NAMBA MOJA AJAYE NCHINI
JF-Expert Member
- Oct 29, 2019
- 8,512
- 17,420
Wakuu,
Awamu zote za serikali Ngorongoro haikuguswa kabisa!
Wamasai waliachwa kama urithi wa ikolojia ya asili kwa Watanzania.
Ngorongoro ilibaki kama utambulisho pekee asilia wa utamaduni wetu na tunu ya kujivunia ulimwenguni mwote.
Wahusika wameamua KUTUMIA udhaifu wa serikali ya awamu hii kukamilisha mchakato wao wa Muda mrefu na kumwangushia jumba bovu mama huyu.
Awamu hii ni HITIMISHO la kilele cha ufisadi na ubadhirifu mkubwa KABLA ya nyakati ngumu za kufunga mkanda zijazo katika kujenga Tanzania mpya.
Nalifananisha sakata hili na mauaji ya kimbari ya Rwanda ya mwaka 1994 KWA unyeti,usiri na ukimya wa Dunia ya vyombo VYA habari.
Sijajua anaeratibu uovu huu ni nani hasa!!na kwanini wako kimya hasa vyombo VYA ulinzi na usalama wa nchi yetu labda KWA sababu mkuu wa majeshi kastaafu na BADO mpya hajateuliwa Hadi Sasa!
Labda kuna juhudi za wanaume wa kweli nyuma ya pazia wanafuatilia sakata hili mimi sijui! Lakini inaumiza Sana kama kuna uhalisia wa hizo zinazovuja Hadi sasa.
Kuna haja ya wenye chama kuipitia ilani yao upya waone kama utekelezwaji wa haya upo na ulinadiwa wakati wa kampeni au kama ni maagizo aliyopewa na Wenye NCHI wakati anaapishwa kushika hatamu.
Ni nani Stan katabalo wa Sasa ajitoe mhanga tujue nini kinaendelea huko KWA kina!!?
Niwaombe whistle blowers waieleze Dunia kinachojiri!
Naizika RASMI awamu hii kwa Damu inayomwagika Ngoro ngoro kama inavoripotiwa KWA siri humu jukwaani na nawalaani wote wanaoficha aibu hiyo!
Mungu ibariki TANZANIA
Mungu libariki jeshi letu lipe akili ya kutotumikishwa vibaya kuua ndugu zao KWA maslahi ya ukoo na manufaa ya wachache!
Ujumbe huu uwafikie wazalendo wenye uwezo wa kufanya jambo na kujitoa KWA ajili ya ndugu zao.
Awamu zote za serikali Ngorongoro haikuguswa kabisa!
Wamasai waliachwa kama urithi wa ikolojia ya asili kwa Watanzania.
Ngorongoro ilibaki kama utambulisho pekee asilia wa utamaduni wetu na tunu ya kujivunia ulimwenguni mwote.
Wahusika wameamua KUTUMIA udhaifu wa serikali ya awamu hii kukamilisha mchakato wao wa Muda mrefu na kumwangushia jumba bovu mama huyu.
Awamu hii ni HITIMISHO la kilele cha ufisadi na ubadhirifu mkubwa KABLA ya nyakati ngumu za kufunga mkanda zijazo katika kujenga Tanzania mpya.
Nalifananisha sakata hili na mauaji ya kimbari ya Rwanda ya mwaka 1994 KWA unyeti,usiri na ukimya wa Dunia ya vyombo VYA habari.
Sijajua anaeratibu uovu huu ni nani hasa!!na kwanini wako kimya hasa vyombo VYA ulinzi na usalama wa nchi yetu labda KWA sababu mkuu wa majeshi kastaafu na BADO mpya hajateuliwa Hadi Sasa!
Labda kuna juhudi za wanaume wa kweli nyuma ya pazia wanafuatilia sakata hili mimi sijui! Lakini inaumiza Sana kama kuna uhalisia wa hizo zinazovuja Hadi sasa.
Kuna haja ya wenye chama kuipitia ilani yao upya waone kama utekelezwaji wa haya upo na ulinadiwa wakati wa kampeni au kama ni maagizo aliyopewa na Wenye NCHI wakati anaapishwa kushika hatamu.
Ni nani Stan katabalo wa Sasa ajitoe mhanga tujue nini kinaendelea huko KWA kina!!?
Niwaombe whistle blowers waieleze Dunia kinachojiri!
Naizika RASMI awamu hii kwa Damu inayomwagika Ngoro ngoro kama inavoripotiwa KWA siri humu jukwaani na nawalaani wote wanaoficha aibu hiyo!
Mungu ibariki TANZANIA
Mungu libariki jeshi letu lipe akili ya kutotumikishwa vibaya kuua ndugu zao KWA maslahi ya ukoo na manufaa ya wachache!
Ujumbe huu uwafikie wazalendo wenye uwezo wa kufanya jambo na kujitoa KWA ajili ya ndugu zao.