Baada ya dhiki ni faraja; vimbwanga vya wauza korosho baada ya mauzo lindi na mtwara

dmkali

JF-Expert Member
Nov 17, 2014
11,279
21,396
Ama kweli mwenzenu nimethibitisha laivu zile semi za wahenga

"baada ya dhiki ni faraja, pesa sabuni ya roho, pesa mwana haram!, mipango siyo matumizi, pata pesa tujue tabia zako"

mimi kama mfanya biashara tangu niliposkia MTWARA NA LINDI KUCHERE! niliwahi fasta kutafta fursa.
Baada ya kufika huku nimejifunza mambo mbalimbali kutoka kwa wakulima wa korosho...........

kikubwa nilichogundua wakulima wengi wana mashamba ya kurithi kwa maana hiyo hawana uchungu na faida ya zao hili, wanafanya tu almradi, heka moja ya korosho wanaambulia 1M, shamba zuri kidogo wanavuna hadi 1.5M,....

Kwa wachache wenye mashamba makubwa ya hekali zaidi ya 30 ndiyo wanaambulia hadi 35mil.
Kwa maana hiyo zoezi la kuwatambua wauza korosho Limerahisishwa, mkulima anaeonekana anauza korosho za 5MIL na kuendelea inabidi waonyeshe kwanza mashamba yao ili kuepuka WALANGUAJI, kiufupi walanguaji wamedhibitiwa ingawa wengine wanafanikiwa kibishi, lakini wanaokamatwa na mzigo wa korosho bila kuonesha mashamba yanayoendana na mzigo wao yanataifishwa mara moja.

TOFAUTI NA MATARAJIO YA WALIOWENGI

Ni kwamba tofauti na matarajio;
  • baada ya kulipwa pesa za korosho wengine wameongeza wake,
  • Baada ya kuuza korosho wengine wametapeliwa na vimada,
  • Baada ya kuuza korosho wengine hawajarudi makwao hadi hivi sasa,
  • Baada ya kuuza korosho wachache wamekumbuka kufanya maendeleo,
  • Baada ya kuuza korosho wengi wameparamia kununua RADIO KUBWA zile PANASONIC na sambufa wakicheza na kuruka,
  • Baada ya kuuza korosho wananywesha SODA hadi mbuzi na kuwavisha miwani kama ishara ya U-doni,
  • Baada ya kuuza korosho wananunua hadi madela ya kuvalisha mbuzi wao.
  • Baada ya kuuza korosho mabasi kama BUTI LA ZUNGU,MANING NICE yanaendelea kushusha warembo wa kila aina kuja kuhakikisha mkulima wa korosho anarudi shambani mapema iwezekanvyo...
Heri maskini Wa roho kuliko Ushamba
 
Kwanini unateseka Mkuu na matumizi yao...btw Hawaamini wanachokiona kama wamelipwa mkwanja wa maana...
 
Wewe mtoa mada ni muongo mkubwa hayo unayosema ni hadithi za kusimuliwa tena ni uzushi unaoenezwa juu ya watu wa kusini ili waonekane ni wajinga.....
Sijawahi kusikia kashfa za kijinga kama hizi kwa wakulima wa kahawa,tumbaku,alizeti,mahindi na pamba isipokuwa korosho tuu,ebu waacheni wakulima wafanye maisha yao
 
Kuongeza wake ni utashi wa mtu mkuu lkn vilevile usisahau ndyo kazi ya pesa! Amefanya matumizi xax shda ik wap
 
Wewe mtoa mada ni muongo mkubwa hayo unayosema ni hadithi za kusimuliwa tena ni uzushi unaoenezwa juu ya watu wa kusini ili waonekane ni wajinga.....
Sijawahi kusikia kashfa za kijinga kama hizi kwa wakulima wa kahawa,tumbaku,alizeti,mahindi na pamba isipokuwa korosho tuu,ebu waacheni wakulima wafanye maisha yao
Miminipo kusini huku nadhibitisha kuwa alicho kiandika mtoa post niukweli mtupu
 
Upo kusini maeneo gani? Wewe unaishi tu huko lakini hujuwi kitu
Acha kudanganywa, Angekua huko, asingeandika yupo kusini, angeandika yupo, Mtwara, Masai Lindi, Sio kusini kusini ni kanda ama eneo.
Ila anaeshangaa watu kufanya vituko wawapo na pesa, ndiyo washamba. Maana hata kwa Wafanyakazi tunaona hali inavyobadili mwisho wa mwezi, kwa watu wamachimboni tunawaona.
Na hata wafanya biashara, wadogo nenda maeneo ya mnada Uone.
 
Wewe mtoa mada ni muongo mkubwa hayo unayosema ni hadithi za kusimuliwa tena ni uzushi unaoenezwa juu ya watu wa kusini ili waonekane ni wajinga.....
Sijawahi kusikia kashfa za kijinga kama hizi kwa wakulima wa kahawa,tumbaku,alizeti,mahindi na pamba isipokuwa korosho tuu,ebu waacheni wakulima wafanye maisha yao
...
Nenda maeneo ambayo kahawa inalimwa uone utofauti uliopo ukilinganisha na maeneo yalimwayo korosho!
 
...
Nenda maeneo ambayo kahawa inalimwa uone utofauti uliopo ukilinganisha na maeneo yalimwayo korosho!
Kuna maeneo ya walefi kama maeneo ya walima kahawa, Si ndiko kuliko na madume suruani, mpaka wanawake wakaalika Midume ya nchi jirani huko.
 
Back
Top Bottom