Azam TV ina matatizo ya kiufundi

Tyupa

JF-Expert Member
Aug 11, 2013
802
653
Kwa muda mrefu Azam tv matangazo yake hayako sawa sawa, kuna mawingu au uchafu unaoziba picha zisionekano vizuri. Awali nilidhani tv yangu ni mbovu kumbe tatizo hili lipo kwa kila mtu anaetumia king'amuzi cha Azam.

Halafu niliona kuwa hili tatizo lipo Azam tu baada kufungua tv ya Zanzibar na kuona hali huko ni shwari kabisa.Uongozi wa Azam TV unapaswa kuangalia tatizo hili na kulipatia ufumbuzi. Wasingoje hadi raisi Maghufuli au Kikwete walalamike ndio waone kuwa kweli kuna tatizo.

Tatizo lipo na lina leta kero.
 
Ni tatizo la TV yako tu. Mbona kwangu shwaaaaaaaaaaaariiiiiiiiiiii. Acha kuharibu biashara za watu.
 
Ni tatizo la TV yako tu. Mbona kwangu shwaaaaaaaaaaaariiiiiiiiiiii. Acha kuharibu biashara za watu.
Ni kweli hilo tatizo lipo wala hajakosea kabisa, ila kakosea tu kusema kuwa ni kila king'amuzi.sio kila king'amuzi kina shida hii bali ni vile ving'amuzi vyote vya zamani vyenye muonekano wa rangi nyeupe na blue.ila vingine vyote vipya viko fresh tu kwa iyo ukienda kununua kipya uwezi ukapata ilo tatizo.
images%20(7).jpeg
 
Ni tatizo la TV yako tu. Mbona kwangu shwaaaaaaaaaaaariiiiiiiiiiii. Acha kuharibu biashara za watu.
Ni kweli kabisa hili tatizo lipo na sio ushabiki wala kuharibu biashara za watu.Ni taarifa na inawezekana hawajafahamu na linjitokeza sio mara nyingi ila linakera. ila sasa taarifa itakuwa imefika naamini Mkueugenzi yupo makini.

Nawapongeza kwa juhudi zenu.Ila mmejisahau kubalance habari sasa.Zamani mliweza,kuna mdudu amewavamia balance habari achana na mtindo wa TBC wa upande mmoja.Watawaponza.
 
Ni kweli hilo tatizo lipo wala hajakosea kabisa, ila kakosea tu kusema kuwa ni kila king'amuzi.sio kila king'amuzi kina shida hii bali ni vile ving'amuzi vyote vya zamani vyenye muonekano wa rangi nyeupe na blue.ila vingine vyote vipya viko fresh tu kwa iyo ukienda kununua kipya uwezi ukapata ilo tatizo.View attachment 1704594
Una maana wanataka tununue hivi vipya tuwaingizie mapato? Tujulisheni tujue cha kufanya,ila star times mchina HAPANA.Bora nibaki bila kingamuzi.
 
Mimi silioni hilo tatizo..naangalia game ya dodoma jiji, muonekano ang'aavu kabisaa
 
Wateja wa Azm tv ni wengi sana na hili tatizo la tv kuonesha uchafu unaoganda kwenye picha linazidi kuongezeka siku hadi siku.Uongozi wa chombo hiki wangetuambia tufanyeje ili kuondokana nalo.Kama tatizo liko kwenye ving'amuzi vya zamani je tuvitupe ili tununue vipya au turudishe kwenye ofisi zao na kupewa vingine vya kisasa? Nimewatembelea jamaa zangu wengi wenye Azam tv na kukuta tatizo hili lipo.Uongozi unapaswa watueleze shida ni nini ?
 
Wateja wa Azm tv ni wengi sana na hili tatizo la tv kuonesha uchafu unaoganda kwenye picha linazidi kuongezeka siku hadi siku.Uongozi wa chombo hiki wangetuambia tufanyeje ili kuondokana nalo.Kama tatizo liko kwenye ving'amuzi vya zamani je tuvitupe ili tununue vipya au turudishe kwenye ofisi zao na kupewa vingine vya kisasa? Nimewatembelea jamaa zangu wengi wenye Azam tv na kukuta tatizo hili lipo.Uongozi unapaswa watueleze shida ni nini ?
Niliwahi kukutana na upumbafu DSTV,king'amuzi kilikuwa kinaleta meseji katikati ya screen na hata ufanye nini haitoki,kuwaeendea wananiambia king'amuzi kimekuwa ni cha siku nyingi natakiwa kununua kingine,nikawaambia maisha yenyewe manati na pia hamkuniambia ni baada ya muda gani kitakuwa ni cha zamani,je kuna guarantee gani ya hiki mnachokiita kipya haitafika muda kiwe cha zamani?,ni uhuni mnaofaoifanyia,okay hiki nakipeleka wapi ?sina muda tena na li king'amuzi lenu na wala sihitaji utumbafu wenu, nikaachana na Dstv nikanununua cha lambalamba,na yeye kama kaanza madudu namuhama,ila ikinitokea na suluhisho lije eti ninunue kingine nawafungulia kesi ,maamake maana hawa tuambii kuwa ni baada ya muda gani kitakuwa hakifai tena.
 
Back
Top Bottom