Baada ya CHADEMA kubweteka, Tanzania hatuna chama mbadala cha kuwasumbua CCM

Enzi na Enzi

JF-Expert Member
May 29, 2020
888
821
CCM chini ya JPM tunaomba iendelee na moto huu huu katika kuisimamia serikali. Ni wazi kuwa nchi hii ilikuwa imeharibika sana kiasi cha kufanya kila mwenye pesa alikuwa na uwezo wa kumfaya maskini chochote.

CHADEMA walisaidia sana kelele na kauli mbiu yao ya VUA GAMBA UVAE GWANDA, ni kweli gwanda za CHADEMA zilikuwa na heshima mitaani kipindi hicho.

CHADEMA wakabweteka, wakaanza kubaguana, na kudharauiana kiasi cha kufikia chama kuwapokea na kuwasafisha na baadae kuwapa kugombea urais jambo ambalo liliwapa nafasi kujipanga upya na kurudisha heshima ya kuvaa nguo za kijani mitaani. Nasasa chadema siyo habari tena ktk nchi hii.

Baada ya chadema nulidhani ACT watajitahidi kurudisha heshima ya vyama vya siasa tanzania .

Lakini nimechunguza siasa na viongozi wa vyama hivi nikagundua ACT nao wamekuja kibiashara kupitia mgongo wa siasa km kosa walilolifanya Chadema baada ya kuaminiwa.

Kiongozi mkuu wa ACT tetesi zilizopo nikwamba amefanya makubariano na maalim seif kuchukua 50% ya rudhuku ya chama akiwa na mtaji wa wabunge wengi kutoka zanziber.

Zitto cyo mwanasiasa wa ukombozi, Zitto anasadikiwa ni CCM pia!
Membe hilo najua mpaka kesho membe ni mwana CCM, ila wajinga ndio waliwao.

Usitangetange baki njia kuu, tanzania tuna chama kimoja tu! Nacho ni CCM.
Nashauri kipatkane chama kipya cha siasa ambacho kitatengeneza wanasiasa wake kusukuma siasa na maendereo ya nchi hii baada ya jpm kumaliza mda wake, maana siamini km tutapata rais kama yeye tena.
 
Mbona nchi ndio imezidi kuharibika, mbunge anachapwa risasi hadharani, CAG akihoji manunuzi ya kifisadi anatenguliwa kienyeji, manunuzi yanafanywa kienyeji kwa amri ya rais kama ananunua magauni ya mkewe, kesi za kubambikiwa n.k !!

Usipepese mdomo! Utakuwa una maanisha tundu lisu alipigwa risasi hadharani, usitumie neno mbunge kumpa heshima ambayo hakustaili wakati anapigwa shaba.

Yawezekana hujui mambo ya hovyo aliyowafanyia watu tundu lisu ktk nchi hii akitumia fani yke ya sheria.

Tundu lisu kaumiza watu sana ktk nchii kuliko jambazi yyte aliyegonga milango ya watu usiku.

Zile risasi zilizomkoswa koswa amshukuru mungu kwakumpa nafasi yapili kujilekebisha badara yakuendelea kuwatukana na kuwasema vibaya watu aliowahujum katika nchi zinazomlipa pesa zakula yy na mke wake na wtt wake.

Aombe msamaha na arudi nyumbani.
 
.
IMG-20200717-WA0028.jpg
 
Usipepese mdomo! Utakuwa una maanisha tundu lisu alipigwa risasi hadharani, usitumie neno mbunge kumpa heshima ambayo hakustaili wakati anapigwa shaba.

Yawezekana hujui mambo ya hovyo aliyowafanyia watu tundu lisu ktk nchi hii akitumia fani yke ya sheria.

Tundu lisu kaumiza watu sana ktk nchii kuliko jambazi yyte aliyegonga milango ya watu usiku.

Zile risasi zilizomkoswa koswa amshukuru mungu kwakumpa nafasi yapili kujilekebisha badara yakuendelea kuwatukana na kuwasema vibaya watu aliowahujum katika nchi zinazomlipa pesa zakula yy na mke wake na wtt wake.

Aombe msamaha na arudi nyumbani.
Wewe utakua unamzungumzia Lissu mwingine, acha ndoto za mchana!
 
Tulia, naona umeanza kuweweseka mapemaa ati kutaka majina ya watia nia!! Acha kutumia Police mapema hivi
 
shithole countries bhana.

Mfumo wa vyama vingi una faida zaidi ya hasara. Siwaelewagi wanaoshabikia vyama shindani kufa, au wanaotaka kuuwa hivyo vyama kama regime ya awamu hii.
 
Ila tusisahau ni ccm,hii hii,ambayo imeshindwa kuifanya TZ,iwe kama China,Malaysia,India,hawa wote tulikuwa sawa 1960s

Ni lichama hili hili,lililosimamia wizi wa kutisha wa Mali ya umma,maskandali ya escrow,Richmond,gesi,mauzo ya nyumba za serikali,
 
Wewe nzi wa kijani ulitaka Chadema washike bunduki kama CCM wanavyotumia vyombo vya dola?


Hapana,
Kosa walilofanya chadema ni kumtukana mwanamke hadharani ukimsema ni maraya na muathirika wa magonjwa hatari harafu baadae wewe mwenyewe unamuoa.( utakuwa umenielewa)

Chadema hao hao wakaanza siasa za kibabe, wao kwa wao wakagawanyika makundi kiasi cha baadhi yao kuwa na hadhi ya kupanda ndege nawengine kuwa makapuku.

Bungeni wakafunga plastic midomo
Burgeti zote wakapinga.
Wakasema serikali dhaifu
Wakatukana police
Wakatukana majaji/mahakama
Wakabeza ununuzi wa ndege
Wakabeza maendeleo yte.

FUNGA KAZI Covid-19 wakahamasisha tufungiwe ndani.

Wakatutangaza kimataifa tunakufa kwa covid-19 mpaka maiti zinazagaa mungu akawaweka wazi.

Wabunge wao wale wanawake wawili wakawa wanatapika maneno katika media wakidhani nisifa. Kumbe wanajidhalilisha kwa mila na desturi ya mwanamke wa kiafrica

Kifupi chadema hawana namna tena walishajichafua wenyewe na wakuwasafisha hayupo.

Ukisema uelezee hapa anguko lao kiukweli ni habari ndefu.

By inzi wa blue.
 
Wamebweteka kwa kunyimwa Kuendesha mikutano, kufungwa, kupigwa risasi, kuharibiwa Mali zao, kupewa kesi, kuumizwa na kutekwa, kuzuiwa wasipandishe bendera zao......hakika wamebweteka, hongera!
Mkuu naona hautaki kuremba kabisa.😎😎
 
Ila tusisahau ni ccm,hii hii,ambayo imeshindwa kuifanya TZ,iwe kama China,Malaysia,India,hawa wote tulikuwa sawa 1960s,
Ni lichama hili hili,lililosimamia wizi wa kutisha wa Mali ya umma,maskandali ya escrow,Richmond,gesi,mauzo ya nyumba za serikali,

Uko sawa kabisa mkuu! Naunga mkono hoja yko kwa 100%
Ndio maana tulijua chadema itatukomboa! Kumbe cku zte unabii wa kristo atatoka kwa wayahudi japo wayahudi walichukiwa sana bado ulitimia kupata kiongozi mzuri ndani ya ccm.

Ndo maana hata yy jpm anasema hata ndani ya ccm mafisadi yamo.

Hivyo tumuunge mkono jpm na ccm yake, na wanasiasa waanzishe vyama vya siasa vya kukomboa wa tz na uchumi wetu kwakuwa bado tuna hitaji siasa zenye ushindani wa hoja cyo siasa walizoanzisha chadema.
 
CCM mnatia aibu!. Mnashindana na chama kilichobweteka alafu mnaogopa tume huru ya uchaguzi!

Mnapiga bomu mochwari alafu mnajisifu mmeua!
 
Wamebweteka kwa kunyimwa Kuendesha mikutano, kufungwa, kupigwa risasi, kuharibiwa Mali zao, kupewa kesi, kuumizwa na kutekwa, kuzuiwa wasipandishe bendera zao......hakika wamebweteka, hongera!
Wangekuwa dhaifu wasingekuwepo hadi sasa. Ni kwa sababu tu uchaguzi huu ni kati ya CDM na vyombo vyote vya dola, adha waisi chadema ndio ingekuwa chama tawala baada ya oktoba.
 
Wamebweteka kwa kunyimwa Kuendesha mikutano, kufungwa, kupigwa risasi, kuharibiwa Mali zao, kupewa kesi, kuumizwa na kutekwa, kuzuiwa wasipandishe bendera zao......hakika wamebweteka, hongera!
Kwa kuongezea tu. Ruzuku na michango ya wabunge waliyokua wanaipata wameshidwa hata kujenga Makao Makuu ya chama, kuimarisha ofisi za kanda. Hakika walibweteka haswaa. Hongera zao wanavuna walichopanda
 
Back
Top Bottom