Baa la Njaa: Rais Magufuli, Serikali haijazuia mvua?

OKW BOBAN SUNZU

Platinum Member
Aug 24, 2011
48,776
102,138
Kutokana na hali ya kukosekana kwa mvua katika sehemu nyingi inatazamiwa kukosekana kwa chakula katika sehemu nyingi.
Mpaka Chrissmas hii bado hali ya mvua haieleweki na mazao yaliyochipua yameanza kukauka. Kama hali itaendelea kuwa hivi ni dhahiri kwamba familia nyingi hasa za wakulima zitakumbwa na baa la njaa.

Ikumbukwe kwamba wahanga wa tetemeko la Bukoba walipoonyesha kuitrgemea serikali kwa malazi na chakula walionywa kuwa serikali haikuleta tetemeko hivyo wajifunge mkanda na kujipigania. Pia wahanga wa mvua ya mawe wilayani Kahama walipewa taarifa katika ziara ya Mh.Rais kwamba serikali haitawajengea nyumba kama ilivyoahidi katika awamu ya NNE

Kwa dalili hizi za baa la njaa(Mungu tuepushe) je tutegemee nini kwa serikali?Je,tujifunge mikanda kwa kuwa serikali haijazuia mvua kama ambavyo haikuleta tetemeko huko Bukoba?
 
Hivi waliotangaza kuwa maisha ni magumu sana mabasi yamepaki hamna abiria wa kusafiri, wanajisikiaje kuona watu wamekosa mabasi ,na wengine wakidandia coaster kwa nauli mara mbili.

Aibu ya kufungia mwaka hii.
 
Punguzeni fitna, unafik na kunyoosha vidole ......jiulize ww utajipangaje kukabili baa hilo la njaa....ama unasubiri serekali ikubebe kama mtoto mdogo ...
 
Hivi waliotangaza kuwa maisha ni magumu sana mabasi yamepaki hamna abiria wa kusafiri, wanajisikiaje kuona watu wamekosa mabasi ,na wengine wakidandia coaster kwa nauli mara mbili.

Aibu ya kufungia mwaka hii.
Umeanzisha mada?
 
Hivi waliotangaza kuwa maisha ni magumu sana mabasi yamepaki hamna abiria wa kusafiri, wanajisikiaje kuona watu wamekosa mabasi ,na wengine wakidandia coaster kwa nauli mara mbili.

Aibu ya kufungia mwaka hii.
MTU akikuambia kuna njaa, usimuulize mbona umekula ugali Leo na umebakiza? Unatakiwa kujifunza kuelewa ktk mawanda mapana
 
Hivi waliotangaza kuwa maisha ni magumu sana mabasi yamepaki hamna abiria wa kusafiri, wanajisikiaje kuona watu wamekosa mabasi ,na wengine wakidandia coaster kwa nauli mara mbili.

Aibu ya kufungia mwaka hii.

Nyie sindio mnasema tunaenda kutambika?
Mkafurahia tunafilisika?
 
Hivi waliotangaza kuwa maisha ni magumu sana mabasi yamepaki hamna abiria wa kusafiri, wanajisikiaje kuona watu wamekosa mabasi ,na wengine wakidandia coaster kwa nauli mara mbili.

Aibu ya kufungia mwaka hii.
Tangu lini MTU Serious akashindwa Kwenda kwao
 
Nyie ni washirikina wakubwa. Mnaamini mambo ya kijinga kabisa. Mwenye mamlaka ya kuleta na kuzuia mvua ni Mungu pekeee
 
Kwakweli hali ningumu sana huu mwaka wakuu, mfano hapa mbeya mjini ambapo mvua huwa sio shida lakini mpaka saizi hakuna mvua ya maana kabisa
 
Ni moja ya mapigo Tisa ya Mungu kwa Watanzania baada ya kulikataa JIWE KUU LA PEMBENI.Njaa ni pigo la kwanza bado nane yanakuja.Stay tuned, usipoguswa na njaa utaguswa na mengine yanayokuja.
 
Kutokana na hali ya kukosekana kwa mvua katika sehemu nyingi inatazamiwa kukosekana kwa chakula katika sehemu nyingi.
Mpaka Chrissmas hii bado hali ya mvua haieleweki na mazao yaliyochipua yameanza kukauka. Kama hali itaendelea kuwa hivi ni dhahiri kwamba familia nyingi hasa za wakulima zitakumbwa na baa la njaa.

Ikumbukwe kwamba wahanga wa tetemeko la Bukoba walipoonyesha kuitrgemea serikali kwa malazi na chakula walionywa kuwa serikali haikuleta tetemeko hivyo wajifunge mkanda na kujipigania. Pia wahanga wa mvua ya mawe wilayani Kahama walipewa taarifa katika ziara ya Mh.Rais kwamba serikali haitawajengea nyumba kama ilivyoahidi katika awamu ya NNE

Kwa dalili hizi za baa la njaa(Mungu tuepushe) je tutegemee nini kwa serikali?Je,tujifunge mikanda kwa kuwa serikali haijazuia mvua kama ambavyo haikuleta tetemeko huko Bukoba?
Unajua kuna watz mpaka sasa wana lala njaa huku Dodoma kutokana na mvua kuzidi walikosa chakula cha kutosha kwa hiyo mvua ikiendelea kuchelewa na selekali ikatoa matamko ya ajabu ajabu tutegemee kiama
 
6 Reactions
Reply
Back
Top Bottom