Aziz Ali wa Gerezani na Mtoni Dar es Salaam

shikamoo mzee Mohamed Said.

wakati unaendelea kutuelimisha kuhusu historia isiyo na shaka ya aziz ally, abdulwahid sykes na wazee wengine mashuhuri wa dar es salaam wa wakati huo walioshiriki kwa namna moja ama nyingine katika harakati za kudai uhuru,naomba kufahamu ushiriki wa waswahili waliokuwa na asili ya kinubi toka sudani.

inasimuliwa kwamba wengi wa hawa askari shupavu wa kinubi,waliletwa tanganyika ama na muingereza au mjerumani kusaidia ktk harakati zao za kusambaza ukoloni.

pia inasimuliwa,baada ya miaka mingi kupita wakiwa ktk ardhi ya tanganyika,hawa wanubi walioa wanawake wa kiswahili na kuzaa nao watoto,pia walishiriki kikamilifu ktk vuguvugu la kudai Uhuru.

wengi wao walikuwa na makazi kariakoo na mji wa kilwa.

kama hutojali,naomba kufahamu majina yao na mchango wao ktk kudai Uhuru.

nimewahi simuliwa kuwa,wakati nyerere alipokuwa anatafuta uungwaji mkono miongoni mwa watanganyika ili awaunganishe kudai uhuru,alipokuwa anaenda kilwa,alikuwa anafikia ktk nyumba ya mzee mmoja mashuhuri wa wakati huo mwenye asili ya kinubi,mzee huyo pia alikuwa na makazi ya kudumu kariakoo.naomba kufahamu jina lake na ushiriki wake ktk kudai uhuru.
natanguliza shukrani.
Kadoda,
Wanubi walikuja Tanganyika kwa kuletwa na Wajerumani kama askari.

Ibrahim Hamisi mmoja wa waasisi wa African Association baba yake
aliingia Tanganyika kama askari wa Wajerumani akitokea Daffur.

Wakati wa utoto wangu kulikuwa na Wanubi wengi Gerezani na naikumbuka
famili ya Mzee Johari waliokuwa wakikaa Kirk Street sasa Mtaa wa Lindi.

Hawa wakiishi jirani na nyumba ya Bi. Mluguru biti Mussa mama yake Abdul
Sykes
.

Kulikuwa na Mwalimu Sakina Arab akiishi Mtaa wa Pemba huyu bi. mkubwa
alikuwa Mnubi na allikuwa na kaka yake akiitwa Mustafa.

Mwalimu Sakina alikuwa ni dada wa kuPpnga wa Abdul Sykes na ni mmoja
wa akina mama wa mwanzo kuiunga mkono TANU.

Yeye alikuwa mwalimu Al Jamiatul Islamiyya Muslim School.
Kulikuwa na koo nyingi za Kinubi Chang'ombe, Dar es Salaam na Dodoma.

Katika kitabu cha Abdul Sykes kuna kisa hiki cha Ahmed Adam Mnubi
aliyeishi Mikindani:

''Julius Nyerere, Ali Mwinyi Tambwe na Rajabu Diwani waliwasili
Mikindani kutoka Lindi siku ya Jumamosi.

Kabla ya kuwasili ujumbe huo, kazi kubwa kuliko zote waliyokuwanayo
uongozi wa TANU Mikindani ilikuwa kutafuta mahali pa kumlaza Nyerere.

Walimwendea Ahmed Adam, Mnubi mmoja tajiri na mtu wa makamo,
aliyemiliki nyumba moja ya fahari.

Nyumba hii ilikuwa ya ghorofa moja na ilijengwa kwa mawe na chokaa.
Ahmed Adam aliombwa awe mwenyeji wa Nyerere na ujumbe wake.

Nyumba hii tayari lilikuwa na kisa chake. Ilijengwa na hayati kaka yake
Ahmed Adam baada ya Vita Kuu ya Kwanza.

Kaka yake alikuwa askari wa Kinubi aliyekuwa katika jeshi la Wajerumani.
Huenda alichukuliwa Misri mwishoni mwa mwa karne ya kumi na tisa na
Wajerumani kuja Tanganyika kama mamluki katika jeshi la Wajerumani
wakati wa vita vya Maji Maji.

Baada ya vita alilipwa kiinua mgongo na serikali ya Ujerumani na kwa
kutumia fedha hizo alijenga nyumba hiyo.

Katika Vita Kuu ya Kwanza yeye alipigana katika jeshi la Wajerumani dhidi
ya Waingereza.

Baada ya vita Wajerumani wakiwa wameshindwa vita, Waingereza waliitikadi
nyumba hiyo kama mali ya adui wa himaya ya Kiingereza na kwa hiyo ilibidi
itaifishwe.

Hii ilikuwa ndiyo nyumba pekee iliyokuwa nzuri yenye kumilikiwa na Mwafrika
na kwa ajili hii haikuweza kukosa kuhusudika.

Utawala wa Waingereza ulikuwa katika taratibu ya kuitaifisha nyumba hiyo
wakati ilipofahamika kwamba serikali isingeweza kufanya hivyo kwa sababu ya
kifungu cha sheria ambacho kilisema kuwa mali ya Waafrika waliokuwa wakitumika
katika majeshi ya watawala wao haiwezi kutaifishwa.

Hii ilinusuru nyumba hiyo na hivyo ilibakia mikononi mwa mwenyewe mpaka alipofariki
na nyumba hiyo ikaja kuwa katika miliki ya mdogo wake, Ahmed Adam.

Ahmed Adam alikubali kumpokea Nyerere na ugeni wake nyumbani kwake.
Nyumba hiyo ilikuja kuwa tawi la kwanza la TANU Mikindani.

Siku hiyo hiyo ya Jumamosi, usiku Nyerere aliitisha mkutano na wanachama kama
thelathini hivi walihudhuria.

Nyerere aliwaeleza kwa ufupi juu ya ile safari yake ya UNO na hali ya siasa kwa
ujumla mjini Dar es Salaam.

Nyerere aliwahakikishia waskilizaji wake kuwa kulikuwa na uwezekano mkubwa
sana kuwa Tanganyika itakuwa huru katika uhai wao.
 
Kadoda,
Wanubi walikuja Tanganyika kwa kuletwa na Wajerumani kama askari.

Ibrahim Hamisi mmoja wa waasisi wa African Association baba yake
aliingia Tanganyika kama askari wa Wajerumani akitokea Daffur.

Wakati wa utoto wangu kulikuwa na Wanubi wengi Gerezani na naikumbuka
famili ya Mzee Johari waliokuwa wakikaa Kirk Street sasa Mtaa wa Lindi.

Hawa wakiishi jirani na nyumba ya Bi. Mluguru biti Mussa mama yake Abdul
Sykes
.

Kulikuwa na Mwalimu Sakina Arab akiishi Mtaa wa Pemba huyu bi. mkubwa
alikuwa Mnubi na allikuwa na kaka yake akiitwa Mustafa.

Mwalimu Sakina alikuwa ni dada wa kuPpnga wa Abdul Sykes na ni mmoja
wa akina mama wa mwanzo kuiunga mkono TANU.

Yeye alikuwa mwalimu Al Jamiatul Islamiyya Muslim School.
Kulikuwa na koo nyingi za Kinubi Chang'ombe, Dar es Salaam na Dodoma.

Katika kitabu cha Abdul Sykes kuna kisa hiki cha Ahmed Adam Mnubi
aliyeishi Mikindani:

''Julius Nyerere, Ali Mwinyi Tambwe na Rajabu Diwani waliwasili
Mikindani kutoka Lindi siku ya Jumamosi.

Kabla ya kuwasili ujumbe huo, kazi kubwa kuliko zote waliyokuwanayo
uongozi wa TANU Mikindani ilikuwa kutafuta mahali pa kumlaza Nyerere.

Walimwendea Ahmed Adam, Mnubi mmoja tajiri na mtu wa makamo,
aliyemiliki nyumba moja ya fahari.

Nyumba hii ilikuwa ya ghorofa moja na ilijengwa kwa mawe na chokaa.
Ahmed Adam aliombwa awe mwenyeji wa Nyerere na ujumbe wake.

Nyumba hii tayari lilikuwa na kisa chake. Ilijengwa na hayati kaka yake
Ahmed Adam baada ya Vita Kuu ya Kwanza.

Kaka yake alikuwa askari wa Kinubi aliyekuwa katika jeshi la Wajerumani.
Huenda alichukuliwa Misri mwishoni mwa mwa karne ya kumi na tisa na
Wajerumani kuja Tanganyika kama mamluki katika jeshi la Wajerumani
wakati wa vita vya Maji Maji.

Baada ya vita alilipwa kiinua mgongo na serikali ya Ujerumani na kwa
kutumia fedha hizo alijenga nyumba hiyo.

Katika Vita Kuu ya Kwanza yeye alipigana katika jeshi la Wajerumani dhidi
ya Waingereza.

Baada ya vita Wajerumani wakiwa wameshindwa vita, Waingereza waliitikadi
nyumba hiyo kama mali ya adui wa himaya ya Kiingereza na kwa hiyo ilibidi
itaifishwe.

Hii ilikuwa ndiyo nyumba pekee iliyokuwa nzuri yenye kumilikiwa na Mwafrika
na kwa ajili hii haikuweza kukosa kuhusudika.

Utawala wa Waingereza ulikuwa katika taratibu ya kuitaifisha nyumba hiyo
wakati ilipofahamika kwamba serikali isingeweza kufanya hivyo kwa sababu ya
kifungu cha sheria ambacho kilisema kuwa mali ya Waafrika waliokuwa wakitumika
katika majeshi ya watawala wao haiwezi kutaifishwa.

Hii ilinusuru nyumba hiyo na hivyo ilibakia mikononi mwa mwenyewe mpaka alipofariki
na nyumba hiyo ikaja kuwa katika miliki ya mdogo wake, Ahmed Adam.

Ahmed Adam alikubali kumpokea Nyerere na ugeni wake nyumbani kwake.
Nyumba hiyo ilikuja kuwa tawi la kwanza la TANU Mikindani.

Siku hiyo hiyo ya Jumamosi, usiku Nyerere aliitisha mkutano na wanachama kama
thelathini hivi walihudhuria.

Nyerere aliwaeleza kwa ufupi juu ya ile safari yake ya UNO na hali ya siasa kwa
ujumla mjini Dar es Salaam.

Nyerere aliwahakikishia waskilizaji wake kuwa kulikuwa na uwezekano mkubwa
sana kuwa Tanganyika itakuwa huru katika uhai wao.

Bahati mbaya saina taarifa za huyo mzee wetu wa KIlwa.
 
asante mzee Mohamed Said kwa kupoteza mda wako kuandika article japo fupi,kuhusu wanubi na harakati za kudai Uhuru wa Tanganyika.

kama una kisa kingine kizuri kuhusu hawa wanubi wa kariakoo na kudai Uhuru,basi usisite kutuwekea hapa.

nikipata wasaa wa kutosha,nitarejea na swali lingine.
 
Mzee wangu Mohamedi Said nakualika ufike katika kijiji chetu cha Moa, Tanga, kijiji maarufu sana kwa mwambao wa kaskazini mwa Tanga, sikua nikijua kuwa Aziz Alli alitokea kijijini kwetu, Subhana Llaah, njoo kuna mzee mmoja ni babu yangu amezaliwa kunano mwaka 1926 au 1927. Bado yu hai na nguvu tele, ana mambo mengi sana unaweza kustafid.
Naam hapo ndipo atalipata chimbuko la Azizi Alli
 
Mkuu hebu jaribu kupinga hicho unachosema ni uongo kwa kuweka wewe ukweli wako, bila hivyo tutakutafsiri kua una chuki fulani tu na wivu usio na maana,huwezi kusifiwa kwa kukashifu watu humu bali tutakusifu kama utajenga hoja ili ueleweke kuliko kukashifu watu usiowajua kisa tu coz upo nyuma ya keyboard,ustaarabu hauuzwi dukani,tujenge kuheshimiana ili tuelimike sote,

One love.
Wewe basi nawe ni Shida inamaana hujasoma tokea mwanzo nini kilichofanya huyu mzee abishiwe ukiwa mvivu Wa kusoma basi utaamini kilichoandikwa ni sawa.. So bora usome alichoandika huyu na nilochopinga na maswali aliyoulizwa na member humu hadi akaanza madharau baada ya kuonwa hawezi kikubali kukanusha uongo... Na pia kasome maandiko yake yote ni udini as if anataka kuonesha Uhuru Wa Tanganyika umeletwa na Uislam kitu hicho asahau... Record zipo uingereza na Dunia inajua Nyerere ndie na sio wauza kahawa wabulundi hawa
 
Wewe basi nawe ni Shida inamaana hujasoma tokea mwanzo nini kilichofanya huyu mzee abishiwe ukiwa mvivu Wa kusoma basi utaamini kilichoandikwa ni sawa.. So bora usome alichoandika huyu na nilochopinga na maswali aliyoulizwa na member humu hadi akaanza madharau baada ya kuonwa hawezi kikubali kukanusha uongo... Na pia kasome maandiko yake yote ni udini as if anataka kuonesha Uhuru Wa Tanganyika umeletwa na Uislam kitu hicho asahau... Record zipo uingeleza na Dunia inajua Nyerere ndie na sio wauza kahawa waburundi hawa
Duduwasha,
Mimi nimetiwa moyo sana na ujasiri wako kuwa ingawa una tatizo katika
kuandikalakini hilo halikuzuii kufanya mjadala na mimi.

Nakupongeza.

Umeandika fikra zako ila kasoro umehamaki na ndiyo unakuja na hizo lugha
za, ''huyu mzee,'' ''wauza kahawa,'' na ''Waburundi,''

Muhimu sana utie juhudi ujifunze kuandika vyema.
 
Hamza Azizi akiwa IGP alikataa Amri ya Amiri Jeshi Julius Kambarage alieamuru Kiongozi Mkuu wa Waislam wa Wakati huo Al marhum Sheikh Hassan Bin Ameir akamatwe na kupelekwa kuishi Zanzibar bila ya kutoa sababu!

Nyerere akaamuru Usalama wa Taifa wa wakati huo ndio wafanye Kazi hiyo bila ya kushirikisha Jeshi la Polisi!
Ila nyerere nae kafanya mengi.kuna mzee kanihadithia baada ya kupigana vita vya kagera wakapelekwa Zanzibar. Wakawekwa sero.wengine wakakimbia.
 
Duduwasha usiandike ukiwa umeghadhibika. Hapa nakusoma lakini nashindwa kupata mtiririko mzuri kufanya mjadala.

Sijasubiri Nyerere afariki ndiyo nisahihishe historia ya TANU.

Nimeandika Nyerere akiwa hai na hili nishalieleza hapa jamvini labda kwa kuwa wewe ni mgeni na maandishi yangu ndiyo hujui.

Kuna "series" zangu kuanzia 1988 nikiandika na Africa Events (London) makala ya kwanza kuandika historia ya TANU tofauti na ile rasmi ya Chuo Cha Kivukoni toleo zima liliondolewa katika "circulation."

Nimechapa kitabu cha maisha ya Abdul Sykes 1998 Nyerere alikuwa hai.

Vizuri kabla ya kuingia mjadala mtu ukafanya utafiti lau kidogo kujua unachokizungumza kuondoa kuonekana hujui kitu.

Laiti ungelifanya hivyo ungejua kuwa nilianza kuandika siku nyingi sana.

Tutazungumza zaidi nina mengi.
Tatizo historia amesimuliwa.ila wewe ulikuwepo.haujasimuliwa,ilo ndo tatizo.
 
Hoja zako umezigeuza ushakuwa popo au huyo mzee ni bwana wako nini? Historia zishawekwa na wenyewe na zipo hivyo kutaka kuja kudanganywa kipumbavu akadanganye wanawe na wajukuu zake na wewe pia mmoja wao.. So me sina kashfa hoja zangu zinasimama wewe ndio una utoto kwangu... Pia huna hoja za kukufanya kuchomeka hoja dhidi yangu juu ya upotoshaji Wa history inayoletwa na Mo Said
Mmmmh.imechezewa Bible. Sembuse historia.
 
Duduwasha,
Mimi nimetiwa moyo sana na ujasiri wako kuwa ingawa una tatizo katika
kuandikalakini hilo halikuzuii kufanya mjadala na mimi.

Nakupongeza.

Umeandika fikra zako ila kasoro umehamaki na ndiyo unakuja na hizo lugha
za, ''huyu mzee,'' ''wauza kahawa,'' na ''Waburundi,''

Muhimu sana utie juhudi ujifunze kuandika vyema.
Haha ndio hoja yako ati utasababisha tuache kuona madhaifu yaki ??? Eti sijui kuandika so what? OK sijui kuandika lakini umeelewa jinsi nilivyokuanika na uongo wako... Hizo reds ulizo mark zingine zimesababishwa na simu nayotumia haswa kwenye harufi kubwa mwanzo so huna hoja zaidi sasa unaleta viroja mnafiki akizeeka huwa mcha.w.i ndipo uelekeo... Na pia kiswahili kisha kuwa proved hakina faida zaidi ya kumfanya mtu abakie level ya chini kimaendeleo...

Wewe unayejua kuandika hapo nilipo mark ni neno moja hilo? Naweza pitia nukuu zako humu nikakuonesha kila ulilokosea ..lete story za kweli na uache kujaza uongo usio hitajika.. Watu wanapenda kupata Elimu haswa za Historia lakini sio kuchonekea na mambo yasiyohusu..
 
Hata Koran zilikuwa na waandishi wawili ikachaguliwa ya muandishi mmoja.
Tatizo lako wewe kiumbe nimeshaanza kuliona,kumbe yote haya yanatokana na chuki zako tu kwa dini ile eeh!

Hujajishtukia tu kua umegeuka kituko kwenye hii thread?
Badilika Mkuu,sio kwa vile uko nyuma ya key board au kwa vile unajibizana na watu usio wajua ndio utumie lugha za kashfa,
usifikiri kua watu hawajui kutukana kama wewe ila hii ni forum tunajifunza na hatuko hapa ili kutukanana,

Mzee wa watu anakujibu kwa busara na uvumilivu wa hali ya juu lakini umeshindwa kuheshimu wenzako, Badilika mkuu,
 
Haha ndio hoja yako ati utasababisha tuache kuona madhaifu yaki ??? Eti sijui kuandika so what? OK sijui kuandika lakini umeelewa jinsi nilivyokuanika na uongo wako... Hizo reds ulizo mark zingine zimesababishwa na simu nayotumia haswa kwenye harufi kubwa mwanzo so huna hoja zaidi sasa unaleta viroja mnafiki akizeeka huwa mcha.w.i ndipo uelekeo... Na pia kiswahili kisha kuwa proved hakina faida zaidi ya kumfanya mtu abakie level ya chini kimaendeleo...

Wewe unayejua kuandika hapo nilipo mark ni neno moja hilo? Naweza pitia nukuu zako humu nikakuonesha kila ulilokosea ..lete story za kweli na uache kujaza uongo usio hitajika.. Watu wanapenda kupata Elimu haswa za Historia lakini sio kuchonekea na mambo yasiyohusu..
Duduwasha,
Umehamaki.
Unatukana.

Tukubali kuwa mimi naandika uongo.
Sasa hebu lete ukweli usomwe kama ninavyosomwa mimi.
 
Duduwasha,
Mimi nimetiwa moyo sana na ujasiri wako kuwa ingawa una tatizo katika
kuandikalakini hilo halikuzuii kufanya mjadala na mimi.

Nakupongeza.

Umeandika fikra zako ila kasoro umehamaki na ndiyo unakuja na hizo lugha
za, ''huyu mzee,'' ''wauza kahawa,'' na ''Waburundi,''

Muhimu sana utie juhudi ujifunze kuandika vyema.

Maalim Mohamed Saidi
Namuomba MwenyeziMungu anijaalie niwe Na HIKMA ZAKO japo kidogo.
Uzidishiwe baraka,Hikma Na kila la kheri
 
Tatizo lako wewe kiumbe nimeshaanza kuliona,kumbe yote haya yanatokana na chuki zako tu kwa dini ile eeh!

Hujajishtukia tu kua umegeuka kituko kwenye hii thread?
Badilika Mkuu,sio kwa vile uko nyuma ya key board au kwa vile unajibizana na watu usio wajua ndio utumie lugha za kashfa,
usifikiri kua watu hawajui kutukana kama wewe ila hii ni forum tunajifunza na hatuko hapa ili kutukanana,

Mzee wa watu anakujibu kwa busara na uvumilivu wa hali ya juu lakini umeshindwa kuheshimu wenzako, Badilika mkuu,

CleverKING
huyo duduwasha ana hasira Kwa sababu Maalim Mohamed anatufungua macho na historia ambayo wengi wetu tulikuwa hatujui.
Nimesoma historia ya Tanganyika nilipokuwa shule ambazo Sasa naziona zilikuwa nusu kweli.Labda Alikuwa miongoni mwa waandishi
 
Hivi huyo Kleist Sykes alilitoa wapi hilo jina?

Kwa sababu naona kama vile ni jina la kigeni hivi....
Huyo alikuwa mhamiaji mateka wa kivita toka Afrika Kusini, kabila lake ni Mzulu......
Kibaya nikuwa Mohamed Said anamfifisha Cesil Matola kwamba hastahili kupewa jina la mtaa kwakuwa si mdarisalamu lakini hapohapo anajisahau na kumtaja Mzee Azizi Ali ambae ana mtaa kabisa na hakuwa kiongozi wa kisiasa wala harakati, kibaya zaidi hana nasaba za Dar Es Salaam, kwakuwa kwao ni Tanga.

Cesil Matola muyao alikuwa rais wa kwanza wa AA, na mpaka leo hakumbukwi popote katika historia ya Dar wala historia ya CCM....
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom