Na mwandishi wetu
Jimbo la Gairo mkoani Morogoro ni kati ya majimbo nchini yatakayokuwa na upinzani mkali. Tajiri wa kampuni ya mabasi ya abiria Ahmed Shabiby awamu hii anakabiliwa na upinzani mkali jimboni kwake.
Mtoto wa mwalimu mstaafu na mzee maarufu wa Gairo Mzee Johnson Mmassa, ajulikanae kama Dr. Joel J. Mmassa msomi wa kiwango cha PhD ya uchumi na mhadhiri wa chuo kikuu kikubwa hapa nchini maarufu kama UDOM ni mmoja kati ya watia nia kuwania ubunge wa jimbo la Gairo.
Wakazi wa mji wa Gairo uliopo mpakani mwa mkoa wa Morogoro na Dodoma barabara kuu ya Dar Es Salaam na Dodoma wanatabainisha kuwa kama Dr. Joel hatachomoa jina lake kwa ushawishi wa aina yoyote toka kwa tajiri Shabiby huenda ikawa ni mwisho wa ubunge kwa Mhe. Shabiby.
Nikiwa njiani kuelekea Dodoma kijana mmoja mkazi wa hapa aliniambia kuwa Gairo baada ya Dr. Chiduo tunakwenda kupata mbunge msomi mwingine mwenye kiwango cha juu cha elimu (Daktari).
Aliendelea kueleza kuwa kwa ushawishi wa pesa ya Shabiby tunaamini ataongoza kwa wingi wa kura ya maoni lakini hata hivyo tunauhakika vikao vya juu vya chama chini ya Mhe. Magufuli havitapitisha jina lake.
Mkazi mwingine alidai kuwa Shabiby pesa yake tunakula kipindi hiki cha uchaguzi akishapata ubunge huwa hatujui mpaka kipindi cha uchaguzi, huwezi kumfananisha na tajiri wa mabasi ya Abood mbunge wa Morogoro mjini ambaye kutokana na pesa yake amekuwa na msaada mkubwa binasi kwa jamii yake.
Mama mwingine ambaye alijitambulisha kwa jina moja la Hadija aliyekuwa akiuza karanga za kuchemsha kwenye ndoo alieleza kuwa tumesikia tetesi Shabiby anawasiliana na ndugu wa Dr. Joel akiwemo baba yake mzazi akiwashawishi kwa fedha ili mwanae ajitoe kwenye kinyanganyiro.
Aliendelea kueleza safari hii tutahakikisha anatoka hata kwa kuchagua upinzani. Mabasi yake hatupatii hata rifti ili tukauze karanga Dodoma kwa kudai tutachafua mabasi yake, ukikosa Abood na Nyehunge za Morogoro kwenda Mwanza siku hiyo hatuendi Dodoma.
Nilipompigia Dr. Joel J. Mmassa baada ya kujitambulisha aliniambia kuwa hakuwa tayari kunithibitishia kama atagombea uubunge wa Gairo, lakini alikiri kuwa huingia mara kwa mara Gairo kuwasalimia wazazi na marafiki zake na amekuwa anafanya hivyo kila wakati siyo kipindi hiki tu cha uchaguzi, kwani yeye amekulia hapo na ana ndugu na marafiki zake wengi.
Jimbo la Gairo mkoani Morogoro ni kati ya majimbo nchini yatakayokuwa na upinzani mkali. Tajiri wa kampuni ya mabasi ya abiria Ahmed Shabiby awamu hii anakabiliwa na upinzani mkali jimboni kwake.
Mtoto wa mwalimu mstaafu na mzee maarufu wa Gairo Mzee Johnson Mmassa, ajulikanae kama Dr. Joel J. Mmassa msomi wa kiwango cha PhD ya uchumi na mhadhiri wa chuo kikuu kikubwa hapa nchini maarufu kama UDOM ni mmoja kati ya watia nia kuwania ubunge wa jimbo la Gairo.
Wakazi wa mji wa Gairo uliopo mpakani mwa mkoa wa Morogoro na Dodoma barabara kuu ya Dar Es Salaam na Dodoma wanatabainisha kuwa kama Dr. Joel hatachomoa jina lake kwa ushawishi wa aina yoyote toka kwa tajiri Shabiby huenda ikawa ni mwisho wa ubunge kwa Mhe. Shabiby.
Nikiwa njiani kuelekea Dodoma kijana mmoja mkazi wa hapa aliniambia kuwa Gairo baada ya Dr. Chiduo tunakwenda kupata mbunge msomi mwingine mwenye kiwango cha juu cha elimu (Daktari).
Aliendelea kueleza kuwa kwa ushawishi wa pesa ya Shabiby tunaamini ataongoza kwa wingi wa kura ya maoni lakini hata hivyo tunauhakika vikao vya juu vya chama chini ya Mhe. Magufuli havitapitisha jina lake.
Mkazi mwingine alidai kuwa Shabiby pesa yake tunakula kipindi hiki cha uchaguzi akishapata ubunge huwa hatujui mpaka kipindi cha uchaguzi, huwezi kumfananisha na tajiri wa mabasi ya Abood mbunge wa Morogoro mjini ambaye kutokana na pesa yake amekuwa na msaada mkubwa binasi kwa jamii yake.
Mama mwingine ambaye alijitambulisha kwa jina moja la Hadija aliyekuwa akiuza karanga za kuchemsha kwenye ndoo alieleza kuwa tumesikia tetesi Shabiby anawasiliana na ndugu wa Dr. Joel akiwemo baba yake mzazi akiwashawishi kwa fedha ili mwanae ajitoe kwenye kinyanganyiro.
Aliendelea kueleza safari hii tutahakikisha anatoka hata kwa kuchagua upinzani. Mabasi yake hatupatii hata rifti ili tukauze karanga Dodoma kwa kudai tutachafua mabasi yake, ukikosa Abood na Nyehunge za Morogoro kwenda Mwanza siku hiyo hatuendi Dodoma.
Nilipompigia Dr. Joel J. Mmassa baada ya kujitambulisha aliniambia kuwa hakuwa tayari kunithibitishia kama atagombea uubunge wa Gairo, lakini alikiri kuwa huingia mara kwa mara Gairo kuwasalimia wazazi na marafiki zake na amekuwa anafanya hivyo kila wakati siyo kipindi hiki tu cha uchaguzi, kwani yeye amekulia hapo na ana ndugu na marafiki zake wengi.