AU waisamehe Tanzania kwa sasa

kavulata

JF-Expert Member
Aug 2, 2012
12,293
12,593
Tanzania tangu ipate uhuru wake ilijihusisha na siasa za Afrika zaidi kiasi cha kukosa nafasi ya kuhusika na maendeleo yake kikamilifu, tulifanya hivyo kwa kuongozwa na fikra za utu, uafrika na umoja. Tanzania ilikuwa na jeshi kubwa kwaajili ya kujilinda wenyewe kutokana na maadui iliyokuwa inajitengenezea kutokana na kuunga mkono juhudi za nchi nyingine zilizotaka kujikomboa dhidi ya wakoloni wao wenye nguvu kama Wareno na Makaburu na kuwasaidia wengine kijeshi.

Tuliamua kuisadia Afrika bila ya kutarajia ujira wowote kiasi cha kupitwa kiuchumi na zile nchi tulizozisaidia kujikomboa. Duniani kote nchi zenye majeshi makubwa na yenye nguvu kama sisi huwa wanayatumia majeshi yao katika kupora mali za nchi nyingine ambazo zitatumika kuliendesha na kulijenga jeshi na nchi, lakini kwetu sisi majeshi yetu yanategemea kuendeshwa kwa kodi za wananchi wenyewe, hayakodishwi wala kutumika kupora mali za wengine. Hii inasababisha gharama za kuyaendesha majeshi yetu iwe kubwa sana.

Hata Marekani au Rwanda huwa wana nguvu kijeshi lakini majeshi yao ni sehemu ya uchumi wao, hivyo yanajiendesha yenyewe na kuendesha uchumi tofauti na sisi. Ni vizuri sasa Afrika ikatusamehe na sisi kidogo kwa muda wakati huu tunarekebisha uchumi wetu chini ya kamanda mpya Rais JPM. Tuachane na ule ukiranja wa Afrika tulioufanya tangu tupate uhuru wetu ambao umetujengea heshima na sifa lakini kutubakiza masikini wa kutupwa.

Hebu watuache kidogo tupumue ili turekebishe uchumi wetu. Tusione aibu kulipa kodi kikamilifu maana hata wazungu wanafanya hivyohivyo kwenye kujenga uchumi wao. Kinachotakiwa hapa ni serikali kutenga ardhi kuuuubwa sana na kuwapa wawekezaji wakubwa watakaolima na kufuga kwa njia za kisasa na kutoa ajira nyingi kwa wananchi watakaoyahudumia mashamba, mazao na viwanda vya kuchakata mazao ya shambani, mifugo na uvuvi mkubwa.

Hii itapanua wigo wa kodi badala ya kila mtu kulima nusu eka ya mananasi, nusu eka mihogo, nusu eka mbaazi. Majeshi yetu yasiwe ya kwenda kupora mali za wengine lakini yawe ya uzalishaji mali mkubwa wakati yanafanyakazi ya kuilinda nchi.

Majeshi yetu yawe mstari wa mbele kuwa na mashamba makubwa ya kujilisha yenyewe na taifa, viwanda, hospitali kubwa, n.k kuliko ilivyo sasa hata jeshi la magereza lenye wafungwa linapewa chakula na uniform kwa kutumia kodi za wananchi.
 
ujumbe wako Mkuu ni kuwa tuache kushiriki katika juhudi za kuleta amani katika Afrika
 
Uko sahihi kabisa kwa mfano wako kuwa majeshi Je ya US na Rwand ani sehemu ya uchumi wa mataifa yao. Jeshi la Rwanda linaiba kule Congo, Jeshi la US hata sihitaji kukwambai linaiba wapi. Na haya sio siri. JE unatushauri na sisi tuanze kuiba jeshi lijiendeshe na kuwa sehemu ya uchumi wetu kama hao
Kuliendesha jeshi la kisasa lenye mbinu na silaha za kisasa kabisa ni kitu ghali sana, kama jeshi lako sio sehemu ya uchumi wa nchi na haliwezi kujiendesha lenyewe basi huhitaji kuwa na jeshi kubwa sana na lenye silaha za kisasa ambazo zitaexpire bila kutumika. Jeshi la namna hiyo litaifilisi nchi kwakuwa silaha nzuri za kivita ni ghali sana na zinapitwa na technologia haraka kwenye soko hivyo utatakiwa kununua sila mpya kila wakati. Nchi inaweza kujikuta inaingia kwenye madeni makubwa sana kutokana na kununua silaha mpya na za kisasa ambazo hazitumiki kuliingizia pesa taifa. Hii amani yetu ingetubidi sisi tuwe na jeshi dogo tu kwakuwa muda mwingi tuko kwenye hali ya amani kuliko vita kama ilivyo Uswis, hii ni tofauti na nchi kama Rwanda, Marekani, Israel, Burundi, Ethiopia ambayo yako vitani muda wote na majeshi yao yanasaidia kujiendesha na kuujenga uchumi wao kwa kugrab mali za watu wengine. Nchi nyingine ni maarufu sana kwa kukodisha majeshi yao kwa kulipwa pesa nyingi, na yako mataifa mengine ambayo yanatafuta nchi zenye mali na kuzichokosa ili wapigane kwakutumia nguvu zake kubwa za kijeshi na kuiba mali zilizoko kule. Lakini sisi hatuna majeshi ya kulipwa wala ya kibiashara, jeshi letu ni jeshi la ulinzi wa wananchi tu na jeshi la hisani/ridhaa na utu kwa wenye shida, Jeshi la aina hii kama hatutalifanya lizalishe mali mashambani, viwandani, baharini au kwenye ukandarasi wa mabarabara basi litaifilisi nchi hii. Tulipaswa kazi kama za ujenzi wa barabara zote nchini zingefanywa na jeshi hili ambalo muda mwingi halipigani na tunalilisha tu miaka nenda rudi na ndio maana sasa tumeamua liwe sehemu ya utawala kwa kuwaingiza baadhi yao kwenye siasa.
 
Daaaah, mleta mada Umeleta uzi unaosadifu maana ya JF hongera kwa kufikirisha kichwa chako.
 
Sasa ndg utwapata wapi wawekezaji wakati waliopo wanakimbia? Huyu ndg yako ni mzee ahambiliki.
 
Back
Top Bottom