Kumbe hakuna linaloshindikana iwapo tu rais akiwakunjia sura watendaji wake na kuonesha ukali. Tumeona viongozi kuanzia ngazi ya wizara, mkoa,wilaya mpaka kata kote nchini wakihaha huku na huku kuhakikisha wanatekeleza agizo la rais JK la kujenga maabara katika shule za kata nchini, zoezi linaendelea vizuri.
Bais mheshimiwa rais nakuomba pia toa agizo la ujenzi wa nyumba za walimu kote nchini, kwani walimu wako wanadhalilika kwa kukosa mahali pa kuishi kulingana na hazi zao. Haiwezekani mwalimu aishi kwenye mazingira magumu ya nyumba za kupanga zenye kudhalilisha taaluma yake.
Naamini ukitoa agizo hili walimu wako hawatakusahau na utamalizia vizuri urais wako. Vile vile watumishi hawa hawatakisahau chama chako cha CCM. Wataonesha ushirikiano kwa kukipa kura nyingi mwakani.
Bais mheshimiwa rais nakuomba pia toa agizo la ujenzi wa nyumba za walimu kote nchini, kwani walimu wako wanadhalilika kwa kukosa mahali pa kuishi kulingana na hazi zao. Haiwezekani mwalimu aishi kwenye mazingira magumu ya nyumba za kupanga zenye kudhalilisha taaluma yake.
Naamini ukitoa agizo hili walimu wako hawatakusahau na utamalizia vizuri urais wako. Vile vile watumishi hawa hawatakisahau chama chako cha CCM. Wataonesha ushirikiano kwa kukipa kura nyingi mwakani.