Baada ya agizo la rais la ujenzi wa maabara rais atoe pia agizo la ujenzi wa nyumba za walimu

mbeyaman

Member
Sep 28, 2013
97
28
Kumbe hakuna linaloshindikana iwapo tu rais akiwakunjia sura watendaji wake na kuonesha ukali. Tumeona viongozi kuanzia ngazi ya wizara, mkoa,wilaya mpaka kata kote nchini wakihaha huku na huku kuhakikisha wanatekeleza agizo la rais JK la kujenga maabara katika shule za kata nchini, zoezi linaendelea vizuri.

Bais mheshimiwa rais nakuomba pia toa agizo la ujenzi wa nyumba za walimu kote nchini, kwani walimu wako wanadhalilika kwa kukosa mahali pa kuishi kulingana na hazi zao. Haiwezekani mwalimu aishi kwenye mazingira magumu ya nyumba za kupanga zenye kudhalilisha taaluma yake.

Naamini ukitoa agizo hili walimu wako hawatakusahau na utamalizia vizuri urais wako. Vile vile watumishi hawa hawatakisahau chama chako cha CCM. Wataonesha ushirikiano kwa kukipa kura nyingi mwakani.
 
haliwezi kutokea,uzi huu unawahusu waalim,lakini tangu umeuweka hakuna aliyejitokeza kupaza sauti yake kuunga mkono hoja, kwahiyo maslah ya waalim yataendelea kuwa duni kwa sababu hata waalimu wenyewe hawajitambui!
 
haliwezi kutokea,uzi huu unawahusu waalim,lakini tangu umeuweka hakuna aliyejitokeza kupaza sauti yake kuunga mkono hoja, kwahiyo maslah ya waalim yataendelea kuwa duni kwa sababu hata waalimu wenyewe hawajitambui!
Mimi ni mwalimu,siwez kupaza sauti kwa kitu ambacho naona kwangu hakiwezekani na hakina tija,serikali inajua kuwa walim hawana nyumba za kuish kila mara inahorojoka,mimi binafs naona haina nia ya kujenga hizo nyumba, why nisijenge ya kwangu mwenyewe ambayo ntaishi comfortable bila kwere?yaani nikae niwaze serikali inijengee nyumba?wakat serikali inauza nyumba kila kukicha?kwa mtu mwenye maono ya mbali hawez hangaika kudai nyumba
 
Kumbe hakuna linaloshindikana iwapo tu rais akiwakunjia sura watendaji wake na kuonesha ukali. Tumeona viongozi kuanzia ngazi ya wizara, mkoa,wilaya mpaka kata kote nchini wakihaha huku na huku kuhakikisha wanatekeleza agizo la rais JK la kujenga maabara katika shule za kata nchini, zoezi linaendelea vizuri.

Bais mheshimiwa rais nakuomba pia toa agizo la ujenzi wa nyumba za walimu kote nchini, kwani walimu wako wanadhalilika kwa kukosa mahali pa kuishi kulingana na hazi zao. Haiwezekani mwalimu aishi kwenye mazingira magumu ya nyumba za kupanga zenye kudhalilisha taaluma yake.

Naamini ukitoa agizo hili walimu wako hawatakusahau na utamalizia vizuri urais wako. Vile vile watumishi hawa hawatakisahau chama chako cha CCM. Wataonesha ushirikiano kwa kukipa kura nyingi mwakani.
Kwanza hilo zoez la ujenzi wa maabara ni kazi ya waziri tu au waziri mkuu,kulikua hakuna haja kwa Jeikei kutoa agizo,
 
Kumbe hakuna linaloshindikana iwapo tu rais akiwakunjia sura watendaji wake na kuonesha ukali. Tumeona viongozi kuanzia ngazi ya wizara, mkoa,wilaya mpaka kata kote nchini wakihaha huku na huku kuhakikisha wanatekeleza agizo la rais JK la kujenga maabara katika shule za kata nchini, zoezi linaendelea vizuri.

Bais mheshimiwa rais nakuomba pia toa agizo la ujenzi wa nyumba za walimu kote nchini, kwani walimu wako wanadhalilika kwa kukosa mahali pa kuishi kulingana na hazi zao. Haiwezekani mwalimu aishi kwenye mazingira magumu ya nyumba za kupanga zenye kudhalilisha taaluma yake.

Naamini ukitoa agizo hili walimu wako hawatakusahau na utamalizia vizuri urais wako. Vile vile watumishi hawa hawatakisahau chama chako cha CCM. Wataonesha ushirikiano kwa kukipa kura nyingi mwakani.

Hawa wa madarasa, nyumba za waalimu na maabara ndiyo size yake? wa escrow je? ametoa amri ipi?
 
Siamini kama Maabara zimejengwa na hata kama zimejengwa siamini kama zitakuwa maabara kama hakuna vifaa na laboratory technicians na walimu wa sayansi.Nadhani wameongeza tu chumba cha darasa ila sio maabara.
 
Aseme kwanza amechukua hatua gani kwa wez wa escrow,kabla hajaanza kuwabana wakurugenzi,maafisa elimu,wakuu wa shule kuhusu majengo
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom