Baada ya ACP Kingai kuonja joto la kutoa ushahidi, tutegemee nini toka kwa ushahidi wa IGP Sirro?

Kijichanganya ni lazima maana hii kesi Ni ya kutunga. Ni uongo hivyo maswali yatategwa kumfanya ajichanganye aonekane anasema uongo. Time will tell the whole story
Ili kujiponya na taabu yote hii ni kujibu ukweli pekee na ndio utamuweka huru.
Unajua yeye anaitwa na upande wa defense lakini akijulikana dhahiri atakuwa hostile witness, sasa lazima awe na wakati mgumu kwani atakuwa katika kiapo na analazimika kusema mambo ambayo atakuwa kinyume na mwajiri wake huku akiogopa kuiongopea mahakama chini ya kiapo
 
Sirro kuanzia olevel hadi advance alikuwa anawaburuza watu kile ni kichwa hatari angeamua kuingia kwenye siasa angekua mtu mkubwa sana
Kuwaburuza siyo tatizo ndugu yangu! Ishu ngumu ni pale mnapokuwa mashahidi wengi ambapo kila shahidi atatoa ushahidi peke yake.

Kama ni kesi ya kubambika basi ni lazima muumbuke tu. Kwa mfano, mashahidi mnaweza kujipanga ila ukikutana na wakili mzuri anakupiga swali ambalo hamkujipanga nalo. Hapo tegemea majibu tofauti kutoka kwa mashahidi!
 
Ushahidi wa IGP hauna nguvu kama ule ambao walitegemea upatikane kwa RPC Kingai ambaye ndio aliwakamata na kufungua jalada na kuwachukua maelezo yao.

IGP naona Hana jipya na ni mtu wa kujivuruga sana atapewa dozi na Kibatala mpaka Ile mimacho yake itoke.

Hiyo kesi wameshindwa mapema sana labda waifute halafu wamkamate upya waandae charge mpya.
 
Maskini Sirrow! Wakati anayasema yale, maskini wa watu hakujua kama hakimu fulani angekuja jitoa! Mategmeo yote yamepormoka... duh! Sintashangaa nkisikia "Case Dismissed".
Kuna wakati mtu anapata madaraka kwa madhara yake mwenyewe. Naisubiri kwa hamu siku hiyo i.e the Sirrow/Sorrow Day
 
Simwoni Sirro kwenye kesi hiyo!

Na kama atalazimika kuwa mbele ya mahakama hiyo, basi huo ndio utakaokuwa mwanzo wa kulitibu taifa letu kwenda mbele.
 
Sirro anahold phd ya sheria udsm
Sirro kuanzia olevel hadi advance alikuwa anawaburuza watu kile ni kichwa hatari angeamua kuingia kwenye siasa angekua mtu mkubwa sana
Siro ana shule ya sheria udsm
Unaona ulivyo 'mjinga' kiwango cha 'upumbavu'?

Mtu huna unalojua, lakini unajifanya wewe ni mjuaji.
Hali hii ndiyo iliyoenea katika jamii nzima sasa hivi, na matokeo yake ndiyo hayo tunayoyaona. Nchi inaporomoka katika kila nyanja.

Mkuu akisema "demokrasia sio Coca Cola", tunamwona kama kagundua jambo jipya ambalo halijawahi dhaniwa na yeyote! Tunashanglia!
 
20 Reactions
Reply
Back
Top Bottom