti mpaka kifo.

Jamani huu si unyonyaji wa wazi wazi huu, hizi hela sio mali yenu, ni mali ya wafanyakazi. Mtueleze mnapozipeleka hadi hii mifuko inapumulia gesi maana hata mfanyakazi wa NSSF mwenyewe ukimwambia astaafu alafu mafao yake umpe asilimia 25 hawezi kukubali maana huo ni unyonyaji wa hali ya juu.

Wabunge wetu tulio wachagua sijui wanakazi gani jamani, Haya mambo ni mazito na ndio tuliyowatuma mkatutetee lakini kwa kujali matumbo yenu mmekaa kimya na mmethubutu kupitisha huu mswada mzito kwa wafanyakazi ambao mnajua hautowagusa nyie,
 
Yaani mtu mzima unapangiwa matumizi,
Sijui na watoto wetu tuwapangie nini

Poleni sana
 
Kipind private sector inalalmikia fao la kujitoa ndio Usaliti Ulipoanza kwa vyama vya wafanyakazi ikaenda kwa wadau wa ajira ikawafikia wale wafanyakaz wa serikalin ikaenda kwa Wabunge kupitsha muswada sa hv wanajifanya wanalia lia baada ya kusikia its only 25%
 
Walianza private sector kuwa mikataba ikiisha no kuchukua chetu wakatuona mapoyoyo then wamehamia kwa wazazi wetu wapewe 25% only hii nchi hii ngoja tu tutifuane kwanza tuanze upya ustaarabu,wamekalia milion 10 eti nitafute ajira ingine utazani wananisaidia kujibu interview PAMBAFUUU
 
Kipind private sector inalalmikia fao la kujitoa ndio Usaliti Ulipoanza kwa vyama vya wafanyakazi ikaenda kwa wadau wa ajira ikawafikia wale wafanyakaz wa serikalin ikaenda kwa Wabunge kupitsha muswada sa hv wanajifanya wanalia lia baada ya kusikia its only 25%
Hatari sana hii
 
Nikikaa nikifikiria hela yangu inavyopasuliwa kwenye mshahara wangu ambao ni jasho langu alafu anayechukua hizo hela ananipangia masharti ya kunilipa roho yangu inaniuma sana, Nikiangalia mshahara wangu kiwango nnachokatwa kwenda NSSF ni kikubwa.

Naona sio mafao tena bali ni sadaka hii natoa kwa mipango ya watu fulani na sio kwa manufaa yangu wallahi. Kama kipindi cha Nyerere, Mwinyi, Mkapa, Kikwete watu walichukua pesa zao bila wasiwasi iweje sasa hii mifuko ikatae kuwalipa watu pesa zao wakati ni majasho ya watu.

Nawaambieni hili swala lilianza polepole kuwakumba watu wa sekta binafsi wenye mikataba mifupi, wale waliopo serikalini ambao wana mikataba ya kudumu wakajiona wapo salama kwa kuwa wanauhakika wakula mshahara hadi umri wa kustaafu na wakazoa mafao yao yote.

Lakini mda ulivyozidi kwenda kibao kikageuka tena yani sasa hata mzee mwenye miaka 55 analazimika kupewa mafao yake kwa 25% tu, mengine atapewa eti kidogo kidogo eti mpaka kifo.

Jamani huu si unyonyaji wa wazi wazi huu, hizi hela sio mali yenu, ni mali ya wafanyakazi. Mtueleze mnapozipeleka hadi hii mifuko inapumulia gesi maana hata mfanyakazi wa NSSF mwenyewe ukimwambia astaafu alafu mafao yake umpe asilimia 25 hawezi kukubali maana huo ni unyonyaji wa hali ya juu.

Wabunge wetu tulio wachagua sijui wanakazi gani jamani, Haya mambo ni mazito na ndio tuliyowatuma mkatutetee lakini kwa kujali matumbo yenu mmekaa kimya na mmethubutu kupitisha huu mswada mzito kwa wafanyakazi ambao mnajua hautowagusa nyie,
Tuliokuwa tukiandika humu kuhusu NSSF mlituona tuna njaa zetu sasa na nyie mkubali yaishe kwani hamkutaka umoja.
 
Back
Top Bottom