Baada ya kujifungua mke akataa kumpa mama mkwe mtoto

Kima mdogo

JF-Expert Member
Sep 17, 2011
303
46
Ni mke halali wa ndoa wa mwanamume wa Kimachame ambao ndoa yao mpaka sasa ina miaka 12,na walianza maisha wakiwa hawamiliki mali yyt zaid ya kitanda na makochi ya mbao,imekua ni kawaida kwa mama mkwe huyu na watoto wake wa kike kuenda kwa kijana huyu na kumsakama na kumzushia maneno ya uongo mke wa kijana huyu hali iliyopelekea ugomvi wa mara kwa mara kati ya mume na mke huyu, Mkasa wa mke huyu kukataa kata kata kumpa mama mkwe wake mtoto amshike ulitokea baada ya mama mkwe huyo kuenda nyumbani kwa kijana wake na kukuta mke wake anaumwa na kusema kuwa mke wa kijana wake AMEENDA KWAO NA KURUDI NA MAMIZIMU YA BABA YAKE (mke alienda kijijini kwao kushiriki dua ya marehemu baba yake na alikua na ujauzito wa wiki 3),Baada ya kauli ya mama huyo ndipo mke huyo alipomweleza mumewe kuwa maneno aliyoongea mama yake juu yake hayakumpendeza,Ndipo mumewe akachukua jukumu la kumuuliza mama yake kama kweli ameongea maneno hayo ndipo mama huyo alipokataa kata kata kuwa hajatamka maneno hayo ....inaendelea next page

Na kudai kuwa mwanamke huyo amemsingizia ili asiende nyumbani kwa mwanae, mama huyo hakuishia hapo akaondoka kwenda nyumbani kwake kijijini Machame na kuendelea kulalamika kwa kila mtu anayemjua kuwa kasingiziwa na mwanae kuona hivyo akaamua kuwauliza dada wa kazi na mwanae wa kike kama walisikia mama yake akiongea hayo,Wote wakasema walimsikia, ndipo ndugu wakike wa mume huyu wakaungana na mama yao kumshinikiza kaka yao amfukuze mke huyo kwa madai kwamba amemsingizia mama yao na hafai kuwa mke,Baada ya kelele nyingi mke akiwa na ujauzito wa miez 4,mume wake akamgeuzia mkewe kibao akaanza kumnyanyasa,Akawa anachelewa kurudi,akirudi anamgombeza mkewake bila sbb za msingi na kwa shock yule mke akapatwa na matatizo makubwa ya kuvuja damu na kulazwa hospitali zaid ya mara 6, naujauzito ulipofikisha miez 7 madaktar wakagundua kw mapigo ya mtoto ya moyo yanadunda taratibu sn kutokana na kitovu cha mtoto kujisokota shingoni na kumnyima pumzi(hii ilitokana na mke kulia mara kwa mara kutokana na manyanyaso).

Ndipo madaktari wakaamua kumfanyia upasuaji ili kuokoa maisha ya mtoto na mama. Mtoto alizaliwa na ilimlazimu atengane na mama yake akawekwe kwenye chumba maalumu cha kutunzia watoto waliozaliwa chini ya miez 9 huku akiwa amewekewa oksijeni,...kwa kipindi chote hichi mpaka mke kufikia kufanyiwa upasuaji wa dharura mama mkwe wake alikua anasema huyo mtoto hatazaliwa na hakuwah kumjulia hali mkwe wake kwa namna yyt. Baada ya siku saba mtoto na mama wt wakawa wanaendelea vizuri na kuruhusiwa kwenda nyumbani. Wiki 2 baadae ghafla mama mkwe akaja tena na kumwambia mke wa kijana wk kw AMLETEE MTOTO AMKAGUE ANATAKA KUONDOKA, baada ya kauli hii mke huyu aliishiwa nguvu na KUSHINDWA KUMPA MAMA MKWE WAKE MTOTO na kuishia kujifungia ndani na kulia.Baada ya hapo mama aliondoka kurudi kwake na wanandugu wanamlazimisha kaka yao amfukuze mke wake,Na taarifa za kusikitisha ni kuwa ni miezi 8 MUME HUYO AMEKATA MAWASILIANO YT NA MKEWE KWA KUHAMA CHUMBA NA KUMNYIMA TENDO LA NDOA, je nani anamakosa na nini kifanyike?

NAOMBENI MNIWIE RADHI KWA UANDISHI MBOVU nilikimbia shule nikakimbilia hela ILA HABARI HII NI YA KWELI KABISA na imemtokea dada yangu.JE KATI YA MUME, MKE NA MAMA MKWE NANI ANAMAKOSA NA WAFANYAJE KUINUSURU NDOA HII.Mods naombeni muiunganishe na mniwekee paragraph
 
kwa post hii, nafuta maneno yangu ya awali.

Pole!

NAOMBENI MNIWIE RADHI KWA UANDISHI MBOVU nilikimbia shule nikakimbilia hdla ILA HABARI HII NI YA KWELI KABISA na imemtokea dada yangu.Mods naombeni muiunganishe na mniwekee paragraph
 
Labda kama mimi si mwanamke nawahakikishia wanajf hakuna binadamu atanitesa,yaani ningekuwa ndio huyu mwanamke after all i went through trust me huyo mama na hao watoto wake ningekuwa nimeshawapa vilema vya ubongo,nyoko zao walale na huyu kaka basi shenzi kabisa,yaani by the time i would be done with them,mtoto wake na kaka yao atakuwa na adabu,huu uvumilivu si utaki unalia nini kama wewe mpole kwenu ulizaliwa mwenyewe,akiii yaani ingekuwa mimi dunia ingeelewa kwani jela si binadamu wapo au eti ni dada yangu he he,jamani huu ni uuaji we mleta mada mpaka sasa umefanyaje?
 
Labda kama mimi si mwanamke nawahakikishia wanajf hakuna binadamu atanitesa,yaani ningekuwa ndio huyu mwanamke after all i went through trust me huyo mama na hao watoto wake ningekuwa nimeshawapa vilema vya ubongo,nyoko zao walale na huyu kaka basi shenzi kabisa,yaani by the time i would be done with them,mtoto wake na kaka yao atakuwa na adabu,huu uvumilivu si utaki unalia nini kama wewe mpole kwenu ulizaliwa mwenyewe,akiii yaani ingekuwa mimi dunia ingeelewa kwani jela si binadamu wapo au eti ni dada yangu he he,jamani huu ni uuaji we mleta mada mpaka sasa umefanyaje?
acha tuu
 
Yaani ndugu wa mume wakianza chokochoko huna raha na mumeo....tukipendeza roho zinawauma...tukivaa vizuri oooh pesa zote anampa mke wake...kupendeza tutapendeza watoto wa wenzenu hata tuvae magunia..CHOYO kinawasumbua

Sent from my BlackBerry 9100 using JamiiForums
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom