Awamu ya Tano na Udhibiti wa Ajali za Barabara I: Semeni Ninyi

Amani Msumari

JF-Expert Member
Aug 21, 2016
1,830
976
Wanajamvi, salaam.

Moja ya Jambo muhimu na la lazima ni serikali kuhakikisha inawalinda raia wake kwa gharama yoyote ile. Moja ya sababu kubwa ya vifo nchini Tanzania ni vile vitokanavyo na ajali za barabarani. Aidha ajali hizo zimesababisha ulemavu na kuongeza idadi ya mayatima nchini kwetu. Vijana hasa bodaboda, waenda kwa miguu, madereva na abiria wengi wamepotea. WHO inasema idadi ya vijana wanaokufa kwa ajali za barabarani inazidi ile ya wanaokufa kwa virusi vya UKIMWI. Hii haikubaliki.

Miongoni mwa mambo yanayotajwa kupelekea ajali hizo ni pamoja na mwendokasi, ubovu wa vyombo vya usafiri, kukosa umakini miongoni mwa madereva na watumiaji wengine wa barabara, madereva wasiopata mafunzo na ubovu wa miundombinu.

Sisi wote ni mashahidi wa jinsi serikali ya awamu ya tano ilivyojitahidi kuhakikisha inaokoa maisha ya raia wake kwa kutekeleza mambo ambayo ni muhimu katika kuzuia ajali za barabarani.

¹ Miundombinu ya barabara na madaraja imejengwa na inaendelea kujengwa nchi nzima. KWELI AU SI KWELI?

² Usimamiaji mzuri wa sheria za barabarani. Tochi, faini, elimu kwa madereva, abiria na watumiaji wa barabara. Ukiwa kwenye mabasi mara kwa mara vipande vya video vya elimu kwa umma kutoka mamlaka husika huchezwa. Namba za simu za RTO's zimebandikwa kwenye mabasi. KWELI AU SI KWELI?

³ Upigwaji marufuku wa viroba. Hivi vilihusika sana kwa ajali za bodaboda. KWELI AU SI KWELI?

Nimetaja mambo machache sana, Ila ningefurahi mkiniongezea hatua nyingine zilizochukuliwa na serikali.

Je, kwa hatua hizo, ajali zimepungua au hazijapungua?

Kama zimepungua, je hili sio jambo la kupongeza?

Je, kuna Jambo kubwa zaidi ya kulinda uhai wa watu wako?

#Amani on Monday night
 
Unalinda uhai wa raia huku kukiwa na kundi la WASIOJULIKANA ambalo linateka, linatesa, linapoteza na KUUA raia huku Serikali ikiwa kimya kabisa na hakuna uchunguzi wowote? 😳😳😳
 
Tupo vibaya sana kuhusu ajali za barabarani na Tz inashika namba 6 duniani kwa wingi wa ajali za barabani. Soma hapa chini kama unajua kimombo. Jiwe hajafanya chochote cha ajabu ni propaganda tu ndio zinamuinua, na watanzania wengi hawajui ni wajinga.

1596485843185.png
 
Unalinda uhai wa raia huku kukiwa na kundi la WASIOJULIKANA ambalo linateka, linatesa, linapoteza na KUUA raia huku Serikali ikiwa kimya kabisa na hakuna uchunguzi wowote? 😳😳😳
BAK na yako Ila jibu ya kwangu
 
Wanaojenga miundo mbinu hawazingatii viwango.

Imagine barabara inayo jengwa kimara kibaha, haina hata sehemu za watembea kwa miguu wakati barabara ipo katikati ya mji.
 
Wanao.jenga miundo mbinu hawazingatii viwango..

Imagine barabara inayo jengwa kimara kibaha, haina hata sehemu za watembea kwa miguu wakati barabara ipo katikati ya mji.
Umeiona design? Wanaojenga ni contractors, wao wanajenga kutokana na design waliyopewa. Je, unaweza kutuwekea design ya hiyo barabara?
 
Azory kupotea, Ben Saanane kupotea, Viroba bya maiti kuokotwa ufukweni mwa bahari, Kamanda Mawazo kuuwawa, kutekwa Roma mkatoliki na wengine wengi. Yote haya ni UZUSHI hahahahahahaha weye bado kweli!



Uzushi mkubwa
 
Tupo vibaya sana kuhusu ajali za barabarani na Tz inashika namba 6 duniani kwa wingi wa ajali za barabani. Soma hapa chini kama unajua kimombo. Jiwe hajafanya chochote cha ajabu ni propaganda tu ndio zinamuinua, na watanzania wengi hawajui ni wajinga.

View attachment 1526418
Haina maana kuwa tuko vizuri sana Ila tumepiga hatua. Ukiacha hiyo ripoti ya mwaka 2018, tuseme tuu ukweli.
Unasikia ajali za mabasi Kama ilivyokuwa mwanzo?
Unasikia ajali za bodaboda Kama ilivyokuwa mwanzo?

Sibishani na takwimu Ila namuaplai mzee Kikwete, za kuambiwa nachanganya na zangu
 
Azory kupotea, Ben Saanane kupotea, Viroba bya maiti kuokotwa ufukweni mwa bahari, Kamanda Mawazo kuuwawa, kutekwa Roma mkatoliki na wengine wengi. Yote haya ni UZUSHI hahahahahahaha weye bado kweli!


Hayo yanauhusiano gani na udhibiti wa ajali Tanzania?
 
Kwanini uandike kitu kisha unataka KUKIKANA? :oops: au roho zao ni roho za panya na si watu?

Je, kuna Jambo kubwa zaidi ya kulinda uhai wa watu wako?

Lakini uzi haukulenga huko ndugu yangu, unayumba bandugu
 
Tanroad inatakiwa kufumuliwa, na kuwa organized.

Imagine barabara ya lindi hadi Rais amekuwa mkali ndio wanaamka kwenda kuikarabati.

Barabara inepojengwa inatakiwa izingatie matumizi yote

1. Wanyama ( kama eneo lina wanyama)
2. Watembea kwa miguu (kama ni mjini)
3. Baskeli ( kama ni mjini)
4. Magari
5. Vituo vya abiria
6. Vituo vya magari Y mizigo
7. Vituo vya ukaguzi ( polisi)
8. Mizani ()
Umeiona design? Wanaojenga ni contractors, wao wanajenga kutokana na design waliyopewa. Je, unaweza kutuwekea design ya hiyo barabara?
 
Na kubaliana na wewe.. matuta yana haribu sana magari.

Tatizo watu hawafanyi kazi zao, kuna mkoa ujautwa Iringa, Madereva wana nidhamu sana kwa sababu police wa huko hawacheki na nyani
View attachment 1526435


Wakati umefika sasa wa kuweka average speed cameras kama wanavyofanya UK. Ni lazima kuwaondoa askari barabarani na kuondoa matuta yasiyokuwa na sababu zozote.
 
Back
Top Bottom