Watanzania masikini wasiwe na wasiwasi kwani sisi watoto wao kamwe hatutakubali kunyanyaswa kwa sababu ya umasikini wetu, tumeanza na tutaendelea hadi dakika ya mwisho pale haki itakaposhinda dhulma.
Tunabaguliwa na wanasiasa kwa kuwatumia wasomi vibaraka na wanaotaka kujipendekeza ili wapewe madaraka.
Mkopo ni haki yetu ya kisheria kwani tuna vigezo kwa mujibu wa sheria na sisi kutodai ni sawa na kukubali dhulma itawale! tutadai mpaka kieleweke kamwe hatuwezi kupumbazika na ahadi za kisiasa zisizo na muda maalum wa utekelezaji. Kama tukishindwa kujitetea hata sisi wenyewe ni dhahiri kuwa hatutaweza kuitetea jamii yetu fukara pindi tutakapopata kazi. Kitu cha msingi ni wazazi kutuunga mkono si kutuona wahunu na wakorofi kama watuitavyo wanasiasa na wasomi vibaraka. Wazazi wanalipa kodi ili sote tupate huduma na si kugharamia safari na posho za viongozi ndumilakuwili waliowadanganya watanzania kuwa wataleta maisha bora kwa kila mmoja wao kitu kilchogeuka ndoto.
TUNAPASWA KUJIFUNZA KWA HILO!
Tunabaguliwa na wanasiasa kwa kuwatumia wasomi vibaraka na wanaotaka kujipendekeza ili wapewe madaraka.
Mkopo ni haki yetu ya kisheria kwani tuna vigezo kwa mujibu wa sheria na sisi kutodai ni sawa na kukubali dhulma itawale! tutadai mpaka kieleweke kamwe hatuwezi kupumbazika na ahadi za kisiasa zisizo na muda maalum wa utekelezaji. Kama tukishindwa kujitetea hata sisi wenyewe ni dhahiri kuwa hatutaweza kuitetea jamii yetu fukara pindi tutakapopata kazi. Kitu cha msingi ni wazazi kutuunga mkono si kutuona wahunu na wakorofi kama watuitavyo wanasiasa na wasomi vibaraka. Wazazi wanalipa kodi ili sote tupate huduma na si kugharamia safari na posho za viongozi ndumilakuwili waliowadanganya watanzania kuwa wataleta maisha bora kwa kila mmoja wao kitu kilchogeuka ndoto.
TUNAPASWA KUJIFUNZA KWA HILO!