Awamu ya 5 hakuna uzembe kwenye ofisi za umma? Help-Desk ya BRELA ina Ushahidi kamili

Mfiaukweli

JF-Expert Member
Aug 30, 2018
5,636
8,774
Wandugu;

Nipo kwenye mizunguko yangu ya kutafuta shekeli kwenye mji mmoja hapa nchini. Sasa hivi nipo kwenye daladala - wanaita mzunguko hapa - na nimemsikia jamaa mmoja akiongea na mwenzake kwa simu. Kwa kawaida sina mazoea ya kusikiliza mazungumzo ya watu, ila attention yangu kwenye mazungumzo ya huyu ndugu yametokana na yeye kulalamikia huduma mbovu za dawati la msaada la BRELA. Kwa kifupi huyu ndugu anasema simu zao ama hazipatikani au hazipokelewi.

Nilidhani ni mimi peke yangu ndie huwa nakumbana na hili tatizo; namba wanazozinadi kuwa ukipiga utapata msaada zaidi ni hizi:

0735 331001, 0735 000003 na/au 0735 331004.

Binafsi SIJAWAHI kupiga namba yeyote kati ya hizo na ikapokelewa. BRELA; kama hamtaki kupigiwa kuna sababu gani ya kuzitangaza hizo namba?

Halafu kuna watu wanatuambia kuwa awamu hii nidhamu ya kazi imepanda na uzembe hakuna!
 
Tatizo la Customer support kwa taasisi za umma au zinazo milikiwa na kuendeshwa na watanzania ni kubwa sana.
Hotline nyingi sana hazifanyi kazi/hazipokelewi hata makampuni binafsi ya kitanzania.

TANROADS nao kuna wakati walikuwa hivi hivi hawana msaada kwenye simu na hata uende ofisini wanakuambia unachotaka kipo mtandaoni kafanye mtandaoni, ukienda huko bado kuna mapungufu mengi.

Hapo Vodacom Tanzania namba ya huduma kwa wateja ni majanga, wanataka mufanye mawasiliano kwa mitandao ya kijamii au kuna menu chache za sauti ambazo kuna matatizo kibao hayapo kwenye category za menu zao, sasa ilitakiwa uongee na mhudumu moja kwa moja haupati nafasi hiyo.

Nabaki najiuliza hawa vodacom hawajui kuna watu wengi wapo vijijini na vitochi hawawezi kutumia hiyo mitandao ya kijamii.
Na kuna wengine wanapiga simu huku wanaendesha gari (wamevaa head set au wanatumia hands free mode), kutokana na mazingira hayo hawawezi ku-chat huko kwenye mitandao ya kijamii.

Sijui hapo Vodacom kaingia kiongozi mbongo au wamejaa wabongo vitengo vyote?

Kuna wakati ukitaka kukwepa sana gharama au kurahisisha kazi yako una haribu ubora wa huduma au bidhaa yako.
 
Na kinachonishangaza ni kuwa hata tatizo likiwa ni kutokana na uzembe wa idara husika ya umma bado anaadhibiwa mtu binafsi ambae ndie mteja wao.
 
CRDB walikosea moja ya jina langu kwa kuweki herufi 'i' mwishoni mwa jina langu ili hali hakuna hiyo herufi mwisho mwa jina langu. Niliacha kuitumia kwa muda baada ya kadi kupotea na wao kuleta ishu za kwenda Polis pamoja na serikali za mtaa ili kui renew. Siku nimeenda kuifufua kadi wakadai kitambulisho changu hakiendani na majina yaliyo kwenye system yao. Kwani kitambulisho hakina hiyo herufi 'i' na wao kwa bahati mbaya waliweka 'i' mwishoni, lakini docs zote nilizowapa wakati wa usajili hakuna hata moja yenye hiyo 'i. So wakadai siyo majina yangu juu ya huu utofauti, nikasema fine basi naombenj kufungua akaunti nyingine kama hayo siyo majina yangu, pia wakakataa eti kwa sababu tayari nina akaunti na ina picha yangu so natakiwa kwa gharama zangu(Muda na Pesa) niende kwa wakili kudhibitisha hayo majina kuwa linye 'i' na lisilo na 'i' yote ni yangu. Yani uzembe wao wameniangushia mimi mzigo !!!
Asanteni sana CRDB popote mlipo sipo....

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Jana nimeenda tanesko kuomba fundi nlivyojibiwa dah af lile tukio nilirekodi kwa simu😡😡😡😡😡

natamani ningepata contact za mkubwa nika share nae
 
Tatizo la Customer support kwa taasisi za umma au zinazo milikiwa na kuendeshwa na watanzania ni kubwa sana.
Hotline nyingi sana hazifanyi kazi/hazipokelewi hata makampuni binafsi ya kitanzania.

TANROADS nao kuna wakati walikuwa hivi hivi hawana msaada kwenye simu na hata uende ofisini wanakuambia unachotaka kipo mtandaoni kafanye mtandaoni, ukienda huko bado kuna mapungufu mengi.

Hapo Vodacom Tanzania namba ya huduma kwa wateja ni majanga, wanataka mufanye mawasiliano kwa mitandao ya kijamii au kuna menu chache za sauti ambazo kuna matatizo kibao hayapo kwenye category za menu zao, sasa ilitakiwa uongee na mhudumu moja kwa moja haupati nafasi hiyo.

Nabaki najiuliza hawa vodacom hawajui kuna watu wengi wapo vijijini na vitochi hawawezi kutumia hiyo mitandao ya kijamii.
Na kuna wengine wanapiga simu huku wanaendesha gari (wamevaa head set au wanatumia hands free mode), kutokana na mazingira hayo hawawezi ku-chat huko kwenye mitandao ya kijamii.

Sijui hapo Vodacom kaingia kiongozi mbongo au wamejaa wabongo vitengo vyote?

Kuna wakati ukitaka kukwepa sana gharama au kurahisisha kazi yako una haribu ubora wa huduma au bidhaa yako.

Sijui umejua vipi. Kipengele cha consumer segments ni mwanamke Mbongo kabisa.
 
CRDB walikosea moja ya jina langu kwa kuweki herufi 'i' mwishoni mwa jina langu ili hali hakuna hiyo herufi mwisho mwa jina langu. Niliacha kuitumia kwa muda baada ya kadi kupotea na wao kuleta ishu za kwenda Polis pamoja na serikali za mtaa ili kui renew. Siku nimeenda kuifufua kadi wakadai kitambulisho changu hakiendani na majina yaliyo kwenye system yao. Kwani kitambulisho hakina hiyo herufi 'i' na wao kwa bahati mbaya waliweka 'i' mwishoni, lakini docs zote nilizowapa wakati wa usajili hakuna hata moja yenye hiyo 'i. So wakadai siyo majina yangu juu ya huu utofauti, nikasema fine basi naombenj kufungua akaunti nyingine kama hayo siyo majina yangu, pia wakakataa eti kwa sababu tayari nina akaunti na ina picha yangu so natakiwa kwa gharama zangu(Muda na Pesa) niende kwa wakili kudhibitisha hayo majina kuwa linye 'i' na lisilo na 'i' yote ni yangu. Yani uzembe wao wameniangushia mimi mzigo !!!
Asanteni sana CRDB popote mlipo sipo....

Sent using Jamii Forums mobile app
Ha ha ha, wakati niko chuo nilikuwa mteja wao, baadae ninakaa mda mrefu bila kuitumia( unajua kwanini). Baada ya mambo yangu kukaa sawa nikaenda kutaka kuifufua kwakuwa ilikuwa imekuwa dormant. Jamaa wakaniambia kuifufua Tsh.30000/=. Niliachana nao nikaenda kufungua akaunti mpya na kwa Benki nyingine.
Mategemeo yangu ilikuwa kwakuwa nilikuwa mteja wao na akaunti imekuwa dormant kwa mda na sasa nataka niifufue wangenipokea kwa mikono miwili badala ya kuanza kuniambia niingie gharama tena.
 
Customer care Tanesco Chato kuna dada mmoja mrembo sana lakini hana majivuno hata kidogo tofauti na wanawake wengi, Mungu ambariki sana.

Ofisi zote za umma nchini zingekuwa na watu wa namna hiyo hata zile takwimu za wenye huzuni duniani tusingeongoza. Yaani umpigie simu, umkute ofisini au namna yoyote ile yupo very very very humble aisee!!!
 
Sijui umejua vipi. Kipengele cha consumer segments ni mwanamke Mbongo kabisa.
Ha haa
Mkuu mimi raia tu huku mtaani sijui chochote ndani ya hiyo taasisi sema naweza kutabiri tabia za wabongo, very predictable hasa kwenye kuhudumia watu.

Kama upo kwenye nafasi ya kuwafikishia huu ushauri waambie wana wachanganyanya na kuwavuruga kabisa wateja wazee au wasiokuwa na akaunti za mitandao ya kijamii, au watu walio banwa na majukumu ambao kwao kuingia kwenye hiyo mitandao ni kupoteza muda.
Mangi au mpemba yupo dukani au mama lishe yupo na wateja wengi anatoa wapi muda wa kuanza ku-chat na huduma kwa wateja wa vodacoma badala ya kupiga na kueleza shida zake haraka aendelee na kazi?

Mfano mimi nilipiga kutaka kuomba niondolewe kwenye usumbufu wa namba flani inanipigia kila siku kuniambia matangazo ya biashara, na jumbe flani. Unasikia simu inaita unaacha kazi muhimu unakutana na simu ya matangazo ya voda!!!
katika menu za sauti hakuna category ya kushughulika nakero au tatizo kama hilo.
Unakuta mtu upo shamba na kitochi huwezi kutumia mitandao ya kijamii, nilikwama kwakweli.
 
Mimi hawakunipa gharama yoyote japo kuna mtu wangu wa karibu walisema wanataka 20K kweli siwaelewi, hiyo ya chuo naijua wala hata usiseme
Ha ha ha, wakati niko chuo nilikuwa mteja wao, baadae ninakaa mda mrefu bila kuitumia( unajua kwanini). Baada ya mambo yangu kukaa sawa nikaenda kutaka kuifufua kwakuwa ilikuwa imekuwa dormant. Jamaa wakaniambia kuifufua Tsh.30000/=. Niliachana nao nikaenda kufungua akaunti mpya na kwa Benki nyingine.
Mategemeo yangu ilikuwa kwakuwa nilikuwa mteja wao na akaunti imekuwa dormant kwa mda na sasa nataka niifufue wangenipokea kwa mikono miwili badala ya kuanza kuniambia niingie gharama tena.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom