Raia Fulani
JF-Expert Member
- Mar 12, 2009
- 10,848
- 2,670
Kumbe wengine wapo. Wabongo wamekuwa wakiwasakama majaji wa BSS kwa sana. Ni kwa vile kile kipindi kinatazamwana na watu wengi na kiko muda muafaka. Kuna huyu jamaa anajiita SSssssebo Chibuluma. ni mganda huyu. yuko EA radio. anaendesha kipindi cha friday night live. ni mbabe. analeta ubabe wa Idi amini ndani ya bongo. si mara ya kwanza kuwakejeli wasanii wetu wa bongo. jana nilijisikia vibaya alipokuwa akihojiana na mtozi (mtozi ni producer) anaitwa steve white. kwa kweli alimharass vibaya hadi kufikia hatua ya kumfukuza. bahati nzuri au mbaya nilikuwa nasikilizia kupitia redio yangu ndogo. wakija wasanii wa kenya au uganda huwa anaongea nao vizuri sana. vipi kwa wasanii wa bongo? akiachiwa huyu atajenga himaya. tunaomba wadau walio karibu na chombo hiki wamweleze huyu jamaa kuwa hatutaki mambo ya ki idi amini hapa!!