Faana
JF-Expert Member
- Dec 12, 2011
- 31,829
- 33,224
Mganga wa kweli ni camera za usalama kila kona ya nchiMtu mmoja ambaye hajatambulika jina lake, mkazi wa Mwanza na mfanyabiashara ya Tax amekutwa amekufa kwenye tax yake wilayani Sengerema baada ya kukodiwa na watu wasiojulikana kutoka jijini Mwanza.
Mtu huyo aligundulika kuwa ameuawa, kwa kunyongwa na kamba ngumu iliyofungwa shingoni kisha kwenye usukani wa gari lake pamoja na mikononi.
Marehemu amekutwa amekatwa Korodani kwa maana ya kende(pumbu), amenyofolewa koromeo na kuchomolewa macho yote mawili.
Marehemu inasemekana alikokodishwa na watu waliohitaji huduma ya tax kutokea mkoani Mwanza kwenda wilaya ya Sengerema.
Watu hao inasemekana baada ya tukio hilo walimtelekeza marehemu kwenye gari na kutokomea kusikojulikana.
Marehemu alipelekwa mochwari na kusafirishwa kupelekwa kwao Kamachumu wilaya ya Muleba na amezikwa Jana Kijijini kwao.
Bwana ametwaa ila wasiojulikana wametwa Zaidi, jina la bwana liimidiwe.
Inasemekana matukio haya ni mengi mkoani Mwanza, Je Nini kinaendelea mkoani Mwanza?.