Baada ya Jamii Media kufungua kesi mahakamani, napendekeza tutoe michango ya pesa kuisapoti

Chillo97

JF-Expert Member
Jun 18, 2016
630
932
Wana jf.

Nimeona uzi ukizungumzia Jamii Media kufungua kesi mahakamani juu ya sheria ya makosa ya kimtandao.. Kwa jinsi nilivyomsikiliza ndg MELO inaonekana sisi watumiaji ndio tutakaokuwa hatarini na wengine wataogopa kufichua maovu wakiogopa msumeno huu wa sheria unaowapa nguvu sana polisi.

Kwa maoni yangu napendekeza uongozu wa Jamii Media uweke namba za simu na acc za benki ili tuweze kuchangia uendeshwaji wa kesi hii ambayo zaidi inatuhusu sisi watumiaji.

Asanteni.
 
Wana jf.

Nimeona uzi ukizungumzia Jamii Media kufungua kesi mahakamani juu ya sheria ya makosa ya kimtandao.. Kwa jinsi nilivyomsikiliza ndg MELO inaonekana sisi watumiaji ndio tutakaokuwa hatarini na wengine wataogopa kufichua maovu wakiogopa msumeno huu wa sheria unaowapa nguvu sana polisi.

Kwa maoni yangu napendekeza uongozu wa Jamii Media uweke namba za simu na acc za benki ili tuweze kuchangia uendeshwaji wa kesi hii ambayo zaidi inatuhusu sisi watumiaji.

Asanteni.
Wazo zuri, Watanzania! nani afanye hivyo! hatujitambui-subiri response you will judge
 
Tuchangie kuendeaha kesi ya kupinga sheria? Sheria iko sawa tumia mtandao kwa weledi vinginevyo miaka kdhaa itakuhusu tu segerea
 
Update ya Kesi mpaka dakika hii kimya ,kuna yeyote anayefahamu maendeleo ya kesi hii.
 
Aisee sijawahi kuona kiazi kama wewe!!!
Nyie ndo walewale! Sheria ifuatwe kama hujui matumizi ya mtandao kwa ustaarabu uwajibishwe tu. Badala tuchange kununua hata madawati eti kuendesha kesi ili watu waruhusiwe kukiuka ustaarabu
 
Kuteketeza MB zetu humu ni mchango tosha.
Nadhani unaweza kuteketeza mb na moderator wasipofucha siri zako na wakizoto pale zunapohitajika unaweza pia kuteketeza muda wako police na usymbufu zaidii...hii kesi unatuumiza sisi zaidi
 
Nyie ndo walewale! Sheria ifuatwe kama hujui matumizi ya mtandao kwa ustaarabu uwajibishwe tu. Badala tuchange kununua hata madawati eti kuendesha kesi ili watu waruhusiwe kukiuka ustaarabu
Kwani kesi iliyofunguliwa ni ya kutaka watu waendelee kukiuka taratibu
 
8 Reactions
Reply
Back
Top Bottom