Baa wanapokuwa waungwana zaidi kuliko kanisani kwa mkosaji

comte

JF-Expert Member
Dec 11, 2011
8,222
5,946
Simu yake iliita kwa Bahati mbaya wakati wa ibada akiwa kanisani.
Mchungaji alimfokea.

Waumini walimzonga baada ya maombi ya ibada Wakati anarudi nyumbani, njia nzima mkewe aliendelea kumsema kwa kutokuwa makini Akajisikia vibaya sana, huzuni, na aibu juu. Hakutia miguu tena kanisani . Jioni yake, ili kupoteza mawazo, alikwenda bar.
Aliagiza bia, akaiweka mezani. Kwa kuwa alikuwa na mawazo mengi, akaigusa pombe ikamwagika .

Muhudumu alikuja, akampa pole kwa unyenyekevu, na akafuta meza kiustaarabu, kisha akamfuta jamaa ilipommwagikia kiunyenyekevu. Meneja wa bar ile alimpa jamaa bia ya ofa kufidia iliyomwagika, Muhudumu wa kaunta alipomletea alim'busu akim'bembeleza, "USIJALI HAKUNA AMBAYE HANA MAKOSA”

Jamaa hajawahi kukosa 'ibada' katika bar hiyo tangu siku ile.

SOMO:Unavyowatendea watu kunaweza kujenga au kuwabomoa, hasa wanapokosea.

42933065_2225799450826947_6349208505378930688_n.jpg
 
  • Thanks
Reactions: Lee
Simu yake iliita kwa Bahati mbaya wakati wa ibada akiwa kanisani.
Mchungaji alimfokea.

Waumini walimzonga baada ya maombi ya ibada Wakati anarudi nyumbani, njia nzima mkewe aliendelea kumsema kwa kutokuwa makini Akajisikia vibaya sana, huzuni, na aibu juu. Hakutia miguu tena kanisani . Jioni yake, ili kupoteza mawazo, alikwenda bar.
Aliagiza bia, akaiweka mezani. Kwa kuwa alikuwa na mawazo mengi, akaigusa pombe ikamwagika .

Muhudumu alikuja, akampa pole kwa unyenyekevu, na akafuta meza kiustaarabu, kisha akamfuta jamaa ilipommwagikia kiunyenyekevu. Meneja wa bar ile alimpa jamaa bia ya ofa kufidia iliyomwagika, Muhudumu wa kaunta alipomletea alim'busu akim'bembeleza, "USIJALI HAKUNA AMBAYE HANA MAKOSA”

Jamaa hajawahi kukosa 'ibada' katika bar hiyo tangu siku ile.

SOMO:Unavyowatendea watu kunaweza kujenga au kuwabomoa, hasa wanapokosea.

42933065_2225799450826947_6349208505378930688_n.jpg
Asikwambie mtu dudu bia tamu

Sent from my SM-N960F using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom