Baada ya kuangalia filamu ya Blood Diamond; Nimejikuta na maswali mengi kuhusu mustakabali wa bara la Afrika

Bavaria

JF-Expert Member
Jun 14, 2011
53,104
53,341
Naangalia blood diamond kwa mara nyingine tena.

Najikuta na maswali mengi kuhusu mustakabali wa bara la Afrika.

Hivi kuna nchi watu wanaishi maisha haya? Kuuana na kuchinjana kama kuku? Nchi kushindwa kujitawala hadi makundi ya waasi wanashika sehemu kubwa ya nchi.

Wapi Afrika tumekosea? Tunashindwa kuzitumia hizo 'resources' kuleta maendeleo? Badala zinakuwa ni laana.

Wananchi wa kawaida hata siku moja sidhani kama wanatamani kama hizi resources kuwepo kwenye nchi zao. Zisingekuwepo wangishi kwa amani.

Hatukuwahi kustahili kuwa na hizo 'resources'.
 
Tanzania tunajipa kichwa kuwa na madini ya kila aina ila asilimia kuwa ya wananchi ni masikini wa kutupwa.

Sasa nini mantiki ya kuwa na hizo resources?

Bora zisingekuwepo.
 
kwani hiyo movie ni based on true fact na ikiwa ndio kwa kiwango gani ili tuweze kujadili facts na fictions
 
Naangalia blood diamond kwa mara nyingine tena.

Najikuta na maswali mengi kuhusu mustakabali wa bara la Afrika.

Hivi kuna nchi watu wanaishi maisha haya? Kuuana na kuchinjana kama kuku? Nchi kushindwa kujitawala hadi makundi ya waasi wanashika sehemu kubwa ya nchi.

Wapi Afrika tumekosea? Tunashindwa kuzitumia hizo 'resources' kuleta maendeleo? Badala zinakuwa ni laana.

Wananchi wa kawaida hata siku moja sidhani kama wanatamani kama hizi resources kuwepo kwenye nchi zao. Zisingekuwepo wangishi kwa amani.

Hatukuwahi kustahili kuwa na hizo 'resources'.
Rejea kauli ya Trump utapata jibu
 
sababu ya ubinafsi wa viongozi wengi Africa, wazungu wanatumia nafasi hiyo kutugawa, jiulize waasi wanauziwa na nani silaha genuine kuliko hata za serikali. ile filamu ukiicheki vizuri unakuta Leonardo DiCaprio yule mzungu aliact kama dalali wa yale madini

images
 
sababu ya ubinafsi wa viongozi wengi Africa, wazungu wanatumia nafasi hiyo kutugawa, jiulize waasi wanauziwa na nani silaha genuine kuliko hata za serikali. ile filamu ukiicheki vizuri unakuta Leonardo DiCaprio yule mzungu aliact kama dalali wa yale madini

images
Sure, ubinafsi ndio unaotumaliza Waafrika
 
Ubinafsi na uroho wa pesa/madaraka. Hiyo movie niliweza kuiangalia mpaka mwisho nikawaza na kuwaza nikabaki kusema Mungu tusaidie na shida zetu tusifike huko.
Inasikitisha mno. Na ukiingalia unauona uhalisia kabisa. Kweli Afrika bado tuna safari ndefu ambayo haitakaa ifike mwisho
 
Ukiangalia vuzuri utagundua hata ile kambi ya jeshi inatumika tu kusafirishia hayo madini
 
Kule kwenye jimbo la Delta nchini Nigeria ambako ndiko mafuta maelfu kwa maelfu ya matani ndiko yanakozalishwa wanaita hayo mafuta ni kinyesi cha shetani kimewaletea nuksi badala ya Baraka.

Ndivyo ilivyo nchi nyingi zenye rasilimali ni kama zina laana.
 
sababu ya ubinafsi wa viongozi wengi Africa, wazungu wanatumia nafasi hiyo kutugawa, jiulize waasi wanauziwa na nani silaha genuine kuliko hata za serikali. ile filamu ukiicheki vizuri unakuta Leonardo DiCaprio yule mzungu aliact kama dalali wa yale madini

images
Hawa ni dini sio resources
 
Ubinafsi na uroho wa pesa/madaraka. Hiyo movie niliweza kuiangalia mpaka mwisho nikawaza na kuwaza nikabaki kusema Mungu tusaidie na shida zetu tusifike huko.
Huwezi muomba Mungu akusaidie kwenye ujinga wako ambao unaweza kuutatua bila hata kumuomba.
Ujinga ulio afrika ni wa kiwango cha lami.
Labda tumuombe Mungu asingetupa hizo resources ili tuwe na amani.
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom