Baada ya awamu ya tatu ya Benjamin Mkapa kumaliza muda wake, mtu sahihi wa kumrithi alitakiwa awe Magufuli. Nchi ingepaa sana

thetallest

JF-Expert Member
Oct 21, 2017
8,256
9,085
Ukifuatilia maelezo ya wachambuzi mbalimbali mitandaoni kuhusu kauli ya Mheshimiwa Kikwete msibani kwa marehemu Mkapa utagundua kuna mabishano ambayo hayana umuhimu wowote,sana yametanguliza chuki binafsi kwa hawa viongozi.

Kauli ya Jakaya kikwete ilijikita katika kumuelezea Mkapa kama muasisi wa mifumo tulionayo kwa sasa na ndoto yake katika kuipaisha Tanzania kiuchumi .

Kikwete kakiri Marehemu Mkapa aliipokea nchi toka kwa Mwinyi ikiwa na hali mbaya sana kiuchumi,hili halina ubishi,ndio maana akatengeneza mifumo ambayo mpaka anaachia madaraka nchi ilikuwa vizuri kiuchumi na serikali ilikuwa na fedha ya kutosha.alidhibiti mfumuko wa bei kwa kiwango cha hali ya juu sana.


Baada ya Kikwete kupokea kijiti alianza vizuri sana ,lakini ukiangalia muda ulivyozidi wasaidizi wa Kikwete walimuangusha sana,pamoja na nia yake njema , kwani baadhi yao hawakuwa waadilifu hata kidogo ,walikuwa ni mchwa,ushikaji pia ulimuharibia sana kazi,kipindi chake tumeona watumishi wa umma walikua na ukwasi usioelezeka , ndio maana wakati anamkabidhi Rais Magufuli kijiti ,serikali ilikuwa haina fedha ,serikali ilikuwa na dollar za kimarekani 1.8 billion tu,hii ilikuwa ni pesa ndogo sana kuendesha nchi kwa mtawala mpya, ilihitaji kazi ya ziada kupata fedha za kuendesha serikali,
Hata hivyo Rais Magufuli alisimama imara sana bila kuyumbishwa na wale waliozoea kuweka serikali mfukoni.

Kwanini nasema Magufuli alitakiwa ampokee kijiti Mkapa,kutupeleka kwenye hicho kipato cha dollar 3000? ,ni kwasababu Mkapa hakucheka na nyani ,alikua serious sana ,alikuwa mkali ,hakuyumbishwa na maneno maneno aliamini kile anachokisimamia,ukimuangalia Magufuli ni typical Mkapa ndio maana kupitia mifumo ilioachwa na Mkapa kafanya makubwa ndani ya muda mfupi sana (,Mega projects),nakadhalika , ili mifumo alioacha Mkapa ilete ufanisi ilihitaji kiongozi mkali asiecheka na watumishi wabovu wasio simamia mifumo ,hivyo "I repeat again Magufuli was a right person after Mkapa ".

Kwahiyo ndoto ya Mkapa ingetimia 2025 kama alivyofikiri, kua na kipato cha dollar 3000,kwani gap lisingekuwa kubwa kama tulionavyo sasa ikiwa awamu ya nne isingezembea kusimamia mifumo ilioachwa na Mkapa .

Nimalize kwa kusema mifumo ilioachwa na Mzee Mkapa ni madhubuti ispokua ilikosa na inakosa viongozi waadilifu wa kuitumikia .

Mwisho tuwaenzi viongozi wetu wote wakuu waliohai na waliotangulia mbele ya haki , kwani kila mmoja ana nafasi yake katika mafanikio ya taifa letu,tusiwabeze hata kidogo kwa chuki zetu binafsi , kufanikiwa kwa Tanzania si kazi ya mtu mmoja ,ni muunganiko wa juhudi zetu sote
 
Ukweli ni kwamba baada ya Nyerere raisi alitakiwa awe mkapa na baada ya Mkapa raisi alitakiwa awe kikwete na baada ya kikwete raisi alitakiwa awe kati ya Emmanuel Nchimbi au January Makamba.

Magufuli na akili zake za kijamaa hakutakiwa kabisa kuwa Raisi bora tungempa Prof Muhongo 2015 mtu Mwenye akili na exposure
 
Sasa sasahivi imeshindwa nini kupaa,five year USD 100.00,five years budget za serikali zinatekelezwa kwa wastani wa chini ya 50%,for five years ukuaji wa uchumi umeongezeka kutoka 7% hadi 4%.in five years ujenzi wa barabara ya njia sita Dar chalinze umeperuruka,In five years idadi ya masikini nchi hii imeongezeka ,in five years tumevuruga masoko ya mazao Kama korosho,mbaazi na kahawa ,in five years nchi hii imepotea kidiplomasia na imepoteza mahusiano na nchi nyingi marafiki.Magu si mchezo mkuu.he is so exceptional
 
Ni kweli kabisa, ila kitendo cha Magufuli kupokea nchi kilofa haina hela mpaka kuahirisha sherehe za uhuru kimagirini kusingizia usafi kumbe hakuna hela kilimtia uchungu. Ndo maana asubuhi asubuhi aliamkia wizara ya fedha kimachungumachungu na kwa kweli ana uchungu na wezi mchwa walioitafuna nchi hii na wote wenye nia hiyo.
 
Ukweli ni kwamba baada ya Nyerere raisi alitakiwa awe mkapa na baada ya Mkapa raisi alitakiwa awe kikwete na baada ya kikwete raisi alitakiwa awe kati ya Emmanuel Nchimbi au January Makamba.

Magufuli na akili zake za kijamaa hakutakiwa kabisa kuwa Raisi bora tungempa Prof Muhongo 2015 mtu Mwenye akili na exposure
Mkuu unafikiri ni akili za kijamaa? Incompetency yake ndo inamfanya aamini kuwa akitembelea kivuli Cha Nyerere labda ataonekana yeye ni bora,yaani hata wakati aliopo haujui
 
Sasa sasahivi imeshindwa nini kupaa,five year USD 100.00,five years budget za serikali zinatekelezwa kwa wastani wa chini ya 50%,for five years ukuaji wa uchumi umeongezeka kutoka 7% hadi 4%.in five years ujenzi wa barabara ya njia sita Dar chalinze umeperuruka,In five years idadi ya masikini nchi hii imeongezeka ,in five years nchi hii imepotea kidiplomasia na imepoteza mahusiano na nchi nyingi marafiki.Magu si mchezo mkuu.he is exceptional
Si amefanikiwa kuhamia dodoma mkuu?!!,ha ha haaaaaa
 
Hivi ni kwa muda mfupi namna hii jitihada na uadilifu wa waasisi wa taifa letu umeshasahaulika namna hii! Hivi kwa namna iwayo vyovyote vile yale ambayo yalifanywa na Mwl. Nyerere kwa sasa hayapaswi kuwekewa misingi kwa wale waliomfuatia ktk kuliongoza taifa letu?

Nchi hii imepitia ktk hatua tofauti za kimaendeleo, na tena chini ya awamu tofauti za uongozi. Kuanza kutoa sifa ktk kipindi cha awamu moja huku tukipuuza misingi ya awamu zilizopita, huu utakuwa ni unafiki na hata kutaka kujipendekeza kwa malengo fulani.

Natambua ukaribu kati ya Magufuli na Mkapa. Bali isiwe sababu ya kutaka kujipendekeza na kutaka kuonekana kuwa unaunga mkono serikali hii.
 
Nini kinamfanya hivi sasa ashindwe kuifanya nchi ikapaa?!

Kakuta GNI per capita ikiwa USD 980 lakini hadi sasa ndo kwanza amefikisha USD 1080; an increase of ONLY USD 100 kwa muda wote aliokaa madarakani!!

GNI.png


Mkapa aliachaForeign Reserve ikiwa roughly USD 2 Billion, na JK akaacha ikiwa USD 4.4 Billion, lakini hadi sasa ndo kwanza inacheza around USD 5 Billion!!

Reserve.png


BOT.png


Nchi ina uhaba mkubwa wa Walimu wa Sayansi; na awamu iliyopita ilifanya jitihada mbalimbali ili kutatua tatizo hilo, na iliposhindikana kabisa, waka-introduce Special Diploma (Science & Mathematics) ili kukabiliana na upungufu huo!!!

JPM alipoingia tu, akafuta ile programme kwa madai wanaosoma ni vilaza, lakini miaka 5 anamaliza sasa lakini bado hajaleta alternative!!

Kwa kuona umuhimu wa Sayansi katika ulimwengu wa leo, awamu iliyopita ikahamasisha ujenzi wa maabara! JPM baada ya kuingia alitarajiwa aanzie wengine walipoishia ili kuhakikisha shule zetu zina maabara lakini kinyume chake, maabara kazipiga chini na bado hana alternative!!

Sasa nchi angeipaza vipi wakati hadi leo hajaona umuhimu wa sayansi?! Wakati hadi sasa hajaona umuhimu wa kuwa na walimu wa kutosha kwa masomo ya sayansi?! Wakati hadi sasa hajaona umuhimu wa kuwa na maabara?!
 
Hivi ni kwa muda mfupi namna hii jitihada na uadilifu wa waasisi wa taifa letu umeshasahaulika namna hii! Hivi kwa namna iwayo vyovyote vile yale ambayo yalifanywa na Mwl. Nyerere kwa sasa hayapaswi kuwekewa misingi kwa wale waliomfuatia ktk kuliongoza taifa letu?

Nchi hii imepitia ktk hatua tofauti za kimaendeleo, na tena chini ya awamu tofauti za uongozi. Kuanza kutoa sifa ktk kipindi cha awamu moja huku tukipuuza misingi ya awamu zilizopita, huu utakuwa ni unafiki na hata kutaka kujipendekeza kwa malengo fulani.

Natambua ukaribu kati ya Magufuli na Mkapa. Bali isiwe sababu ya kutaka kujipendekeza na kutaka kuonekana kuwa unaunga mkono serikali hii.
Kama ulisikiliza hotuba ya Magu pale taifa wakati wa kumuaga Mkapa,nchi hii ilianza kipindi Cha BWM.Huko nyumba ilikuwa utopolo tu
 
Shida ni pale tunapoona magufuli ndie wa usahihi kuliko yoyote aliewahi kuwepo! Na alimtangulia kuwepo aliharibu sana. Utadhani huyu magufuli alizuka tu from no where, na hakua sehemu ya waharibio!!!

Hii yote ndio gharama ya kumstukiza mtu.
 
ni kweli kabisa, ila kitendo cha Magufuli kupokea nchi kilofa haina hela mpaka kuahirisha sherehe za uhuru kimagirini kusingizia usafi kumbe hakuna hela kilimtia uchungu. Ndo maana asubuhi asubuhi aliamkia wizara ya fedha kimachungumachungu na kwa kweli ana uchungu na wezi mchwa walioitafuna nchi hii na wote wenye nia hiyo.
Hamna lolote ni kiki tu
 
Back
Top Bottom