Azimio jipya la walalahoi

MAMMAMIA

JF-Expert Member
Feb 26, 2008
3,811
1,603
Angalia Azimio la Arusha, 1967.
"TUMEONEWA KIASI CHA KUTOSHA, TUMENYONYWA KIASI CHA KUTOSHA, TUMEPUUZWA KIASI CHA KUTOSHA. UNYONGE WETU NDIO ULIOTUFANYA TUONEWE, TUNYONYWE NA KUPUUZWA. SASA TUNATAKA MAPINDUZI, MAPINDUZI YATAKAYOTUFANYA TUSIONEWE, TUSINYONYWE NA TUSIPUUZWE TENA," (AZIMIO LA ARUSHA, 1967).
Azimio hili liishia pale lilipopitishwa Azimio la Zanzibar, na tokea wakati huo, miaka 43 imepita na bado tunaendelea KUONEWA, KUNYANYASWA na KUPUUZWA. Kinachouma zaidi ni kuwa wanaotuonea, kutunyanyasa na kutupuuza si wakoloni wa Ulaya bali Watanzania wenzetu ambao tumewaamini kuwakabidhi madaraka ya dola (Ingawaje mara hii ya mwisho wamechakachachua waziwazi na wapo si kwa ridhaa ya Watanzania.
Kwa hiyo wana JF, Watanzania na wote walio na uchungu na Tanzania, tunahitaji kuwa na Azimio Jipya la Walalahoi, ambalo pamoja na mikakati mengine, litasomeka:

"TUMECHAKACHULIWA KIASI CHA KUTOSHA, TUMEIBIWA KIASI CHA KUTOSHA, TUMEPUUZWA KIASI CHA KUTOSHA. UAMINIFU WETU NDIO ULIOTUFANYA TUCHAKACHULIWE, TUIBIWE NA KUPUUZWA. SASA TUNATAKA KATIBA, KATIBA MPYA ITAKAYOTUFANYA TUSICHAKACHULIWE, TUSIIBIWE NA TUSIPUUZWE TENA," (AZIMIO LA WALALAHOI, 2010).
 
Ni nani anaekuonea, sisi ni wa Tanzania na tupo tayari kukusaidia, ikiwa tu utatubainishia ni nani ane-kunyonya na kukuonea. Haya lete vitu.
 
Ni nani anaekuonea, sisi ni wa Tanzania na tupo tayari kukusaidia, ikiwa tu utatubainishia ni nani ane-kunyonya na kukuonea. Haya lete vitu.

Alosema w(a)meonewa ni Nyerere, mimi ninasema TUMECHAKACHULIWA (kura), TUMEIBIWA (mali zetu) na TUNAPUUZWA (matakwa yetu ya Katiba hayasikilizwi).
 
unalipakodi kweli wewe maana wengu wenu hamlipi kodi hafu mtaka maendeleo si jui maendeleo gani wakati hamchai hata kidogo?
 
Ccm imewanyonya watanzania, mafisadi wa ccm, masultani madikiteta wanaongangania kutawala, sio uongo tunanyanyasika na tunaonewa saana anaepinga basi na yeye ni sehem ya wanyonyaji wnaoinyonya tanzania
 
Alosema w(a)meonewa ni Nyerere, mimi ninasema TUMECHAKACHULIWA (kura), TUMEIBIWA (mali zetu) na TUNAPUUZWA (matakwa yetu ya Katiba hayasikilizwi).

1) Nyerere anasema "w(a)meonewa" wakati yeye ndie aliekuwa anaonea watu? kahamisha watu kutoka makazi yao kupeleka vijiji vya ujamaa, walioliwa na simba, waliogongwa na nyoka, waliokosa matibabu wakafia maporini. Kama si kuonea huko ni nini?

2) Nipe ushahidi wa kura zilizochakachuliwa na mimi ntawapeleka mahakamani hao wachakachuaji.

3) Umeibiwa mali zako na nani? unasema "zetu", wewe na nani? mimi sijaibiwa!

4) "TUNAPUUZWA (matakwa yetu ya Katiba hayasikilizwi", ni nani anepuuza swala muhimu kama hili? wakati Serikali ya CCM ilisha liundia tume na tume imesema katiba mpya ni muhimu na lazima. Sasa nani aliopuuza> bwana Mkapa hajatimiza hilo, sasa ni zamu ya JMK, na hilo ongea na Mbunge wako tu, afikishe mswaada Bungeni,mbona ni jambo zuri tu hili? nani aliepinga hili? nani ambae kapuuza kukusikiliza kwa kitu muhimu namna hii?
 
Ccm imewanyonya watanzania, mafisadi wa ccm, masultani madikiteta wanaongangania kutawala, sio uongo tunanyanyasika na tunaonewa saana anaepinga basi na yeye ni sehem ya wanyonyaji wnaoinyonya tanzania

Hivi< wewe ungenyonywa au kunyanyaswa na CCM< saa hizi ungekuwa unakaa starehe una post maupuuzi yako kwenye JF? subuuutu!
 
Ni nani anaekuonea, sisi ni wa Tanzania na tupo tayari kukusaidia, ikiwa tu utatubainishia ni nani ane-kunyonya na kukuonea. Haya lete vitu.

mafisad ambao bila shaka wewe una mahusiano nao ya karibu ndo mliotunyonya na kutuonea na ninyi kuendelea kununua majumba ya mabilion ulaya, kuhifadh hela zenu kwny visiwa, kutuingiza kwny mikataba mibovu na kutupeleka ICC kujivutia 185b_yaan na hasira na niny_utawala ukiangushwa mhame nchi
 
1) Nyerere anasema "w(a)meonewa" wakati yeye ndie aliekuwa anaonea watu? kahamisha watu kutoka makazi yao kupeleka vijiji vya ujamaa, walioliwa na simba, waliogongwa na nyoka, waliokosa matibabu wakafia maporini. Kama si kuonea huko ni nini?

2) Nipe ushahidi wa kura zilizochakachuliwa na mimi ntawapeleka mahakamani hao wachakachuaji.

3) Umeibiwa mali zako na nani? unasema "zetu", wewe na nani? mimi sijaibiwa!

4) "TUNAPUUZWA (matakwa yetu ya Katiba hayasikilizwi", ni nani anepuuza swala muhimu kama hili? wakati Serikali ya CCM ilisha liundia tume na tume imesema katiba mpya ni muhimu na lazima. Sasa nani aliopuuza> bwana Mkapa hajatimiza hilo, sasa ni zamu ya JMK, na hilo ongea na Mbunge wako tu, afikishe mswaada Bungeni,mbona ni jambo zuri tu hili? nani aliepinga hili? nani ambae kapuuza kukusikiliza kwa kitu muhimu namna hii?
1. Kumbe na wewe pia ulionja kisago cha Nyerere? Nyerere huyu huyu aliyeanzisha CCM ambayo leo unaitetea? Nimefurahi angalau kwa kulielewa hilo.
2 & 3. Mtu anaweza akawa na macho bado akawa haoni, na hii inakuja pale inaposemwa "mwenye kupenda haoni".
4. Kwa kuwa inaonesha wewe mwenzangu ni mdau (angalau shabiki) naomba ahadi yako, tusubiri miaka mingapi kuona katiba inaandikwa upya?
 
Back
Top Bottom