Azam TV: Mapinduzi ya Zanzibar kutoka kumbukumbu zilizozikwa

Paskali,
Unasema wewe umekuta neno tukufu linatumiwa kueleza mapinduzi
kwa hiyo hukuona sababu ya kutaka kujua kwa nini mapinduzi yaitwe
''matukufu.''

Hivi wewe kama mwandishi hutaki ''to go an extra mile,'' katika uandishi
wako ukataja kujua zaidi?

Nimeeleza kuwa mapinduzi hayawezi kuwa na utukufu je unakubaliana
na sababu nilizoweka?

Unajaribu na kujitahidi kukwepa lakini ukweli ni kuwa unayapamba mauaji
kwa chuki uliyokuwanayo.

Post zako zote hapa ni shahidi.
Unasema wewe hukuwepo wala mimi sikuwapo.

Umekosea.

Mimi nilikuwapo na baba yangu alikuwa na uhusiano mkubwa sana na
jamaa wengi kutoka Zanzibar toka miaka ya 1950s au kabla.

Kwenye varanda ya nyumbani kwetu ukutani kulikuwa na picha moja
waki vijana watatu.

Katikati alikuwa baba yangu, Salum Abdallah na pembeni alikuwa Jaha
Ubwa
na Abdulaziz Twala.

Picha hii ilipigwa kabla ya mapinduzi.

Baada ya mapinduzi Jaha na Twala waliuliwa na baba yangu hakuweza
kuitazama hii picha akaitungua ukutani na sijui iko wapi.

Nina kumbukumbu ya ''June Riots,'' za 1963 kwa kuona katika gazeti la
Ngurumo nyumbani ingawa sikuwa nafahamu kwa uhakika nini khasa
kilikuwa kinaendelea huko Unguja na wazee wakizungumza nami nikisikia
mazungumzo yao.

Watu wa Dar es Salaam walikuwa na uhusiano wa karibu sana na watu wa
Zanzibar kwa hiyo vurugu zilizokuwa zinatokea visiwani zikiwagusa sana.

Mapinduzi yametokea wazee walikuwa na shauku ya kutaka kujua hali ya
jamaa zao kama wako salama au vipi.

Hii ndiyo yangu mimi kuwa ingawa sikuwa Zanzibar lakini nilikuwa najua kuwa
yametokea mapinduzi visiwani.

Katika jamaa zetu waliouawa nimekutajia Jaha Ubwa na Abdulaziz Twala
lakini mauaji na mateso kwa baadhi ya jamaa zetu hayakuisha hapo na nilikuwa
wakati mwingine nikimsikia mzee akizungumza kwa sauti zay chini akiulizia mtu
fulani na fulani na inapokuwa habari hazikuwa nzuri akiinamsiha kichwa chini.

Wakati ule nilikuwa na umri wa miaka 14.

Nadhani unaweza kuona kwa haya machache ni kiasi gani wengi wetu tumeathirika
na tunasikitika sana tunapokusoma.
Hivi huyu pascal anahadhi ya kuitwa mwandishi kweli! Maana inaonekana huwa anahoja nyepesi na zenye lengo La ubishi na kubuy time tu

Au ndo uandishi wa mtandaoni(kila MTU mwandishi)!?

Embu leta kazi zako zinazotokana na primary source km mzee Mohammed anavyofanya
 
Pasco anazingua yeye source zake anakwambia "nimehadithiwa" hahaaa yan mwandishi zima anatupa source great thinker za kusimuliwa, mwenzako anatupa vitabu. Ameenda mbaaali anatupa link za maandishi yake ya nyuma! Pasco Kuwa criaz bn. Maandiko yako yanawezaje kuwa biography and references tena hata ithibati hayana.
 
Azam TV inaleta revisionist theory za hawa waarabu .Mapinduzi ya Zanzibar ni tukio lililompa mwafrika uhuru baada ya mamia ya miaka ya kutawaliwa na kufanywa mtumwa na fe hdhuri mwarabu.

Sasa inashangaza bado kuna watu leo hii wanatetea Unyama wa waarabu.
 
Kwenye kipindi cha Tuongee asubuhi cha Star TV, siku ya Mapinduzi, alialikwa mzee Mkinga kujadili kama dhima ya Mapinduzi imefikiwa.
Kikubwa alisema kuwa imefikiwa kwa kuwa hakuna tena watwana na kila mtu ana haki mbele ya sheria, achilia mbali maendeleo makubwa yaliyoletwa na serikali zote hizo baada ya Mapinduzi.
Ila mzee Mkinga aliongeza kitu kimoja kuwa yapaswa waandishi wanaopotosha Mapinduzi yale washughulikiwe na maandishi ya vitabu vyao yasiruhusiwe kokote ndani ya JMT.

Alitolea mfano wa kitabu alichokuwa nacho mkononi cha" Kwa heri ukoloni cha mwandishi Ghasani.
Kwa maoni yake hao kina Ghasani na kina Mudi wote waangaliwe vyema maana maandishi yao yana matokeo hasi
 
Hivi huyu pascal anahadhi ya kuitwa mwandishi kweli! Maana inaonekana huwa anahoja nyepesi na zenye lengo La ubishi na kubuy time tu

Au ndo uandishi wa mtandaoni(kila MTU mwandishi)!?

Embu leta kazi zako zinazotokana na primary source km mzee Mohammed anavyofanya
Kwa humu jf, mimi ni mwandishi tuu wa mtandaoni, na specialization yangu sio uandishi, ila kwa kule kwenye speciality yangu na mimi pia ni nguli kama alivyo Mzee MSA katika uandishi wa vitabu.

Paskali
 
Kwenye kipindi cha Tuongee asubuhi cha Star TV, siku ya Mapinduzi, alialikwa mzee Mkinga kujadili kama dhima ya Mapinduzi imefikiwa.
Kikubwa alisema kuwa imefikiwa kwa kuwa hakuna tena watwana na kila mtu ana haki mbele ya sheria, achilia mbali maendeleo makubwa yaliyoletwa na serikali zote hizo baada ya Mapinduzi.
Ila mzee Mkinga aliongeza kitu kimoja kuwa yapaswa waandishi wanaopotosha Mapinduzi yale washughulikiwe na maandishi ya vitabu vyao yasiruhusiwe kokote ndani ya JMT.

Alitolea mfano wa kitabu alichokuwa nacho mkononi cha" Kwa heri ukoloni cha mwandishi Ghasani.
Kwa maoni yake hao kina Ghasani na kina Mudi wote waangaliwe vyema maana maandishi yao yana matokeo hasi
Kwa kiwango cha mkinga hiyo ilikuwa mada kubwa kwake maana hana uweledi NATO sana sana itakuwa alitoka povu tu
 
Nashindwa kufahamu sikuzote. Kwanini wabongo wanakua na hasira na uarabu na kuchukia usultani kuliko hata ao wazanzibari wenyewe. Ikiwa wazanzibari wenyewe hawana tatizo na uarabu wala usultani. Na wala hawana mpango na mapinduzi. Kwanini wabongo wao ndo wanakua wanaumwa na mapinduzi na kua na chuki na hasira dhidi ya uarabu na usultani?
 
Hawa Azam TV wanapochagua mzungumzaji kwenye issue sesitive kama hii ya Mapinduzi ya Zanzibar, walibidi walete watu antogonistic, ili kuzuia umma wote wa Watanzania kudanganywa na warongo wale wale kwa kutumia urongo ule ule kuwa eti Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, hayakuwa mapinduzi bali uvamizi!. Mwandishi ni vizalia vya waliopinduliwa, msimulizi ni nasaba ya waliopinduliwa, objectivity, impartiality, fairness and balance itatoka wapi zaidi ya bias tupu mwanzo mwisho?!.

Tangu mwanzo humu jf, tumesema wazi maandishi ya baadhi ya waandishi wa mapinduzi yale ni urongo!, sasa unapowaleta mashabiki wa urongo, kuja kutetea maandishi ya hao warongo, matokeo yake ni urongo juu ya urongo!. Okello mwenyewe ameandika kitabu ya kilichotokea!, leo asubuhi nimeangalia TBC shuhuda mmoja wa mapinduzi yale aliyepigana ametoa ushuhuda wa kilichotokea na sio uongo huu wa wasimuliwaji!, ameeleza jinsi utawala dhalimu wa Sultani ulivyokuwa ukiwatenda Waarika!.

Ili tusiendelee kubishania urongo, kwa nini baadhi ya mashujaa wa mapinduzi yale walio hai, wasihojiwe na mambo ya mapinduzi yale kuwekwa sawa?!.

Pasco
Nawatakia kumbukumbu njema ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar yaliyovikomboa visiwa hivi.
P
 
Nawatakia kumbukumbu njema ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar yaliyovikomboa visiwa hivi.
P
Leo tarehe 12 January ni Sikukuu ya Mapinduzi ya Zanzibar, nachukua nafasi hii kuwatakia nyote heri na fanaka za Mapinduzi na kukutakieni maadhimisho mema ya sherehe ya kumbukumbu ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar kwa watakao shereheka kwa wale wenye kumbukumbu njema, na kwa vile Mapinduzi Matukufu yale pia yaliandamana na umwagaji damu, natoa pole kwa wenye kumbukumbu chungu.
P
 
Hawa Azam TV wanapochagua mzungumzaji kwenye issue sesitive kama hii ya Mapinduzi ya Zanzibar, walibidi walete watu antogonistic, ili kuzuia umma wote wa Watanzania kudanganywa na warongo wale wale kwa kutumia urongo ule ule kuwa eti Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, hayakuwa mapinduzi bali uvamizi!. Mwandishi ni vizalia vya waliopinduliwa, msimulizi ni nasaba ya waliopinduliwa, objectivity, impartiality, fairness and balance itatoka wapi zaidi ya bias tupu mwanzo mwisho?!.

Tangu mwanzo humu jf, tumesema wazi maandishi ya baadhi ya waandishi wa mapinduzi yale ni urongo!, sasa unapowaleta mashabiki wa urongo, kuja kutetea maandishi ya hao warongo, matokeo yake ni urongo juu ya urongo!. Okello mwenyewe ameandika kitabu ya kilichotokea!, leo asubuhi nimeangalia TBC shuhuda mmoja wa mapinduzi yale aliyepigana ametoa ushuhuda wa kilichotokea na sio uongo huu wa wasimuliwaji!, ameeleza jinsi utawala dhalimu wa Sultani ulivyokuwa ukiwatenda Waarika!.

Ili tusiendelee kubishania urongo, kwa nini baadhi ya mashujaa wa mapinduzi yale walio hai, wasihojiwe na mambo ya mapinduzi yale kuwekwa sawa?!.

Pasco
Wana bodi, japo tuko kwenye harakati za kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Rais na Wabunge, kuna swali linanitatiza kuhusu Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, ambapo majibu yake sahihi, pia yanaweza kuwa ni kiashiria tosha cha mshindi wa urais wa Zanzibar, iwapo uchaguzi utakuwa huru na wa haki.

Swali hili lahusu ukweli haswa kuhusu Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar ya Januari 12, 1964, baada ya kuibuka kwa kitabu kingine kiitwacho "Kwaheri Ukoloni, Kwaheri Uhuru"
View attachment 2077603
kilichoandikwa na Mwanazouni wa Zanzibar, Dr. Harith Ghassany, kama kilivyofanyiwa mapitio na mwandishi Mohamed Said kwenye gazeti la Al-Nuur la leo.

Ghasanny anasema kumbe Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar yalitekelezwa na askari mamluki wa Kimakonde (Wakata Mkonge) ambao waliongozwa na Mzee Mohamed Omar Mkwawa (Tindo) chini ya Amiri Jeshi wa jeshi la mamluki hao Victor Mkello (RIP). (kumbe amiri jeshi hakuwa Mganda John Okello pekee, bali pia Mkello yumo?!.

Mamluki hao walitumia zana zao za kukatia mkonge, zile sime za makali kuwili, walizisunda kwenye nguo zao za ndani na kusafirishwa kwa mitumbiwi usiku usiku kupitia Kipumbwi. Jee wale mashuhuda wa Mapinduzi yale Matukufu ya Zanzibar, wanayakubali haya?.

Pia mwandishi anamalizia kwa kusema hata mauaji ya Karume, hayakutekelezwa na wapinga Mapinduzi, bali ni miongoni mwa hao hao wanamapinduzi, baada ya kupishana kauli fulani fulani za uendeshaji wa Zanzibar baada ya Mapinduzi.

Nimesoma kitabu cha John Okello kuhusu Mapinduzi ya Zanzibar,
View attachment 2077618
yeye anasema yake, vitabu kadhaa vya waandishi wazungu wanasema yao, historia tukuka ya Mapinduzi Matukufuya ya Zanzibar nayo nayo inasema kivyake, hivi hakuna any straight line yoyote kuhusu Mapinduzi hayo, ya Zanzibar?.
Jee yalipangwa na nani? Yalitekelezwaje?.
Nini haswa kilichotokea usiku ule wa Januari 11?.
Nani alifanya nini wapi?
Na mwisho tuzungumzie wafaidika wa Mapinduzi hayo Matukufu ya Zanzibar na bila kuwasahau wahanga wa Mapinduzi hayo ambao kwako yatakuwa sio Matukufu, ni kina nani haswa?, na kama kuleta amani na utangamano wa Zanzibar kuhusu Mapinduzi hayo kutahitajika kuundwa kwa Tume ya Ukweli na Upatanisho, "Truth and Reconciliation Commission" ili waliohasimiana kutokana na Mapinduzi hayo, wapatanishwe kwa maslahi mapana ya Zanzibar?.

Majibu ya maswali haya yatasaidia kujua mustakabali wa matokea ya uchaguzi wa Zanzibar kudhirihisha kuwa Wazanzibari ni wamoja, hakuna kundi la walishiriki Mapinduzi ndio wenye uhalali zaidi kuitawala Zanzibar kuliko wasioshiriki, after all kumbe Mapinduzi yenyewe, yametekelezwa na askari mamluki wa Kimakonde, toka mashamba ya mkonge Tanga!.

Pasco
Rejea za Mwandishi huyu kuhusu Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar
  1. Miaka 50 Ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, Bado Kuna Maswali Bila Majibu -1
  2. Neno "Matukufu" Katika Mapinduzi ya Zanzibar, Lilitoka Wapi, na Yana Utukufu Gani?!,
  3. Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar: Kumbe Waarabu Hawakufukuzwa! Walikimbia Wenyewe - Mzee Sukari
Tarehe kama ya leo 11/01/1964 miaka 60 iliyopita, ndio Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar yalifanyika!. Alfajiri ya Tarehe 12 Januari, 1964 ilikuwa ni kutangazwa tuu!.

Nawatakia maadhimisho mema ya miaka 60 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.
Paskali
 
Mkuu Maalim, Mohamed Said, kwanza nisamehe sana kwa kukuita mrongo, ila siku zote kunakuwepo na ukweli mmoja tuu, kinyume cha ukweli huo, mengine yote ni urongo!. Katika kusema ukweli kunaweza kuwepo kweli mbalimbali kwa kila mtu kuwa na ukweli wa upande wake wenye manufaa nao, lakini bado ukweli halisi huwa ni mmoja tuu!, ndio maana nimekuomba msamaha, kwa kuutegemea ukweli wa Dr. Ghasany kama refference ya ukweli wako, kumbe ni urongo tuu!.

Tukianzia na chanzo cha Mapinduzi yale Matukufu ya Zanzibar, Wananchi wa asili wa Zanzibar ni Wakwezi na Wahadimu kuchoshwa na udhalimu wa utawala wa Sultani na madhila waliyoyapata, shuhuda niliyemsikia leo TBC akishuhudia, alisema walijitolea kufa, kwa sababu hakuna aliyejua hatma ya mapinduzi yale kama yangefanikiwa au laa, na ndio maana hata Abedi Karume na wanaye, Amani na Ali, walikimbilia bara kuja kujificha kusikilizia kwanza!.

Kitendo cha kudai kuwa eti Mapinduzi yale Matukufu ya Zanzibar, yalikuwa sii mapinduzi bali ni uvamizi, ndio urongo mkubwa kabisa wa kwanza!. Kitendo cha kumdismiss John Okello kuwa had no role and did not play any vital part pia ni urongo wa pili!. Kwa Wakwezi na Wahadimu, yale yalikuwa ni Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, yaliyovikomboa visiwa hivyo, kutoka mikononi na kwenye makucha ya wavamizi madhalimu wa Kiarabu waliotoka zao kwao Oman, wakavivamia visiwa vile, wakaviteka, na kuifanya Zanzibar ni mali yao makao yao!. Hata Carl Peters alipokuja aliandaa mikataba ya kilaghai kurubuni mababu zetu akina Sultani Mangungo, ndipo wakaichukua ardhi ya Tanganyika kuigeuza yao. Hassan Bin Amiri, alipokitwaa kisiwa cha Kilwa, alikinunua kwa thamani ya kitambaa kilichokizunguka kisiwa chote cha Kilwa!, Sultan Seyyid Said alipotoka Oman kuihamishia sultanate yake toka Oman hadi Zanzibar, alivamia, na hakuwafanyia chochote Wahadimu as if watu wale ni kama manyani tuu, na visiwa hivyo aliviokota kama dodo chini ya mwembe, au sadakalawe!. Hivyo Mapinduzi yale Matukufu ilikuwa ni kuvikomboa visiwa hivyo toka kwa wavamizi na kuvirejesha mikononi mwa wenyewe!.

Kwa Waarabu Mapinduzi yale Matukufu ni uvamizi, lakini kwa wenyewe wenye visiwa vile Mapinduzi yale Matukufu ni ukombozi!. Sasa ukimleta kwenye TV mtu wa mrengo wa Mapinduzi ni uvamizi, bila kumuweka na mtu wa ku counter kuwa Mapinduzi yale ni ukombozi, matokeo yake watazamaji wataishia kulishwa matango pori na urongo wa uvamizi bila kusikia ukweli wa ukombozi!.

Kila binadamu ana haki ya uraia wa popote pale alipozaliwa regardless ya asili ya wazazi wake!, sasa hawa wazalia wa wavamizi wa Kiarabu waliozaliwa Zanzibar, ili kujenga uhalali wa asili yao ni Zanzibar na kuifuta dhana ya wazaliwa wa wavamizi, ndipo wakaja na andiko la kuonyesha Waarabu walikuwepo Afrika miaka mingi hata kabla ya wenyeji wa asili wa Afrika, nikasema huu ni urongo!.

Tanzania tumewahi kutawaliwa na mtawala mwenye asili ya Kitutsi, tukaja kutawaliwa na mtawala kutoka Nchumbiji, na sasa tunatawaliwa na Banyamulenge fulani kutoka Burundi, lakini no body cares kuhusu asili ya wazazi wao simply because wamezaliwa Tanzania!, vivyo hivyo kwa wazalia wa wavamizi hawa wa Kiarabu, Zanzibar ndio kwao, ila huo uarabu wao, usiwapofushe kuyaona Mapinduzi Matukufu yale ni uvamizi badala ya ukombozi!.

Wewe umesoma kuhusu Mapinduzi na kuhadithiwa na mashuhuda, Ghasani pia kasoma na kuhadithiwa, mimi pia nimesoma na kuhadithiwa, hivyo acconts zote za Ghasani, zako na zangu zote ni hadithi tuu kutoka fasihi simulizi zikahifadhiwa kwenye fasihi andishi!, kwa vile mpaka sasa tunapoandika hapa, hawa mashujaa wa Mapinduzi Matukufu, baadhi wangali hai, kwa nini hawa wenye vituo vya TV, wasifanye juhudi za kuwatafuta watupe first hand inforrmation, badala ya kutegemea second hand news or third parties?!. Kwenye kitu kinachoitwa acuracy first hand news ndio the truth, tha rest inaweza kuwa urongo!.

Kwenye mada zangu hizi, nilijaribu kuhoji, nikaishia kutukanwa!.
Mapinduzi ya Zanzibar: Ukweli ni Upi?

Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar: Kumbe Waarabu Hawakufukuzwa, Walikimbia Wenyewe!.

'Karume Hakuyakimbia Mapinduzi ya ZnZ'-

Miaka 50 Ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, Bado Kuna Maswali bila majibu!


Utanisamehe sisi wengine wa huku bara lugha zetu ni ngumu kidogo, hatuna maneno malaini malaini, au lugha za kubembeleza, kama jambo ni urongo, tunaliita urongo na hatulirembi!.

Pole.

Pasco
Wana bodi, japo tuko kwenye harakati za kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Rais na Wabunge, kuna swali linanitatiza kuhusu Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, ambapo majibu yake sahihi, pia yanaweza kuwa ni kiashiria tosha cha mshindi wa urais wa Zanzibar, iwapo uchaguzi utakuwa huru na wa haki.

Swali hili lahusu ukweli haswa kuhusu Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar ya Januari 12, 1964, baada ya kuibuka kwa kitabu kingine kiitwacho "Kwaheri Ukoloni, Kwaheri Uhuru"
View attachment 2077603
kilichoandikwa na Mwanazouni wa Zanzibar, Dr. Harith Ghassany, kama kilivyofanyiwa mapitio na mwandishi Mohamed Said kwenye gazeti la Al-Nuur la leo.

Ghasanny anasema kumbe Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar yalitekelezwa na askari mamluki wa Kimakonde (Wakata Mkonge) ambao waliongozwa na Mzee Mohamed Omar Mkwawa (Tindo) chini ya Amiri Jeshi wa jeshi la mamluki hao Victor Mkello (RIP). (kumbe amiri jeshi hakuwa Mganda John Okello pekee, bali pia Mkello yumo?!.

Mamluki hao walitumia zana zao za kukatia mkonge, zile sime za makali kuwili, walizisunda kwenye nguo zao za ndani na kusafirishwa kwa mitumbiwi usiku usiku kupitia Kipumbwi. Jee wale mashuhuda wa Mapinduzi yale Matukufu ya Zanzibar, wanayakubali haya?.

Pia mwandishi anamalizia kwa kusema hata mauaji ya Karume, hayakutekelezwa na wapinga Mapinduzi, bali ni miongoni mwa hao hao wanamapinduzi, baada ya kupishana kauli fulani fulani za uendeshaji wa Zanzibar baada ya Mapinduzi.

Nimesoma kitabu cha John Okello kuhusu Mapinduzi ya Zanzibar,
View attachment 2077618
yeye anasema yake, vitabu kadhaa vya waandishi wazungu wanasema yao, historia tukuka ya Mapinduzi Matukufuya ya Zanzibar nayo nayo inasema kivyake, hivi hakuna any straight line yoyote kuhusu Mapinduzi hayo, ya Zanzibar?.
Jee yalipangwa na nani? Yalitekelezwaje?.
Nini haswa kilichotokea usiku ule wa Januari 11?.
Nani alifanya nini wapi?
Na mwisho tuzungumzie wafaidika wa Mapinduzi hayo Matukufu ya Zanzibar na bila kuwasahau wahanga wa Mapinduzi hayo ambao kwako yatakuwa sio Matukufu, ni kina nani haswa?, na kama kuleta amani na utangamano wa Zanzibar kuhusu Mapinduzi hayo kutahitajika kuundwa kwa Tume ya Ukweli na Upatanisho, "Truth and Reconciliation Commission" ili waliohasimiana kutokana na Mapinduzi hayo, wapatanishwe kwa maslahi mapana ya Zanzibar?.

Majibu ya maswali haya yatasaidia kujua mustakabali wa matokea ya uchaguzi wa Zanzibar kudhirihisha kuwa Wazanzibari ni wamoja, hakuna kundi la walishiriki Mapinduzi ndio wenye uhalali zaidi kuitawala Zanzibar kuliko wasioshiriki, after all kumbe Mapinduzi yenyewe, yametekelezwa na askari mamluki wa Kimakonde, toka mashamba ya mkonge Tanga!.

Pasco
Rejea za Mwandishi huyu kuhusu Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar
  1. Miaka 50 Ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, Bado Kuna Maswali Bila Majibu -1
  2. Neno "Matukufu" Katika Mapinduzi ya Zanzibar, Lilitoka Wapi, na Yana Utukufu Gani?!,
  3. Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar: Kumbe Waarabu Hawakufukuzwa! Walikimbia Wenyewe - Mzee Sukari
Tarehe kama ya leo 11/01/1964 miaka 60 iliyopita, ndio Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar yalifanyika!. Alfajiri ya Tarehe 12 Januari, 1964 ilikuwa ni kutangazwa tuu!.

Nawatakia maadhimisho mema ya miaka 60 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.
Paskali
 
Back
Top Bottom