Ndio! Acheni kwenda msikitini au makanisani kusali kwani waumini wengi mmejaa unafiki, majungu na mnaleta utani na swala!! Why? Wengi wanasali kila Ijumaa na Jumapili na hata jumamosi lakini matendo yao yanachefua na hawana dhamira ya kuacha dhambi.
Yanini kwenda msikitini au kanisani wakati baada tu ya sala unaenda kuiba, kuzini, kusengenya na ama kufitini?
Kuna haja gani ya kujimwambafai kanisani au msikitini kwa kutoa sadaka kubwa wakati unajijua utajiri wako sio wa halali? Hivi dhamira haiwasutii?
Ni bure kabisa kujishebedua kanisani au misikitini wakati unajiua unatembea na waume za watu. Ni upumbavu kuimba 'bwana asifiwe' kila kukicha wakati wewe ni tapeli mkubwa.
Kipindi hiki tuache kwenda kanisani na au misikitini kwa vile viongozi wa dini karibu wote wamegwaya kukemea ukandamizaji na kuchagua kuwa vibaraka wa serikali.
Tusiende kanisani na misikitini kuswali kwani baadhi ya viongozi wengi wa dini ni wanafiki wakubwa. Hawana ujasiri wa kuieleza Serikali maovu yake. Baadhi ya masheik, wachungaji ama maaskofu ni 'nunuliwabo'.
Hakika viongozi wa dini wamewaangusha sana Watanzania katika awamu hii ya uongozi kwa kuushabikia utawala wa Sasa na hivyo kuufanya uzidi kujimwambafai.
Viongozi wa dini wafahamu kuwa mtu kusema 'mniombee' kila kukicha haina maana kwamba ni kiongozi mzuri.
Tuache kwenda kanisani na misikitini kama dhamira zetu chafu. Ni kupoteza muda. Bora wanaotambika kwa mababu na au kujiita athiests!!! Kataa unafiki wa viongozi wa dini kwa kususia ibada zao!
Yanini kwenda msikitini au kanisani wakati baada tu ya sala unaenda kuiba, kuzini, kusengenya na ama kufitini?
Kuna haja gani ya kujimwambafai kanisani au msikitini kwa kutoa sadaka kubwa wakati unajijua utajiri wako sio wa halali? Hivi dhamira haiwasutii?
Ni bure kabisa kujishebedua kanisani au misikitini wakati unajiua unatembea na waume za watu. Ni upumbavu kuimba 'bwana asifiwe' kila kukicha wakati wewe ni tapeli mkubwa.
Kipindi hiki tuache kwenda kanisani na au misikitini kwa vile viongozi wa dini karibu wote wamegwaya kukemea ukandamizaji na kuchagua kuwa vibaraka wa serikali.
Tusiende kanisani na misikitini kuswali kwani baadhi ya viongozi wengi wa dini ni wanafiki wakubwa. Hawana ujasiri wa kuieleza Serikali maovu yake. Baadhi ya masheik, wachungaji ama maaskofu ni 'nunuliwabo'.
Hakika viongozi wa dini wamewaangusha sana Watanzania katika awamu hii ya uongozi kwa kuushabikia utawala wa Sasa na hivyo kuufanya uzidi kujimwambafai.
Viongozi wa dini wafahamu kuwa mtu kusema 'mniombee' kila kukicha haina maana kwamba ni kiongozi mzuri.
Tuache kwenda kanisani na misikitini kama dhamira zetu chafu. Ni kupoteza muda. Bora wanaotambika kwa mababu na au kujiita athiests!!! Kataa unafiki wa viongozi wa dini kwa kususia ibada zao!