Sam Gidori
Senior Member
- Sep 7, 2020
- 165
- 414
Serikali ya Australia imepanga kutunga sheria itakayolazimu mitandao ya kijamii kuonesha utambulisho wa watumiaji wasiotumia majina halisi watakaochapisha maudhui yenye kuudhi, au kulazimu mitandao hiyo kulipa faini kama fidia kwa madhara yatakayotokana na maudhui hayo ikiwa watashindwa kutoa utambulisho wa watumiaji.
Sheria hiyo mpya inalenga kuiwajibisha mitandao ya kijamii kwa maudhui yanayochapishwa na watumiaji pamoja na kuanzisha utaratibu utakaomwezesha mtumiaji yeyote atakayeudhiwa na maudhui yaliyopo katika mtandao wa kijamii kutoa malalamiko na kutaka maudhui hayo yaondolewe ikiwa yataonekana kumuudhi, kumchafua au kumtishia mtumiaji huyo.
Ikiwa mtandao wa kijamii utakataa kufuta maudhui hayo, mahakama inaweza kuamuru kuonesha utambulisho wa mtumiaji, na endapo mtandao wa kijamii utakataa amri ya mahakama, basi mtandao huo utalazimika kulipa kiasi chochote cha faini kitakachoamuliwa na mahakama.
Akizungumza siku ya Jumapili katika hotuba iliyorushwa kupitia televisheni, Waziri Mkuu wa Australia, Scott Morrison amesema uhuru wa kutoa maoni unapaswa kuendana na uwajibikaji kwa yale utakayozungumza.
“Uhuru wa kutoa maoni hautakiwi kuwaruhusu waoga wanaojificha na kuwachafua au kuwatishia wengine kwa kuwaharibia maisha yao lakini wao wakiwa hawataki kujulikana,” alisema Morrison.
Morrison hakutoa maelezo zaidi juu ya jinsi sheria hiyo itakavyotekelezwa na ni kwa jinsi gani mitandao ya kijamii itaweza kuthibitisha utambulisho wa watumiaji.
Chanzo: RT
Sheria hiyo mpya inalenga kuiwajibisha mitandao ya kijamii kwa maudhui yanayochapishwa na watumiaji pamoja na kuanzisha utaratibu utakaomwezesha mtumiaji yeyote atakayeudhiwa na maudhui yaliyopo katika mtandao wa kijamii kutoa malalamiko na kutaka maudhui hayo yaondolewe ikiwa yataonekana kumuudhi, kumchafua au kumtishia mtumiaji huyo.
Ikiwa mtandao wa kijamii utakataa kufuta maudhui hayo, mahakama inaweza kuamuru kuonesha utambulisho wa mtumiaji, na endapo mtandao wa kijamii utakataa amri ya mahakama, basi mtandao huo utalazimika kulipa kiasi chochote cha faini kitakachoamuliwa na mahakama.
Akizungumza siku ya Jumapili katika hotuba iliyorushwa kupitia televisheni, Waziri Mkuu wa Australia, Scott Morrison amesema uhuru wa kutoa maoni unapaswa kuendana na uwajibikaji kwa yale utakayozungumza.
“Uhuru wa kutoa maoni hautakiwi kuwaruhusu waoga wanaojificha na kuwachafua au kuwatishia wengine kwa kuwaharibia maisha yao lakini wao wakiwa hawataki kujulikana,” alisema Morrison.
Morrison hakutoa maelezo zaidi juu ya jinsi sheria hiyo itakavyotekelezwa na ni kwa jinsi gani mitandao ya kijamii itaweza kuthibitisha utambulisho wa watumiaji.
Chanzo: RT