Zawadi Ngoda
JF-Expert Member
- Aug 13, 2009
- 3,804
- 1,871
Tanzania imeshatawaliwa na marais wanne tofauti, maarufu kwa jina la awamu nne. Akianza J.K. Nyerere, Alhaji Ali Hassan Mwinyi, Benjamin Che Mkapa na J.K. Mrisho.
Kwanza, kabla sijaendelea tuangalie muujiza mkubwa kabisa uliojitokeza kati ya awamu ya kwanza na ya nne. Angalia kwa makini majina hayo, J.K yanalingana. Na hii si bahati mbaya, bali iltabiriwa na Kinjeketile mwaka 1903 kabla ya kuanza vita vya maji maji. Lakini nini maana ya kushabihiana huko. Hili ni swali ninalowaachia wasomaji.
Kwa bahati nzuri mimi nimepata sababu moja wanayoshabihiana, nayo ni kupata umaarufu sana kwa watu wa ndani na nje. Pili kushika madaraka wakiwa vijana. Uchumi je? Sitii pua yangu huu ni uwanja wenu.
Ali Hassan Mwinyi na Mkapa. Hawa nao wana sifa moja inayoshabihiana, kuwa ni maraisi waliopata urais bila wananchi kuwadhania kuwa wangekuwemo katika jopo la wagombea Urais. Ya mwisho lakini si ndogo, wote huacha mouth touch.
Lakini yote tisa kumi, yupi ni mbora kuliko wote kama rais wa nchi? Tupe data zako za kina na toa ushadi tosha. Ni hoja makini tu ndizo zitazohesabiwa.
Kwanza, kabla sijaendelea tuangalie muujiza mkubwa kabisa uliojitokeza kati ya awamu ya kwanza na ya nne. Angalia kwa makini majina hayo, J.K yanalingana. Na hii si bahati mbaya, bali iltabiriwa na Kinjeketile mwaka 1903 kabla ya kuanza vita vya maji maji. Lakini nini maana ya kushabihiana huko. Hili ni swali ninalowaachia wasomaji.
Kwa bahati nzuri mimi nimepata sababu moja wanayoshabihiana, nayo ni kupata umaarufu sana kwa watu wa ndani na nje. Pili kushika madaraka wakiwa vijana. Uchumi je? Sitii pua yangu huu ni uwanja wenu.
Ali Hassan Mwinyi na Mkapa. Hawa nao wana sifa moja inayoshabihiana, kuwa ni maraisi waliopata urais bila wananchi kuwadhania kuwa wangekuwemo katika jopo la wagombea Urais. Ya mwisho lakini si ndogo, wote huacha mouth touch.
Lakini yote tisa kumi, yupi ni mbora kuliko wote kama rais wa nchi? Tupe data zako za kina na toa ushadi tosha. Ni hoja makini tu ndizo zitazohesabiwa.