Elections 2010 Atupwa jela miaka 3 kwa kutaka kupiga kura mara 2

Fidel80

JF-Expert Member
May 3, 2008
21,947
4,444
DAUDI Gimbishi (41) mkazi wa Kijiji cha Mwamitumi, Kata ya Ipililo, Wilaya ya Maswa, mkoani Simiyu, jana amehukumiwa kifungo cha miaka mitatu jela bila faini kwa kosa la kutaka kupiga kura zaidi ya mara mbili kinyume na utaratibu wa sheria ya uchaguzi ya mwaka 2010 kifungu cha 102(a).
Hukumu hiyo ilitolewa na Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Maswa, Thomson Mtani, baada ya mshitakiwa kukiri kosa huku akijitetea kuwa alifanya kosa hilo baada ya kuahidiwa kupatiwa sh 10,000 kutoka kwa Matege Magoto, aliyewahi kuwa diwani kipindi cha miaka ya nyuma.
Hakimu Mtani alisema mshitakiwa alitenda kosa hilo huku akijua anafanya kosa kisheria, jambo ambalo lingeweza kuvuruga matokeo ya uchaguzi na kusababisha uvunjifu wa amani sambamba na kuondoa haki ya mchaguliwa halali, hivyo anamhukumu kutumikia kifungo hicho ili liwe fundisho kwake na kwa watu wengine wenye tabia kama hiyo.
Awali Mwendesha Mashitaka, Mkaguzi Msaidizi wa Polisi, Pili, alidai kuwa mshitakiwa alitenda kosa hilo Oktoba 31 mwaka huu majira ya saa 7:00 mchana katika chumba cha kupigia kura kituo cha Ghalani kijijini humo.
Upande wa mashitaka ulidai mahakamani hapo kuwa mshitakiwa huyo alikutwa na jumla ya karatasi sita za kupigia kura zikiwa mbili za udiwani, mbili za ubunge na mbili za urais huku tayari akiwa ameshapiga kura awali.
Alidai wakala wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Bundala Ndogani, aliyekuwepo ndani ya kituo hicho aliweza kumgundua na kutoa taarifa kwa Mrakibu Msaidizi wa Polisi (ASP) Jumanne Mkwama ambaye alimweka chini ya ulinzi na alipompekua alimkuta akiwa na karatasi hizo.


Atupwa jela miaka 3 kwa kutaka kupiga kura mara 2

Hii sheria kwa nini haiwabani wanao chakachua?
 
Wanao chakachua wanapeta huyu kataka kupiga kura mara 2 kala mvua 3
 
DAUDI Gimbishi (41) mkazi wa Kijiji cha Mwamitumi, Kata ya Ipililo, Wilaya ya Maswa, mkoani Simiyu, jana amehukumiwa kifungo cha miaka mitatu jela bila faini kwa kosa la kutaka kupiga kura zaidi ya mara mbili kinyume na utaratibu wa sheria ya uchaguzi ya mwaka 2010 kifungu cha 102(a).
Hukumu hiyo ilitolewa na Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Maswa, Thomson Mtani, baada ya mshitakiwa kukiri kosa huku akijitetea kuwa alifanya kosa hilo baada ya kuahidiwa kupatiwa sh 10,000 kutoka kwa Matege Magoto, aliyewahi kuwa diwani kipindi cha miaka ya nyuma.
Hakimu Mtani alisema mshitakiwa alitenda kosa hilo huku akijua anafanya kosa kisheria, jambo ambalo lingeweza kuvuruga matokeo ya uchaguzi na kusababisha uvunjifu wa amani sambamba na kuondoa haki ya mchaguliwa halali, hivyo anamhukumu kutumikia kifungo hicho ili liwe fundisho kwake na kwa watu wengine wenye tabia kama hiyo.
Awali Mwendesha Mashitaka, Mkaguzi Msaidizi wa Polisi, Pili, alidai kuwa mshitakiwa alitenda kosa hilo Oktoba 31 mwaka huu majira ya saa 7:00 mchana katika chumba cha kupigia kura kituo cha Ghalani kijijini humo.
Upande wa mashitaka ulidai mahakamani hapo kuwa mshitakiwa huyo alikutwa na jumla ya karatasi sita za kupigia kura zikiwa mbili za udiwani, mbili za ubunge na mbili za urais huku tayari akiwa ameshapiga kura awali.
Alidai wakala wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Bundala Ndogani, aliyekuwepo ndani ya kituo hicho aliweza kumgundua na kutoa taarifa kwa Mrakibu Msaidizi wa Polisi (ASP) Jumanne Mkwama ambaye alimweka chini ya ulinzi na alipompekua alimkuta akiwa na karatasi hizo.


Atupwa jela miaka 3 kwa kutaka kupiga kura mara 2

Hii sheria kwa nini haiwabani wanao chakachua?

Huyu ni messenger karatasi za kupigia kura amepata wapi? Upelelezi ulitakiwa uende mbali zaidi ili kuchimbua hilo shina
 
Back
Top Bottom