Awamu ya tatu ya mgomo wa madaktari 23 June, 2012

Hatujapata mapendekezo ya upande wa serikali ili tupime uzuri na ubaya wa maoni yake. Ni vigumu kutolea maamuzi kwa maoni ya upande mmoja. Ikumbukwe kuwa mgogoro ni wa pande mbili: Serikali na Madaktari. Upande wa madaktari hauwezi kuwa HAKIMU kwa shauri lake yenyewe. Madaktari hawawezi kusema kwa uhakika kuwa Serikali imekosa hiki au kile, jambo hili kwa maoni yangu haliwezi kuwa sawa.
Madaktari wamekuwa wakisisitiza kutaka kugoma kila mara, lakini jamii na maadili ya taaluma ya udaktari yana wazuia. Hivyo kila wakipata kisingizio cha aina yoyote wanahamaki kutaka kutimiza azma yao ya kutaka kumuumiza bila huruma mlalahoi mnyonge. Hii haikubaliki hata kidogo kama malaria. Madaktari mnatuonea bure sisi wanyonge huku mkiwa tayari mlikula fedha zetu kwa kuwasomesha. Hawa mnaodhani mnawaadhibu hawapati adhabu hiyo. Lakini pia uchumi wetu bado ni mdogo, ikiwa Viongozi wanaonekana kufuja mali isivyohalali isiwe kigezo cha kudai zaidi hata ya uwezo halisi wa nchi. Hata leo hii tukimteua mwiungoni mwenu Daktari mmoja aende Ikulu hataweza kuwalipa madaktari kadri ya madai yao. Nakubaliana maslahi ya madaktari yanaweza kuboreshwa, lakini uboreshaji ni mchakato, huwezi kuboresha maslahi kwa usiku mmoja.

mkuu hilo linawezekana kabisa. Almasi za Mwadui tu zinatosha, pipi moja mil 800! Tafakari
 
Mpaka kieleweke, Ndugai lazima aeleweshwe watanzania tunaposema JK ni dhaifu in maana gani..
Hata afya zetu anaendelea kucheka na kutabasamu tuuuuuuu.......
Aibu kwa nchi, aibu kwa Taifa. Madaktari na watumishi wengine wa afya Aluta continua.. mpaka kieleweke..
Manesi nao tafadhali waunge mkono... wafamasia..., watu wa maabara....wakatuletee wanajeshi tena..
Nasema hivi The President is Weak
 
MADAKTARI SUBIRINI BAJETI MPYA

nawashangaa madaktari kugoma ktk mwezi wa sita! wasubiri makadirio mapya ya bajeti ndiyo waiulize serikali kuhusu madai yao
 
Siungi mkono madaktari kugoma. Uwezo wa serikali tuliyo nayo sasa umeishia hapo... Huwezi kumgomea kobe ukimlazimisha amfukuze hadi kumkamata kuku. Wafanyakazi wa serikali tuamue tu kujitolea kwa kuhurumiana kwa kipindi hiki cha mpito, hadi 2016, itakapokuwepo serikali yenye hadhi yake... Je kwa kugoma mnatukomoa wananchi au mnamkomoa "MDHAIFU"? Madaktari kumbukeni nyie ni sehemu ya Watanzania 'walioichagua' serikali hii dhaifu, ama kwa kuipigia kura, au kwa kutojitokeza kupigia kura mtu mwingine anayefaa, ama kwa kushindwa kulinda kura zetu, au hata kwa kutokugombea kama ulikuwa na uwezo...
Gomeni hata miaka kumi, tutakufa tutaisha, but serikali ya CCM haina uwezo (kwa maana ya nia au kuhurumia watanzania) wa kutatua mahitaji yenu...

Hivi kama baba wa familia ni mlevi, kibaka mvuta bangi... unadhani mama akigoma kuwapikia maharage watoto na kusema waache wafe na njaa, anayeumia ni baba au watoto?
 
Haya yote yanatokana na ulegelege, watu legelege huchagua viongozi legelege ambao huteua serikali legelege!!!!! Sisi sote kwa kuukubali huu mfumo legelege, tumedhihirisha ni kwa jinsi gani sisi ni legelege!!!!
 
Yafuatayo ni madai ya madaktari na majibu yaliyotolewa na serikali.

Kupandisha mishahara,
Bajeti ni finyu, kuwaongezea madaktari mishahara kutaongeza migogoro ktk secta nyingine,

Bima ya kijani kwa watumishi wa afya
serikali itaendelea na mazungumzo na mifuko hii, ili kuona kama wataboresha.

Risk allowances
serikali itatoa chanjo ya homa ya Ini(Hepatitis B) tu, nayo watapewa kwa awamu kutokana na ufinyu wa bajeti.

Hardship allowances
S
erikali inaboresha miundombinu katika sehemu zenye maisha magumu,

House allowances
serikali inajenga nyumba ktk halmashauri 70 za watumishi wa umma hata madaktari wakiwemo.Hata hivyo sio madaktari wote watapata.

Malipo ya kuitwa kazini usiku
S
erikali itaendelea kuliopa Tsh 25000 kwa daktari bingwa, 20000 kwa madaktari na Tsh 10000 kwa kada nyingine mpaka hapo bajeti itakaporuhusu.

Madaktari kukopeshwa magari
wafanyakazi wa serikali kuu wataanza mpango huo ktk bajeti ya 2011/2012.

Kwani Risk allowance ni Risk management mimi ninavyoelewa ni kwamba Risk na Hardship allowances ni hela za ziada wanozopewa kwa ajili ya kufanyakazi katika mazingira magumu au?
 
kwa jinsi alivyo dhaifu atasema huu upepo unapita na KUNA MKONO WA CHAMA CHA SIASA...............
 
Once again, nasimama upande wa madaktari. Na tutawashangaa wale ambao watasema madaktari wameharakisha na wasubiri "serikali ifanyie kazi madai yao"! Serikali hii haiwezi kwenda isipokuwa kwa kulazimishwa. I support the doctors and other health workers in the country!

Mzee mwanakijiji hapo naona kuna technical success or failure ya timing ya mgomo wa madaktari. serikali yaweza kujitetea kua madai yao yatazingatiwa katika bajeti itakayosomwa hivi karibuni. Ikumbukwe kua mama Sitta alishaikataa bajeti ya waziri wa afya hivyo kumlazimu waziri kwenda kuifanyia marekebisho ili kukidhi hoja za madai ya madaktari. Hii itasababisha mgomo ukose nguvu katika hatua za awali. Kwa upande mwingine inaweza kua ni technical approach ya kuilazimisha serikali kuzingatia madai yao kwenye bajeti tunayoisubiria. Time will tell!
 
madaktari please please msigome.. Zungumzeni..mtafute njia mbadala.. Ya kufikia muafaka wagonjwa hawana hatia mtakuwa hamwatendei haki.. Tafuteni next best altenative !
 
Madaktari na wauguzi, pamoja na wafanyakazi wote wa umma. Mbaya wenu sio serikani hata kidogo,mbaya wenu ni hawa wabunge ambao mliwachagua kuwawakilisha katika kuisimamia serikali na kuikosoa. Mfano,serikali inaleta budget mbovu ambayo haitekelezeki lakini wao wanaamua kuikubali kwa 100% na kuitetea hata kwa kutumia matusi kuwa ni bora sana.

Wanadiriki kuwaita vichaa wale wote wanaopinga kuwa haiwezi kuleta tija na nyie kutimiziwa mahitaji yenu ya msingi huku wakishauri wale wanaowatetea waletwe kwenu Mirembe muwapime akili.

Hapo mnailaumu serikani kwa lipi? wakati wale mlio wachagua kuwasemea kwa mujibu wa katiba wanawasaliti na nyie mnawaangalia na kuwatibia kama waheshimiwa wajapo wao au familia zao kwenu?

Mnawafahamu ni wabunge wa kundi lipi (tena ndio wengi) wanaofanya hayo, lakini hamtoi kauli yeyote kuwalaani kwa usaliti huo wala kutoa tamko kuwa hamridhishwi na wawakilishi wenu hao kwa kuhofia kuwa mtaonekana mko kisiasa zaidi,huo ni unafiki na UDHAIFU mkubwa.

Anayeunga mkono budget mbovu isiyojali maslahi yenu wakati katiba imempa mamlaka ya kukataa huyo ndiye asili ya shida zenu na za wengine. Huo ndio ukweli.

Mie nawashauri pamoja na mgomo huo (ambao utatuathiri wengi) mtoe tamko kuhusu tabia hii ya wabunge kuitetea serikali hata kwenye mambo yanayowaumiza walio walio watuma na uungaji mkono wa budget mbovu isiyo na tija kwenu.

Hata mkiweza tumeni wawakilishi wenu waende Dodoma wakaungane na wale walioko huko muandamane kwenda Bungeni kuonyesha kukerwa kwenu na jinsi Baadhi ya wabunge wa CCM wanavyofanya kazi inayowaumiza.
 
Kuna watu dhaifu ndani ya serikali wanafikiri madaktari na wauguzi wanatania.. tujitayarishe for the worse scenario
 
Wakitaka mafao mazuri waingie jeshini. Kule JWTZ ukiwa MD unapigwa u-captain then major fasta! Waende jeshini kwanza kuna uhaba wa madaktari sana na pilots! Mkishindwa haulazimishwi kufanya kazi, acha kazi, jiungeni, fungueni kadispensary then pigeni dili sio lazima muajiriwe hiyo profession yenu inauzika. Kama mnagoma tutawashangaa sana kwa kweli ila ni haki yenu maana siri ya mtungi aijuaye kata.
 
madaktari please please msigome.. Zungumzeni..mtafute njia mbadala.. Ya kufikia muafaka wagonjwa hawana hatia mtakuwa hamwatendei haki.. Tafuteni next best altenative !
Hiyo waliyoichagua ndiyo next........ MWENGE HAUVUKI KIJIJI
 
Huu mgomo haukuwahi kuisha kwa maana ya kuisha. Mimi nina watu wa karibu pale Muhimbili, mgomo baridi ulikuwa unaendelea. Watu walikuwa wanaingia wanasaini wanaenda kwenye mishe mishe zao. Lakini kwa kuwa serikali yetu sio makini, hakuna ufuatialiaji uliokuwa ukifanywa kujua kama kazi zinaendelea kama kawaida ama la. Ikawa kama hadithi ya mbuni kufunika kichwa kwenye mchanga..
 
Siungi mkono madaktari kugoma. Uwezo wa serikali tuliyo nayo sasa umeishia hapo... Huwezi kumgomea kobe ukimlazimisha amfukuze hadi kumkamata kuku. Wafanyakazi wa serikali tuamue tu kujitolea kwa kuhurumiana kwa kipindi hiki cha mpito, hadi 2016, itakapokuwepo serikali yenye hadhi yake... Je kwa kugoma mnatukomoa wananchi au mnamkomoa "MDHAIFU"? Madaktari kumbukeni nyie ni sehemu ya Watanzania 'walioichagua' serikali hii dhaifu, ama kwa kuipigia kura, au kwa kutojitokeza kupigia kura mt
haiingii akilini serekali kutenga 12bn kukrabat ikulu tena 2 yrs cosecatively
 
Back
Top Bottom