Baada ya kuacha kumlea mwanangu kimayai, nimeona akiimarika

Bado sijutii uamuzi nliofanya,

Hapo awali mtoto nlikuwa namlea kimayai huku nikijioa moyo sitaki apitie shida nlizopitia kumbe nlikuwa navuka mipaka kabisa ambayo haikuwa vema kwa mtoto,

Nikabadili malezi na kweli dhana yangu ya kutotaka mtoto asipate ahida nlizopitia nliendelea nayo ila iliishia tu kuhakikisha mtoto anapata chakula, anavaa, anapata elimu, n.k na sio kuvuka mipaka.

Schoolbus nliacha kulipia maana shule ipo karibu tu kutembea ni dakika 25, kuna wenzake wanaosoma shule za kata hutembea masaa sasa mimi nikaona kwani huyu ni kilema hadi asitembee??

anajifulia,,, Zamani lilikuwa jukum la haus gel ila nikaona huu upuuzi tu, kwani mikono yake imevunjika?? mama yake alisema namtesa ila nikamkumbusha adha atayopata mtoto endapo asipokua na msaada.


anapalilia bustani ndogo .

, anafyeka nyasi (sio ombi)...Saizi silipi mtubaje kufyeka,

kutandika kitanda,...Ashazoea kabisa,

kufagia uwanja ... Hapa saus gel nae kapunguza mzigo

Zamani mchana mama yake alipendelea kumwekea ratiba apikiwe wali au chips, nikaona hayo ndio ni mapenzi ya mama hasa ukiangalia uwezo wa kumudu hivi vitu upo lakini kama baba niliingilia kati hii ishu, Saizi mchana ni ugali kwa kwenda mbele nimempiga marufuku house girl kumpikia wali au chips, Saizi ni ugali tu na hii ni kwa faida ya mtoto.

Kucheza nje na wenzake,..ni haki yake, tatizo wazazibwenye uwezo huwa tunawaona watotot wetu ni kama malaika wasicheze nje na wenzao, Nlikuwa namfungia ndani nikamnunulia Playstation kuchezea game na kuangalia katuni ila kiukweli maisha halisi sio katuni bali ni watu, japo kwa tahadhari.

Shule kwangu nataka mtoto awe na uwezo kawaida tu, kipimo changu huwa ni wastani, yeye hushika nafasi ya tano kati ya wanafunzi 30 na mimi wala sina shida kabisa, sina mambo ya kuhakikisha anashika nafasi gani, ilimradi ana wastani unaoridhisha wala sina shida, ila huo wastani asipoufikia hata awe wa kwanza hapo nina shida.

Huu ni mwaka wa pili nadhani tangu nibadili style ya malezi na sijaona anakosa chochote zaidi ya kupata vingi zaidi.

Ushauri wangu kwa wazazi wenzangu ni kwamba wazazi wenye uwezo msitumie visingizio vya sitaki mwanangu aishi shida nlizopitia huku mkivuka mpaka huo na kutengeneza mtoto ambae ni mayai mayai.

hata maua ukiyamwagilia sana maji mizizi yake huwa mifupi maana maji yapo tele ila mvua kali au upepo mkali ukipita maua yanatoka kwasababu mizizi haijaenda chini kutafuta maji kama maua yanayomwagiwa wastani tu yenye mizizi mirefu inayotafuta maji yaliyo chini hata mvua kali au upepo mkali ukipita mizizi inashikilia ua halitoki.
Mkuu wewe kama baba ukizembea kwenye malezi ya mtoto hasa wa kiume jua unaandaa bomu litakalo kulipukia huko baadae.

Uko kwenye right track komaa!!
 
Siku zingine mnapotaka 'Kujimwambafai' Kwetu kutokana na kupata 'Vipesa' vyenu vya Ngama ( Kubahatisha ) msiwe mnazunguka sana katika kutaka Kututangazia kwani wengine huwa tunawashtukieni mapema tu.
Mazao ya awamu ya tano ndio Kama hivi wenyewe Kila kitu mtu anaona ana onewa na kutambishiwa pole mzee
 
Binafsi naamini mtoto kutanua kwa pesa ya Mzazi wake Ni upunguani kwani unamuharibia moral ya kupambana na kuja kujipambania kivyake.

Utakuta mzazi umenunua ki gali chako au Cha mkopo kabisa usivyo na akili unampa nae akae mbele eti akiendeshe na wewe unajikenulisha meno unazani sifa . Kiufupi unaua spirit ya mtoto wako ya kujipambania na kuifanya akili yake ilalee doro .

Ndio maana watoto wakishua wengi hata wakiachiwa urithi hawawezi kuendeleza Mali zaidi ya option ya kuuza na wakiuza wanafilisika na kubakia na sifa tu mjini kuwa walikuwa nazo sijui boni hia hia..na wengine kufikia hatua ya kuwaombea wazazi mfe ili abaki na mali na kuwaona nyie ndio mnao mchelewesha katika utajiri wake.

Lkn yote hiyo tatizo Ni mzazi mwenyewe unaandaa mabomu ya kuja kukulipua mwenyewe . Lkn ukimcholea mipaka kuwa bwana wee umeona ile gari eeee....! Basi ile gari halikuhusu komaaa uje upate la kwako kwa pesa yako na ili uweze kumiliki vitu Kama hivi unatakiwa upite hapa utokeee hapa uzamie hapa uibukie kule zaidi ya hapo ndugu utaumia maishani na hii tabia yako ya kulala Kama paka.

Sasa nyie endeleeni kuwafungia watoto wenu na washinde wanagaragara kwenye hizo sofa utafikiri vijibwa vya kizungu nawa hakikishia mkikatika gafla hao watoto wenu sijui watakaa na nani mwingine anae penda kuishi na vijibwa vya kizungu na sio watu ambao wanaweza kuamka asubuhi na kufanya usafi hata kujifulia vijinguo vyao.

Mzazi pesa Ni zako wewe ndio unajua umezipataje hivyo mjengee mwanao misingi ya kuja kuzisaka zake na sio kutegemea zako.
 
Miaka miwili anaanza kujifunza kula mwenyewe akifika mitatu tayari fundi.

Waacha..!!! Mi mbona wangu ana miaka minne na nusu saiz na bado naona analishwa kila kitu kuanzia uji mpaka chakula.?🙆‍♀️🙆‍♀️🙄🙄
 
Waacha..!!! Mi mbona wangu ana miaka minne na nusu saiz na bado naona analishwa kila kitu kuanzia uji mpaka chakula.?🙆‍♀️🙆‍♀️🙄🙄
Duh pole mama yake anamuona bado hawezi.
 
Wazazi wengine baadhi hawajui kulea watoto katika njia zipasazo... Huu usasa/utandawazi pia unachangia

"Mtoto mayai" unakuta hata chai kuchemsha hawezi, kujipikia hawezi, kufua, kudeki, kuosha vyombo hawezi pia

Wazazi msijisahau sana, tekelezeni wajibu wenu wa malezi, mfundishe shida na raha azijue pia akiwa mkubwa asijutie (Ajifunze kupitia changamoto zimkomaze, sina maana ya kumtesa)

Majukumu na kazi ndogondogo zitamjenga vizuri kujitegemea mwenyewe
Naitikia ni vizuri sana.
Unajua watu wanafikiri watoto tutakuwa nao milele, kumbe sivyo, ataondoka kwako kwenda kujitegemea. Ajifunze vitu hivuoy ni muhimu. Naamini wengine wanaodrkeza watoto wafuate.
Nimeona kwa jursni binyi smezaa akiwa nyimbani kwa mama yske. Hajui kumtinza hata mtoto wake, smemwachia mama yake amlee mjukuu. Huyu hata akoolewa sidhani majukumu ya mke ataweza kuyamudu?
 
Naitikia ni vizuri sana.
Unajua watu wanafikiri watoto tutakuwa nao milele, kumbe sivyo, ataondoka kwako kwenda kujitegemea. Ajifunze vitu hivuoy ni muhimu. Naamini wengine wanaodrkeza watoto wafuate.
Nimeona kwa jursni binyi smezaa akiwa nyimbani kwa mama yske. Hajui kumtinza hata mtoto wake, smemwachia mama yake amlee mjukuu. Huyu hata akoolewa sidhani majukumu ya mke ataweza kuyamudu?
Inasikitisha sana

Sent from my SM-J720F using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom