Azim Dewji: Tunasema kwamba, kazi kubwa ya mkuu wa Dini ni kuongoza waumini wake sio kuwapotosha, unazungumza maneno ya kuwapotosha waumini na kuleta taharuki kwenye Jamii, hiyo haifai kabisa na isiendelee kufanyika hivyo, sisi hatutakubali.
Kwa njia moja au nyingine unawatukana waliobobea kwenye fani hiyo kwamba kamati iliundwa, waliofanya utafiti wewe unawaona hawana akili. Saa nyingine naweza kusema labda wewe ndio huna akili ya sayansi, wewe labda una akili ya kuhubiri peke yake kwa hiyo usijaribu kuwatukana wenzako.
Mwisho Azim amemwambia mchungaji Gwajima amuheshimu Rais na kiongozi wa chama ambacho kimemlea na kumpatia ubunge kwani bila chama cha CCM asingepata ubunge na wengine kama yeye hajampigia kura Gwajima bali alipigia chama.
PIA, Soma> Askofu Gwajima: Ni jambo baya sana kuwapa Chanjo ya Corona Wanajeshi, Polisi na watu wa Usalama
ana akili ya kuhubiri majitu yasiyojitambua, misukule, majitu yanapumua lakini ni kama maiti, hayajitambui