Aunt Ezekiel: Tununue bongo movie, movie za mbele hazituhusu

Nucky Thompson

JF-Expert Member
Sep 20, 2016
1,817
4,058
Msanii wa Bongo movie aunt ezekiel amedai bongo movie bado ina uhai ila soko limedorora kidogo, lakini kudorora huko ni kutokana na watanzania kutopenda vitu vya kwao
Amesema ni bora kununua bongo movie kuliko kununua movie za nje ambazo haziwahusu na za kutafsiriwa
 
Watu wengi wanazipotezea bongo movie kwasababu sio wabunifu wanatengeneza kazi mbovu yaani jambazi anavua viatu kuingia kufanya tukio!
20aecc8e906dc6be43d324f47c9fb8f2.jpg
 
Tatizo la wasanii wetu hawajui wanachotaka ili bongo movie iuzike.. Ni kama wale wanamuziki waliulizwa wanataka nn wakasema studio. Jk akawapatia..
Soko la movie duniani kote halipo Kwenye CD Bali Kwenye majumba ya cinema.. So wasanii wasitegemee chochote cha ajabu kwa mfumo huu wa kutoa CD na kupeleka Mtaani... Hakuna mwekezaji anayeweza ekeza fedha zake sehemu isiyo na faida.. Cheki wamarekani walipofikia.. Wanauwezo wa kuwekeza bilion 400 na wanauhakika itarudi.
So wasanii wakipata nafasi ya kuonana na serikali wawaombe msaada wa kushawishi wawekezaji zaidi Kwenye majumba ya cinema..
Pili na wasanii wetu pia wawe serious kidogo na kazi yao.. Mara ya mwisho kuangalia bongo movie sijui ni mwaka gani.. Kwa sababu kwanza story ni zile zile. Mtu na demu wake wanasalitiana.. Au uchawi.. No scene zao hazizidi nne.. Yaani chumbani sebleni na baa...
Na kudorora kwa soko ni matokeo ya Wateja kuzichoka movie za bongo... Yaani kwa mtu kama mm ambaye ni mpenzi wa movie hawawezi nishawishi toa fedha yangu tizama movie zao watawashika wasiijua English na bahati mbaya kuna jamaaa wanatafsiri now.. Wasipobadilika kuanzia Kwenye utunzi. Directing and acting wajiandae tafuta kazi nyingine za kufanya
 
Msanii wa Bongo movie aunt ezekiel amedai bongo movie bado ina uhai ila soko limedorora kidogo, lakini kudorora huko ni kutokana na watanzania kutopenda vitu vya kwao
Amesema ni bora kununua bongo movie kuliko kununua movie za nje ambazo haziwahusu na za kutafsiriwa

Tatizo akili fupi za waigizaji wa kibongo pamoja na madirector wao ndio wanafanya tusinunue movie zao. Yaani ninunue bongo movie nikaangalie jambazi anavua viatu kabla ya kuingia ndan ya nyumba kufanya uhalifu dah!. SIPENDAGI UJINGA MM.Bora niendelee kufaidi series za mbele
 
Watu wengi wanazipotezea bongo movie kwasababu sio wabunifu wanatengeneza kazi mbovu yaani jambazi anavua viatu kuingia kufanya tukio!
20aecc8e906dc6be43d324f47c9fb8f2.jpg
Yani hapo jambazi na aliyetekwa wote wanafanya utani hawako makini kabisa na kazi lini sijui tutafika level za wenzetu bado sana aise.
 
Tatizo la wasanii wetu hawajui wanachotaka ili bongo movie iuzike.. Ni kama wale wanamuziki waliulizwa wanataka nn wakasema studio. Jk akawapatia..
Soko la movie duniani kote halipo Kwenye CD Bali Kwenye majumba ya cinema.. So wasanii wasitegemee chochote cha ajabu kwa mfumo huu wa kutoa CD na kupeleka Mtaani... Hakuna mwekezaji anayeweza ekeza fedha zake sehemu isiyo na faida.. Cheki wamarekani walipofikia.. Wanauwezo wa kuwekeza bilion 400 na wanauhakika itarudi.
So wasanii wakipata nafasi ya kuonana na serikali wawaombe msaada wa kushawishi wawekezaji zaidi Kwenye majumba ya cinema..
Pili na wasanii wetu pia wawe serious kidogo na kazi yao.. Mara ya mwisho kuangalia bongo movie sijui ni mwaka gani.. Kwa sababu kwanza story ni zile zile. Mtu na demu wake wanasalitiana.. Au uchawi.. No scene zao hazizidi nne.. Yaani chumbani sebleni na baa...
Na kudorora kwa soko ni matokeo ya Wateja kuzichoka movie za bongo... Yaani kwa mtu kama mm ambaye ni mpenzi wa movie hawawezi nishawishi toa fedha yangu tizama movie zao watawashika wasiijua English na bahati mbaya kuna jamaaa wanatafsiri now.. Wasipobadilika kuanzia Kwenye utunzi. Directing and acting wajiandae tafuta kazi nyingine za kufanya
Sanaa inahitaji ubunifu ambao unakuja kwa kutokana na udadisi, unaoonglea hizo movie za Hollywood nyingi zimetokana na novels. Uliza wasanii wetu mwaka uliopita tu wamesoma vitabu vingapi? Ukiamua kufanya kitu kuwa occupation yako unahitaji kujenga passion na kitu hicho. Mfano ukisoma murder she wrote, unaangalia utamaduni wetu, unachanganya na current technology available. Hapa ndiyo ninapoona tatizo.
 
Matendo halisi ya wabongo movie (mimi I never call u stars) na na mnavyo act movie zenu ni sawa sawa kabisa.

Aunt Ezekiel kashugulikie kumsaidia mumeo halisi aliyeko jela umangani huko, movie huwezi kabisa.
 
Sanaa inahitaji ubunifu ambao unakuja kwa kutokana na udadisi, unaoonglea hizo movie za Hollywood nyingi zimetokana na novels. Uliza wasanii wetu mwaka uliopita tu wamesoma vitabu vingapi? Ukiamua kufanya kitu kuwa occupation yako unahitaji kujenga passion na kitu hicho. Mfano ukisoma murder she wrote, unaangalia utamaduni wetu, unachanganya na current technology available. Hapa ndiyo ninapoona tatizo.
Umeongelea angle nzuri sana.. Yaani umegusia kwa wasanii wenyewe... Hope kama watakuwa wanapitia hizi page na kusoma haya mawazo yetu..
Natamani siku moja nikae kuangalia filamu ya kibongo nikasisimka..
Yaani soko la filamu bongo lina changamoto kila idara.. Waigizaji.. Watunzi. Waongozaji.. Yaani shaghala baghala..
Mfano mzuri ni wahindi.. Yaani kiteknologia na uwekezaji wako nyuma bado tena sana.. Sema kinachowabeba na kuwapatia umaarufu ni simulizi zao.. Yaani unaweza ukaangalia ukajikuta unalia...
Wenzetu wako makini kiasi cha kukubali fanya mazoezi au kujikondesha ili kukidhi mahitaji ya role..
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom