Azam FC 1-2 Yanga SC|| Uwanja wa Chamazi|| NBC Premier League

Linguistic

JF-Expert Member
Mar 16, 2021
3,671
8,237
Leo kutakuwa na Mtanange wa Kukata na Shoka kati Azam Fc na Yanga SC.
.
Wakuu mechi hii itaanza majira ya saa 2:15 usiku Uwanja wa Chamazi Complex.
.
Tunajua ugumu wa game hii ya leo Ukizingati timu hizi zinapokutana hupigwa mpira wa nguvu sana.
.
Azam FC ni Mwenyeji wa Mchezo wa Leo Dhidi ya Yanga.
.
Huku Team Ya Yanga ikiwakosa Wachezaji wake kama Feisal Salum, Bangala, Aucho nk.

==================================

YANGA YAIFUNGA AZAM FC 2-1, YAFIKISHA POINTI 51

Yanga wameendelea kujiimarisha katika kilele cha Ligi Kuu Bara baada ya kupata ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Azam FC kwenye Uwanja wa Azam Complex, Aprili 6, 2022.

Yanga imepata mabao yake kupitia wa Djuma Shaban kwa njia ya penati na Fiston Mayele, bao la Azam FC limefungwa na Rodgers Kola.

Yanga imefikisha pointi 51 wakati Azam FC imebaki na pointi 28 katika nafasi ya tatu kwenye msimamo wa Ligi.
 
Ina maana mpaka NBC wanabrand nyuma hiyo ni pre match press. Aibu kwa ligi Hata kufunika na Kitambaa tu Mezani Hawakuona umuhimu Wake.
.
Halafu angalia walivyopandishia viti vya Kukaa
Screenshot_20220406-161021.jpg
 
Ina maana mpaka NBC wanabrand nyuma hiyo ni pre match press. Aibu kwa ligi Hata kufunika na Kitambaa tu Mezani Hawakuona umuhimu Wake.
.
Halafu angalia walivyopandishia viti vya Kukaa
Hiyo meza usipotazama kwa makini inaweza kukumeza
 
Ina maana mpaka NBC wanabrand nyuma hiyo ni pre match press. Aibu kwa ligi Hata kufunika na Kitambaa tu Mezani Hawakuona umuhimu Wake.
.
Halafu angalia walivyopandishia viti vya Kukaa View attachment 2177905
Kwa mujibu wa kanuni za Mashindano, anaeandaa Press conference ya Club ni Club Mwenyeji/TFF/Board ya Ligi au ni Azam Tv ambae ndio Rights za Kurusha Ligi Kuu?
 
Sasa hii meza ameandaa Simba,Hawa TFF wenyewe kama msimamizi wa ligi, Simba njoo ofisini
Kwa mujibu wa kanuni za Mashindano, anaeandaa Press conference ya Club ni Club Mwenyeji/TFF/Board ya Ligi au ni Azam Tv ambae ndio Rights za Kurusha Ligi Kuu?
 
Back
Top Bottom