Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,600
- 218,001
Hili ni tatizo la muda mrefu la Azam TV, hawana mabingwa wa promotion , huwezi kujua mechi inayochezwa hadi uingie kwenye channel ya soka , kwa mfano hakuna matangazo yoyote kwenye channel zao yanayoonyesha kwamba kuna ligi ya ufaransa , wala haijulikani game gani inaonyeshwa na channel fulani.
Wako duni mno kwenye eneo hili na wanaachwa nyuma kabisa na DSTV ambao hata channel ya sinema inakueleza gemu gani iko channel gani tarehe ngapi , yaani hawa Azam wanataka tuotee tu , wale wanaoangalia sinema zetu wala hakuna tangazo lolote linaloonyesha kama channel fulani inaonyesha game fulani ! wala hata mkanda unaotembea kama wafanyavyo super sports , haya ni maajabu ! na ni aibu kwa wahusika.
Biashara yoyote ni matangazo , Kwani kuna ugumu gani kutembeza hata mkanda wa maandishi kwenye kila channel yenu kuonyesha mechi fulani itachezwa tarehe fulani na itaonyeshwa kwenye channel fulani?
Kwa mfano, unaweka mechi kisirisiri kwenye ZBC2 huku ukijua hiyo ni channel ya misikiti unadhani ni nani atajua kuna gemu huko ? Kama lengo lenu ni kutufanya tuangalie hizo mechi basi ni lazima mtutangazie Mechi gani iko channel gani na ni saa ngapi , iwe EPL , BUNDESLIGA, CARABAO, NBC, YA KIRAFIKI AU YOYOTE.
Acheni kuzifanya mechi za soka kuwa siri yenu.
Wako duni mno kwenye eneo hili na wanaachwa nyuma kabisa na DSTV ambao hata channel ya sinema inakueleza gemu gani iko channel gani tarehe ngapi , yaani hawa Azam wanataka tuotee tu , wale wanaoangalia sinema zetu wala hakuna tangazo lolote linaloonyesha kama channel fulani inaonyesha game fulani ! wala hata mkanda unaotembea kama wafanyavyo super sports , haya ni maajabu ! na ni aibu kwa wahusika.
Biashara yoyote ni matangazo , Kwani kuna ugumu gani kutembeza hata mkanda wa maandishi kwenye kila channel yenu kuonyesha mechi fulani itachezwa tarehe fulani na itaonyeshwa kwenye channel fulani?
Kwa mfano, unaweka mechi kisirisiri kwenye ZBC2 huku ukijua hiyo ni channel ya misikiti unadhani ni nani atajua kuna gemu huko ? Kama lengo lenu ni kutufanya tuangalie hizo mechi basi ni lazima mtutangazie Mechi gani iko channel gani na ni saa ngapi , iwe EPL , BUNDESLIGA, CARABAO, NBC, YA KIRAFIKI AU YOYOTE.
Acheni kuzifanya mechi za soka kuwa siri yenu.