Au nasema uongo ndugu zangu?Kila kitu hapa bongo ukiwa na pesa,,hata polisi hawata kugusu,, nchi ni yako,, pesa ndiyo mchongo unaweza hata lala ndani ya maji
Utakapoelewa nini Kirefu cha RUSHWA! Ndio utaelewa alipitapitaje kwenye viwanja vyetu Licha ya kuonwa amezibeba!!!
Askari ni nani? Hawana njaa kwani? Hawapendi maendeleo kama haya yawanasiasa?Awamu hii, Askari wa kila aina wamejaa katika kila sekta, haya mambo bado yanawezekanaje? pale airport asilimia kubwa ya wanaonekana ni wahudumu wa kawaida kabisa ni askari, tena wengine wabobezi.
Bro aina hiyo ya vinyonga " vinyonga wenye pembe mbili" dunia nzima wanapatikana Lushoto kwenye milima ya usambara pekee.Hata mimi ningemuona huyo mtu na vinyonga kisha anipe rushwa ningechukua mapema. Maana hao vinyonga wana faida gani hapa nchini? Ni bora waende huko kwa watu wanaodhani wana thamani. Mfano mrahisi mpaka sasa huyo jamaa kakamatwa, lakini huwezi sikia serikali imeenda kuwakamata hao vinyonga na kwenda kuwauza huko wajenge madarasa.
Kama ni hivyo waturudishie huyo bwana ili tumuulize Kama alifuata taratibu na Kama alifuata taratibu anawasafirishaje kwenye soksi viumbe hai?Ni mategemeo yangu huku kwetu aliondoka nao kwa kufuata taratibu zote, tatizo la uelewa liko huko kwao.
Bro aina hiyo ya vinyonga " vinyonga wenye pembe mbili" dunia nzima wanapatikana Lushoto kwenye milima ya usambara pekee.
Watu wanatoka Ulaya kuja kuwaangalia hao vinyonga, halafu unasema hawana faida?Sina tatizo na upatikanaji wa hao vinyonga huko Lushoto, je wanafaida gani kwa watu wa huko Lushoto? Nimekaa Lushoto na hao vinyonga nawafahamu sana, sioni chochote cha maana toka kwa hao vinyonga zaidi ya kuona wakikera watu wanapochuma matunda huko mashambani. Serekali iwakamate ikawauze ili hizo fedha zijenge madarasa.
Watu wanatoka Ulaya kuja kuwaangalia hao vinyonga, halafu unasema hawana faida?
itakula kwako kama huyo jamaa, serikali inakukamata unafunguliwa mashtaka kama huyo jamaa, vinyonga serikali inachukua inapeleka kwenye mbuga zao, inapiga hela.Ayeyeee nimeona fursa hapa. Yani nafikisha vinyonga ausralia na kula milion kama 70 asee. Hivi na nyinyi mmeona kama mimi navyo ona?
Haya mwenye conection ya upatikanaji wa hivi vinyonga anitafte.
Umasikini ni ujinga!