UHURU JR
JF-Expert Member
- Jul 24, 2014
- 16,239
- 7,603
Kuna wakati huwa najiuliza hivi Tanzania ilikuaje kabla ya uongozi wa Magufuli? Maana ukisikiliza lawama anazobeba Magufuli kwa mtu mgeni na Tanzania pengine anaweza kufikiri Tanzania chini ya Magufuli inautofauti wa ardhi na mbingu na Tanzania chini awamu zilizopita nyuma yake. Magufuli katawala kipindi kifupi sana cha miaka mitano ila lawama anazobeba ni kana kwamba matatizo yote ya uongozi kwenye nchi hii chanzo ni Magufuli au kwamba yeye ndio chanzo cha Tanzania kuwa nyuma kimaendeleo.