Awamu ya 6: Tusije zembea ujenzi wa Bwawa la uzalishaji umeme Stieglers Gorge

Kwanza nianze kwa kusema mimi si mpenzi mkubwa wa Rais wetu aliyepita, JPM.

Hata hivyo, pamoja na figisu nyingi za JPM katika mambo mbali mbali, mengine ambayo yalikuwa miradi ya upendeleo ulio wazi kimaeneo, katika mradi wa bwawa la umeme Stieglers alikuwa spot on.

Mradi wa ujenzi wa bwawa la kuweza kufua umeme la Nyerere Hydropower(Stieglers Gorge), ni kati ya miradi ya kimkakati yenye matokeo yanayoweza kuleta mapinduzi ya uchumi kwa miaka mingi ijayo.

Katika hili, nampongeza JPM kama ambavyo nimempongeza mara kadhaa huko nyuma.

Maneno maneno tunayosikia toka kwa Waziri wa sasa wa Nishati, Januari Makamba, yanatutia wasiwasi juu ya azma kukamilisha ujenzi wa bwawa hilo kwa wakati.

Tunajua naye JPM aliupa kisogo mradi wa uendelezaji wa uchimbaji wa gesi kwa matumizi ya uzalishaji umeme.

Lakini Waziri Makamba awe careful katika kutekeleza miradi hii ili yote yakamilike kwa manufaa ya nchi, Tanzania.

Haya maneno maneo …………..mara oooh, maji hayajazwi kwenye bwawa leo wala kesho,………… mara mradi uko nyuma, …………….mara mkandarasi hawezi kazi,
hayo wananchi hatupendi kuyasikia.
Tunachotaka kusikia ni lini mradi unakamilika, na tupate umeme wa bei chee.

Tunajua figisu kati ya JPM na baba yake January, Yusufu Makamba, lakini ni vyema tukayaweka hayo nyuma yetu na tugange yajayo, afterall JPM sasa hayupo.

Tunataka mradi wa JNHPP (Julius Nyerere Hydropower Project) ukamilike kwa wakati.

(NB: Tunasikia kutoka kwa ka nzi, kuwa kuna wakubwa wamejipanga kuingiza figisu kwa makusudi mradi huu)
Serikali haina HELA za kulipa wakandarasi sisi wengine tumezikimbia hizo kazi Jiwe alikuwa anatumia ulaghai hakuwa na Hela hizi anazofanya January ni sarakasi tu unaamini kwamba Tanzania hakuna Crane ya Tani 26?
 
Hiyo miradi mingine siikubali sana, ile mradi wa bwawa la kuzalisha umeme JNHPP lazima ukamilike kwa maendeleo ya nchi kiuchumi.

Mkuu bila kupinga uzi wako namba moja. Huo mradi wa SG una matatizo makubwa toka enzi za Magufuli, wanachokifanya akina Januari sasa ni kukabiliana na changamoto za mradi huo, huku wakihakikisha ukweli wa mradi huo hauvuji. Hivi hukumbuki ripoti ya CAG Mussa Asad iliyoonyesha kuwa mradi huo unajengwa kwa uholela mkubwa? Hivi hujui kuwa kingo za hilo bwawa zilibomoka na kusababisha mafuriko huko Lindi? Je mradi unaojengwa kwa usiri mkubwa wa hivyo unatarajia uwe na ufanisi tarajiwa?

Mimi naamini kabisa Magufuli angeweka shilingi 3t. Kwenye umeme wa gas tungepata hizo 2,115mg ambazo kawekeza 6.5t kwenye SG. Kuna watu wanaosema umeme wa maji ni rahisi na kuwa eti tumejenga kwa fedha zetu za ndani. Ukitazama dhana hii sioni ukweli wa kunishawishi, maana tulikuwa na umeme wa maji lakini haukuwa rahisi, bado mkaa ulikuwa rahisi kuliko umeme wa hydro. Mfano mwingine kuwa kitu kuwa chetu na kwa fedha zetu hakumaanishi urahisi, ndege ni za kwetu, mbona nauli yake sio nafuu kama ilivyokuwa fastjet?

Je itakuwaje kama ukweli wa umeme wa gas v/s maji ni gharama nafuu kiuwekezaji watu wakaamua kurudi kwenye gas? Maana. Hata maamuzi ya Magufuli haimaanishi kuwa alikuwa sahihi. Kama maji yameanza mgao kwa ukame wa mwezi mmoja, kipi kinatufanya tuamini umeme huo wa maji hautakutana na changamoto ya mabadiliko ya tabia nchi?
 
Serikali haina HELA za kulipa wakandarasi sisi wengine tumezikimbia hizo kazi Jiwe alikuwa anatumia ulaghai hakuwa na Hela hizi anazofanya January ni sarakasi tu unaamini kwamba Tanzania hakuna Crane ya Tani 26?
Liwe na liwalo, Awamu ya Sita lazima imalizie huu mradi wa JNHPP.
Watapata fedha wapi?
Tozo zina kazi gani?
 
Mkuu bila kupinga uzi wako namba moja. Huo mradi wa SG una matatizo makubwa toka enzi za Magufuli, wanachokifanya akina Januari sasa ni kukabiliana na changamoto za mradi huo, huku wakihakikisha ukweli wa mradi huo hauvuji. Hivi hukumbuki ripoti ya CAG Mussa Asad iliyoonyesha kuwa mradi huo unajengwa kwa uholela mkubwa? Hivi hujui kuwa kingo za hilo bwawa zilibomoka na kusababisha mafuriko huko Lindi? Je mradi unaojengwa kwa usiri mkubwa wa hivyo unatarajia uwe na ufanisi tarajiwa?

Mimi naamini kabisa Magufuli angeweka shilingi 3t. Kwenye umeme wa gas tungepata hizo 2,115mg ambazo kawekeza 6.5t kwenye SG. Kuna watu wanaosema umeme wa maji ni rahisi na kuwa eti tumejenga kwa fedha zetu za ndani. Ukitazama dhana hii sioni ukweli wa kunishawishi, maana tulikuwa na umeme wa maji lakini haukuwa rahisi, bado mkaa ulikuwa rahisi kuliko umeme wa hydro. Mfano mwingine kuwa kitu kuwa chetu na kwa fedha zetu hakumaanishi urahisi, ndege ni za kwetu, mbona nauli yake sio nafuu kama ilivyokuwa fastjet?

Je itakuwaje kama ukweli wa umeme wa gas v/s maji ni gharama nafuu kiuwekezaji watu wakaamua kurudi kwenye gas? Maana. Hata maamuzi ya Magufuli haimaanishi kuwa alikuwa sahihi. Kama maji yameanza mgao kwa ukame wa mwezi mmoja, kipi kinatufanya tuamini umeme huo wa maji hautakutana na changamoto ya mabadiliko ya tabia nchi?
Mkuu mengine ni spin.
Mradi haujawahi kubomoka na kusababisha mafuriko.
Ila tujue kuwa bwawa lipo sehemu ambapo kuna unstable rock na kinachofanywa ni kustabilize rock face.
Nakuambia hivyo maana nimefika Stieglers mwanzoni mwa mwaka huu kushudia mwenyewe.
ITS A BIG PROJECT.
No doubt!
 
Mkuu mengine ni spin.
Mradi haujawahi kubomoka na kusababisha mafuriko.
Ila tujue kuwa bwawa lipo sehemu ambapo kuna unstable rock na kinachofanywa ni kustabilize rock face.
Nakuambia hivyo maana nimefika Stieglers mwanzoni mwa mwaka huu kushudia mwenyewe.
ITS A BIG PROJECT.
No doubt!

Je ripoti ya CAG kuwa mradi unaendeshwa kwa uholela nayo ni spin? I was in Lindi during the tragedy, unless you prove me wrong.

Unaposema kuwa it's a big project, huenda unachanganya au umeshindwa kuweka utetezi wako vizuri, sina tatizo na ukubwa wa mradi since ni mradi wa 6.5t, obvious utakuwa ni mkubwa. Mimi nazungumzia ubora wa mradi na changamoto zake, na sio ukubwa wa project.
 
Nchi hii bwana, kila mtu anaingia madarakani na vipaumbele vyake, hata huyu aliyerithi kiti ana vipaumbele vyake, terrible! SSH alitakiwa kujikita kwenye miradi inayoendelea ili iishe, yote ni kwa faida ya watanzania.
 
Je ripoti ya CAG kuwa mradi unaendeshwa kwa uholela nayo ni spin? I was in Lindi during the tragedy, unless you prove me wrong.

Unaposema kuwa it's a big project, huenda unachanganya au umeshindwa kuweka utetezi wako vizuri, sina tatizo na ukubwa wa mradi since ni mradi wa 6.5t, obvious utakuwa ni mkubwa. Mimi nazungumzia ubora wa mradi na changamoto zake, na sio ukubwa wa project.
Kiukweli mradi ulianza bila matayarisho ya kutosha, hilo halina ubishi.
Mradi hadi sasa unaendeshwa empirically, yaani ni kama design and build.
Kwa serikali hapakuwepo matayarisho kibajeti.
Hilo ni tatizo.

Lakini mafuriko ya Lindi hayakusababishwa namradi huu.
Hizo zilikuwa mvua zisizo za kawaida huko Lindi naMtwara, hata TMA waliliongelea hilo.
 
Kiukweli mradi ulianza bila matayarisho ya kutosha, hilo halina ubishi.
Mradi hadi sasa unaendeshwa empirically, yaani ni kama design and build.
Kwa serikali hapakuwepo matayarisho kibajeti.
Hilo ni tatizo.

Lakini mafuriko ya Lindi hayakusababishwa namradi huu.
Hizo zilikuwa mvua zisizo za kawaida huko Lindi naMtwara, hata TMA waliliongelea hilo.

Bila kupinga maelezo yako mazuri kwani naona hata ww umekubali kuna changamoto za dhahiri kwenye huo mradi. Sasa kama kulikuwa na mapungufu hayo yote, ni kipi kilishindikana kwa kingo za hilo bwawa kumomonyoka wakati wa hiyo mvua kubwa? Yote tisa ni hapo ulipomalizia kuwa hata TMA iliongelea mvua hizo! Hiyo TMA ni baadhi ya taasisi za umma zinazofanya kazi zake kwa Uduni mkubwa. Acha niishie hapa nisihame mada ya msingi.
 
Liwe na liwalo, Awamu ya Sita lazima imalizie huu mradi wa JNHPP.
Watapata fedha wapi?
Tozo zina kazi gani?
Ha ha ha kaka tozo watu wanatumia kulipia polisi kubambia watu wengi kesi.... kumbuka ule Mradi hata mabeberu wanaotusaidiaga waliugomea jiwe alitumia mbavu zake tu sasa hayupo waliopo hawajui watokeje mimi nilikuwa mkandarasi huko nimeacha kazi hakuna Hela
 
Nchi hii bwana, kila mtu anaingia madarakani na vipaumbele vyake, hata huyu aliyerithi kiti ana vipaumbele vyake, terrible! SSH alitakiwa kujikita kwenye miradi inayoendelea ili iishe, yote ni kwa faida ya watanzania.
Eleweni jambo hili Serikali haina HELA yakufanya hizo mambo
 
Kiukweli mradi ulianza bila matayarisho ya kutosha, hilo halina ubishi.
Mradi hadi sasa unaendeshwa empirically, yaani ni kama design and build.
Kwa serikali hapakuwepo matayarisho kibajeti.
Hilo ni tatizo.

Lakini mafuriko ya Lindi hayakusababishwa namradi huu.
Hizo zilikuwa mvua zisizo za kawaida huko Lindi naMtwara, hata TMA waliliongelea hilo.
Mradi ulianzishwa kwa ajili ya political mileage tu
 
Ha ha ha kaka tozo watu wanatumia kulipia polisi kubambia watu wengi kesi.... kumbuka ule Mradi hata mabeberu wanaotusaidiaga waliugomea jiwe alitumia mbavu zake tu sasa hayupo waliopo hawajui watokeje mimi nilikuwa mkandarasi huko nimeacha kazi hakuna Hela
Mradi wa kukukomboa mzungu hakupi hela.
Ule mradi tegemezi atakupa hela fasta
 
Nchi hii bwana, kila mtu anaingia madarakani na vipaumbele vyake, hata huyu aliyerithi kiti ana vipaumbele vyake, terrible! SSH alitakiwa kujikita kwenye miradi inayoendelea ili iishe, yote ni kwa faida ya watanzania.
Miradi ya ujenzi mwendazake alikua anapiga deal zake(mfano mzuri akiwatumia wale jamaa wa Mayanga co. ambapo mtoto wake Ni mmoja wa wakurugenzi wa co. hio) na sio kwamba alifanya kisa uzalendo,acha Sasa walioko madarakani nao watafute miradi yao wapige maana Ile iliyonzishwa hawana faida nayo mwendazake alishakunja chake mapema.
 
Mkuu bila kupinga uzi wako namba moja. Huo mradi wa SG una matatizo makubwa toka enzi za Magufuli, wanachokifanya akina Januari sasa ni kukabiliana na changamoto za mradi huo, huku wakihakikisha ukweli wa mradi huo hauvuji. Hivi hukumbuki ripoti ya CAG Mussa Asad iliyoonyesha kuwa mradi huo unajengwa kwa uholela mkubwa? Hivi hujui kuwa kingo za hilo bwawa zilibomoka na kusababisha mafuriko huko Lindi? Je mradi unaojengwa kwa usiri mkubwa wa hivyo unatarajia uwe na ufanisi tarajiwa?

Mimi naamini kabisa Magufuli angeweka shilingi 3t. Kwenye umeme wa gas tungepata hizo 2,115mg ambazo kawekeza 6.5t kwenye SG. Kuna watu wanaosema umeme wa maji ni rahisi na kuwa eti tumejenga kwa fedha zetu za ndani. Ukitazama dhana hii sioni ukweli wa kunishawishi, maana tulikuwa na umeme wa maji lakini haukuwa rahisi, bado mkaa ulikuwa rahisi kuliko umeme wa hydro. Mfano mwingine kuwa kitu kuwa chetu na kwa fedha zetu hakumaanishi urahisi, ndege ni za kwetu, mbona nauli yake sio nafuu kama ilivyokuwa fastjet?

Je itakuwaje kama ukweli wa umeme wa gas v/s maji ni gharama nafuu kiuwekezaji watu wakaamua kurudi kwenye gas? Maana. Hata maamuzi ya Magufuli haimaanishi kuwa alikuwa sahihi. Kama maji yameanza mgao kwa ukame wa mwezi mmoja, kipi kinatufanya tuamini umeme huo wa maji hautakutana na changamoto ya mabadiliko ya tabia nchi?

Ona Huyu na Ma gas yake ambayo Tunanunua kwa Wazungu kwa bei ghali wanatuuzia halafu tunauchakata ndipo Tanesco anauziwa...
Acha Hizo bana...
Kama unataka Kufaidika Na Gas tafuta namna nyingine waache watu wengi wafaidike na Umeme wa Nafuu wa Maji!
 
Bila kupinga maelezo yako mazuri kwani naona hata ww umekubali kuna changamoto za dhahiri kwenye huo mradi. Sasa kama kulikuwa na mapungufu hayo yote, ni kipi kilishindikana kwa kingo za hilo bwawa kumomonyoka wakati wa hiyo mvua kubwa? Yote tisa ni hapo ulipomalizia kuwa hata TMA iliongelea mvua hizo! Hiyo TMA ni baadhi ya taasisi za umma zinazofanya kazi zake kwa Uduni mkubwa. Acha niishie hapa nisihame mada ya msingi.
Kwa vile hujafika pale Stieglers Gorge, itakuwa vigumu kwako kuelewa rock formation ya sehemu hiyo.
Kwanza, pa
le site penyewe ni sehemu ambayo ni miamba, ambayo mingine ni loose.
Na dam inaanzwa kujengwa kwa chini, na ili hilo liwezekane kuna mtaro mkubwa sana uliojengwa ku divert maji toka site ya dam.
Napale chini palichim wa mita 50 kwenda chini ili kupata msingi mzuri wa dam, litakapo malizika dam hili litakuwa mita 190 kwenda juu!

Pili maji hayajawahi kuwa dammed, yaani kutengeneza bwawa lolote so far, kwa hiyo pale site hapawezi kuwa source ya maji yanayoweza kuleta uharibifu mpaka sasa.
Tatu, kwa hiyo loose rock formation( kwa miamba ya juu ya dam) ndiyo yano kaziwa kwa zege ili miamba hiyo isije poromoka wakati wowote.

Nne, TAASISI ya TMA, kwa ulelewa wangu ni WATABIRI, nasema watabiri wa hali ya hewa, ila wao ni wamesoma si kama Toboa Tobo.
 
Back
Top Bottom