Auwawa kwa risasi katika tukio la ujambazi Shinyanga

Bahimba

JF-Expert Member
May 8, 2013
510
346
Wakuu mko poa?

Kama mko poa, sisi hapa kwetu Shinyanga hatuko poa kivile! weekend tuliaanza vyema lakini tumeimaliza vibaya kwa tukio la ujambazi lilitokea jana jioni mida ya saa 2 kasoro hivi mitaa ya Ndala Darajani tukio lililoambatana na mauji ya mtu mmoja ambaye alikuwa akitoa huduma ya m.pesa walipo mwamuru awape hela na ndipo yalipotokea majibizano baina yake na majambazi na ndipo yalipomfyatulia risasi na kufa hapohapo.

Polisi walifika eneo la tukio saa moja baadae na kukuta majambazi wameshatokomea na pesa ambazo bado haijajulikana hesabu yake.
 
Kisha bila hofu majambazi hayo saa 2.30 uck huo yakaenda kata ya Ibinzamata yakapora 300,000 taslimu, vocha za 150,000, simu 4 yakatoweka kiulaini bila hofu yoyote. Polisi walifika eneo la tukio baada ya muibiwaji kwenda mwenyewe kituoni! polisi kata hakupatikana INADAIWA ALIZIMA CM YAKE YA KIGANJANI! - Source m/kiti wa mtaa! RPC Shy Evarist Mangalla amethibitisha.
 
Back
Top Bottom