Atlantropa super-continent: Mradi mkubwa wa kuunganisha Afrika na Ulaya kuwa bara moja.

zitto junior

JF-Expert Member
Oct 7, 2013
19,031
28,667
Mwanadamu kwa haiba yake akiwa kwenye changamoto ndio anapata wasaa mzuri wa kuchakata akili yake ili kupata suluhisho la matatizo yanayomzunguka. Na hili ndio lilimkuta Msanifu majengo na mhandisi wa kijerumani Herman Sorgel kuja kubuni mradi wenye maono makubwa uliohitaji wafanyakazi zaidi ya million moja na kukamilika baada ya miaka 150!!
atlantropa-001-title.jpg


Prologue
Herman Sorgel alikua msanifu majengo (Architect) aliyezaliwa mji wa Bavaria,ujerumani mnamo 1885 na kufariki mwaka 1952. Baada ya kushuhudia vita kuu mbili za dunia zikileta madhara makubwa na migogoro isiyoisha, mhandisi huyu ikabidi abuni mradi ambao ungeiunganisha ulaya kuwa kitu kimoja na kuepusha vita ya tatu ya dunia huku dunia nzima ikihakikishiwa amani milele sio kwa kutumia bunduki au siasa za majukwaani bali teknolojia.

Mpango wa Mradi:
images (19).jpg

Strait of Gilbraltar
Ningependa wasomaji mfahamu kuwa umbali kati ya ulaya na Afrika ni km 14 pekee kiufupi ukiwa morocco unaiona Hispania kabisa na katika historia kuna tukio linaitwa Messinian Salinic Crisis ambapo eneo hilo la ulaya lilishikamana na eneo la Afrika hivyo bahari ya Mediterranean ikazibwa jambo lililofanya maji yasiingie kutoka Bahari ya Atlantic. Ilichukua takribani miaka kadhaa kina cha maji kilipungua sana na bara la Afrika na ulaya yaligusana kabisa kwa nchi kavu. However mafuriko makubwa yalitokea huko mbeleni na kurudisha bahari hiyo mahala pake mpaka leo hii.

Dhana hii ilimfikirisha sana Mhandisi Sorgel kwamba kma ataweza kurudia tukio hilo la kijiografia kwa kutumia mbinu za kiuhandisi basi anaweza unganisha Ulaya na Afrika kuwa bara moja lenye nguvu na tishio kuliko yote.

Kiini cha mradi ingekua pale Gilbraltar ambapo ungejengwa bwawa la kufua umeme kubwa katika historia ya dunia ambalo lingefua megawatt elfu 50. Lingekua na urefu wa mzunguko km 34 na msingi wenye urefu wa km 2.5 kwenda chini ndani ya maji na 300 m juu ya maji.

Mpango ulikuwa, angeziba bahari ya Atlantic na mito inayozunguka kma Dardenelles kuleta maji kwenye bahari ya Mediterranean ili kupunguza kina cha maji hadi kufika Mt 200 magharibi na Mt 100 mashariki.

Bwawa hili lingezuia (Divert) maji kuingia bahari ya Mediterranean hivyo kina cha maji kingepungua kwa zaidi ya mita 200. Na maji mengine yangetumika kwenye kuzalisha umeme, mradi mkubwa wa kurutubisha jangwa la sahara kwa ajili ya kilimo cha kisasa pamoja na kutenga ardhi mpya ambayo ingeunganisha mabara ya Afrika na Ulaya ili kumaliza changamoto ya udogo wa ardhi.

images (17).jpg

Atlantropa ikikamilika mabara yangeungana hivi kwa nchi kavu

Mafanikio aliyotarajia
1.Kuwepo bara lenye nguvu kuweza kuchallenge nguvu ya America na Asia kama zingekuja kuwa tishio kiuchumi/Kisiasa.

2.Kumaliza tatizo la ajira ulaya maana wangetapakaa Huku Afrika kutafuta fursa mpya kma kilimo,madini n.k

3.Kungemaliza tatizo la ardhi ulaya maana aliona vita nyingi zilikua kugombania ardhi. Ulaya ingekua extended mpaka kusini mwa Afrika hivyo ardhi ingekua zaidi ya mahitaji.

4.Chakula kisingepungua maana ardhi mpya ingetumika kwa ajili ya kilimo na jangwa la sahara lingerutubishwa kwa mradi mkubwa wa umwagiliaji hivyo ardhi yake ingeanza kuwa na rutuba ya kukuza mimea. Yangejengwa mashamba makubwa kabisa ya kilimo cha kisasa hivyo chakula kisingewahi isha ulaya.

5.Nishati ingekuwa ya kutosha mfano huo mradi wote wa mabwawa ya umeme takribani 8 ungezalisha megawatts zaidi ya Laki moja hivyo umeme ungekuwa wa uhakika Atlantropa nzima hivyo kupunguza vita za kugombea nishati ndogo iliyobaki mfano mafuta na makaa ya mawe n.k

6.Mradi huu ungeunganisha mataifa yote ya Ulaya yaliyokua kwenye vuguvugu la vita kuu za dunia maana mradi ungehitaji ushirikiano wa mataifa yote kwenye utekelezaji na ukikamilika wangeishi kama familia moja na hivyo kusahau tofauti zao maana nishati ipo,chakula kipo,ardhi ya kumwaga!! Mpigane kwa lipi tena??!!

Utekelezaji Afrika
Screenshot_2019-12-23-14-03-23-1.png

Afrika ingejengwa maziwa makuu mapya mawili pale DRC kwenye mto congo na ziwa Chad lingetanuliwa kina. Hapa pia yangejengwa mabwawa makubwa ya kufua umeme kulisha Afrika nzima. Maziwa haya yangefanya eneo lote la sahara ambalo ni jangwa kuwa sehemu ya kilimo maana yangeathiri uoto kutokana na unyevu unaoletwa. Pia hali ya hewa ingebadilika ambapo joto lingepungua na kufanya eneo kuwa zuri kwa makazi ya wazungu pia.

Gilbraltar na sicily pia kungewekwa daraja la magari na treni kuunganisha mabara haya mawili na watu wangevuka kwa urahisi tu kupitia Tunisia na Morocco. Kiufupi mabara yangeunganishwa na kuifanya ulaya nzima kuhamia Afrika na viceversa ili kupata bara moja lenye nguvu na maisha mazuri.

Aliamini kuwa amani ingeletwa sio kwa mitutu na kelele za wanasiasa majukwaani ila kwa teknolojia ambayo ingeleta maisha bora kwa watu wote hivyo amani ingepatikana. Alipanga mataifa yote Atlantropa yaunganishwe na hiyo "gridi ya taifa" ili akitokea mkorofi mmoja kutaka kuleta vita basi anazimiwa umeme ili kumdhoofisha so ingeleta discipline kwa mataifa yote ya ulaya na Afrika.

Matokeo
Mradi huu licha ya kupata support ya baadhi ya wahandisi na viongozi wa kisiasa ila mataifa ya ulaya hayakuutilia maanani. Alitumia nguvu kubwa hata ya kumshawishi Hitler kuutimiza ili agenda yake ya kutawala dunia itimie ila pamoja na udikteta wake bado aliikataa sababu mradi unawaza kuleta amani wakati ambao ujerumani ulihubiri vita ndio suluhu ya kuwakomboa watu wake kutoka mikono ya ''wazungu''. Mpaka anafariki mwaka 1952 mradi wake haukuwahi anza utekelezaji wake na toka azikwe hajapatikana bado mtu wa kuendeleza ndoto yake hiyo ya bara kuu.

Swali langu kwa Great thinkers humu
1. Je kwanini wazungu hawakusupport mradi huu??
2. Je nini hatma ya Afrika kujikomboa kwenye ukoloni huu??
3. Je mradi huu ungefanikiwa?
4. Nini madhara ya kimazingira?
5. Na je malengo kamili ya mradi huu kuleta amani ya milele ingetimia??

Naomba kuwasilisha

image-20150911-1569-beg02y.png
 
Binafsi hata Mimi BabaMorgan kwa uzalendo wangu nisingesupport huo mpango kama leo hii sio bara moja lakini tumekuwa tunatumika kufaidisha bara la Europe ingekuwa vipi kama tungekuwa bara moja ina maana tungewarahisishia lengo lao na matokeo yake tusingekuwa na sauti kwenye maamuzi yanayohusu bara.
 
Binafsi hata Mimi BabaMorgan kwa uzalendo wangu nisingesupport huo mpango kama leo hii sio bara moja lakini tumekuwa tunatumika kufaidisha bara la Europe ingekuwa vipi kama tungekuwa bara moja ina maana tungewarahisishia lengo lao na matokeo yake tusingekuwa na sauti kwenye maamuzi yanayohusu bara.
Lakini mzalendo, huoni labda kungekua angalau na unafuu wa maisha kwa waafrika. Kama tu hukp chad na sudan kusini watu wanateseka na umaskini na vita zisizoisha je wangekua na cha kupoteza kweli kutawaliwa ila wana uhakika wa nyumba zao kuwa na umeme, kusafiri kwa treni za mwendokasi na kula balanced diet!!

Mkuu hivi unafahamu uchumi wa afrika kusini kwa mtu mweusi ulikua mzuri kuliko baada ya uhuru?? Yaani pamoja na ukoloni na mateso ila Afrika kusini ilikua na unafuu wa maisha kuliko hata baada ya uhuru wa mtu mweusi. Sasa imejaa viongozi mafisadi wanaojinufaisha wenyewe huku wakiacha weusi wenzao wakipigika kwa umaskini mkubwa.

Kiufupi sioni kama Afrika tuna la kupoteza hata kama tungeburuzwa tena maadam tungeishi kwenye bara la kijanja !!
 
Lakini mzalendo, huoni labda kungekua angalau na unafuu wa maisha kwa waafrika. Kama tu hukp chad na sudan kusini watu wanateseka na umaskini na vita zisizoisha je wangekua na cha kupoteza kweli kutawaliwa ila wana uhakika wa nyumba zao kuwa na umeme, kusafiri kwa treni za mwendokasi na kula balanced diet!!

Mkuu hivi unafahamu uchumi wa afrika kusini kwa mtu mweusi ulikua mzuri kuliko baada ya uhuru?? Yaani pamoja na ukoloni na mateso ila Afrika kusini ilikua na unafuu wa maisha kuliko hata baada ya uhuru wa mtu mweusi. Sasa imejaa viongozi mafisadi wanaojinufaisha wenyewe huku wakiacha weusi wenzao wakipigika kwa umaskini mkubwa.

Kiufupi sioni kama Afrika tuna la kupoteza hata kama tungeburuzwa tena maadam tungeishi kwenye bara la kijanja !!
Uchumi wa Afrika kusini kuwa mzuri kabla ya Uhuru haimaanishi wanufaika wakuu walikuwa watu weusi na kama kweli wote walinufaika na uwepo wa mzungu ni kwa nini palikuwa na movement za kudai Uhuru zilizopelekea vifo na mateso kwa baadhi ya wananchi weusi? Karne hii ya 21 bado kuna watu weusi wanaonekana kama nyani mwachoni mwa wazungu kiasi kwamba hawastaili huduma sawa na wazungu. Je wangefanikisha Kufanya Europa na Afrika kuwa bara moja uoni kwamba wangeanzisha mipango ya kutukandamiza na kutuaminisha kuwa sisi sio binadamu(nyani) so point ni kuwa tungekuwa sehemu ya mafanikio kiuchumi ila tusingekuwa wanufaika wa jasho letu kama ilivyotokea kipindi cha ukoloni.
 
Uchumi wa Afrika kusini kuwa mzuri kabla ya Uhuru haimaanishi wanufaika wakuu walikuwa watu weusi na kama kweli wote walinufaika na uwepo wa mzungu ni kwa nini palikuwa na movement za kudai Uhuru zilizopelekea vifo na mateso kwa baadhi ya wananchi weusi? Karne hii ya 21 bado kuna watu weusi wanaonekana kama nyani mwachoni mwa wazungu kiasi kwamba hawastaili huduma sawa na wazungu. Je wangefanikisha Kufanya Europa na Afrika kuwa bara moja uoni kwamba wangeanzisha mipango ya kutukandamiza na kutuaminisha kuwa sisi sio binadamu(nyani) so point ni kuwa tungekuwa sehemu ya mafanikio kiuchumi ila tusingekuwa wanufaika wa jasho letu kama ilivyotokea kipindi cha ukoloni.
Mkuu sasa kwa maisha ya somalia,Chad na Sudan kusini uhuru kwao una faida gani?? Kama wanakufa kwa maelfu wakizamia kwenda ulaya wanapoitwa nyani je wangeona hasara gani kubaki chini ya wazungu hapa Afrika??

Mkuu je huoni hata kama tungekuwa chini ya ukoloni bado tu maisha ya kiuchumi ya mtu mweusi yangekua na unafuu angalau kuliko hizo nchi nlizotaja hapo juu.

Cc mtu chake
 
Ulaya na Afrika ni jamii mbili zilizo mbali mbali kiuelewa na elimu ya mambo.

Mfumo wa hizi jamii bara la Ulaya na la Afrika ni mbali mbali.

Ukitumia akili kuchunguza Ulaya na Afrika unagundua tofauti kubwa ya maliasili kwa Afrika ukilinganisha na ulaya, na uelewa na elimu ya mambo na mfumo kwa Ulaya ukilinganisha na Afrika.

Nyakati zetu hatuoni teknolojia yoyote Afrika. Kadhalika uzalishaji wa uchumi.
 
Mwanadamu kwa haiba yake akiwa kwenye changamoto ndio anapata wasaa mzuri wa kuchakata akili yake ili kupata suluhisho la matatizo yanayomzunguka. Na hili ndio lilimkuta Msanifu majengo na mhandisi wa kijerumani Herman Sorgel kuja kubuni mradi wenye maono makubwa uliohitaji wafanyakazi zaidi ya million moja na kukamilika baada ya miaka 150!!
View attachment 1301280

Prologue
Herman Sorgel alikua msanifu majengo (Architect) aliyezaliwa mji wa Bavaria,ujerumani mnamo 1885 na kufariki mwaka 1952. Baada ya kushuhudia vita kuu mbili za dunia zikileta madhara makubwa na migogoro isiyoisha, mhandisi huyu ikabidi abuni mradi ambao ungeiunganisha ulaya kuwa kitu kimoja na kuepusha vita ya tatu ya dunia huku dunia nzima ikihakikishiwa amani milele sio kwa kutumia bunduki au siasa za majukwaani bali teknolojia.

Mpango wa Mradi:
View attachment 1301391
Strait of Gilbraltar
Ningependa wasomaji mfahamu kuwa umbali kati ya ulaya na Afrika ni km 14 pekee kiufupi ukiwa morocco unaiona Hispania kabisa na katika historia kuna tukio linaitwa Messinian Salinic Crisis ambapo eneo hilo la ulaya lilishikamana na eneo la Afrika hivyo bahari ya Mediterranean ikazibwa jambo lililofanya maji yasiingie kutoka Bahari ya Atlantic. Ilichukua takribani miaka kadhaa kina cha maji kilipungua sana na bara la Afrika na ulaya yaligusana kabisa kwa nchi kavu. However mafuriko makubwa yalitokea huko mbeleni na kurudisha bahari hiyo mahala pake mpaka leo hii.

Dhana hii ilimfikirisha sana Mhandisi Sorgel kwamba kma ataweza kurudia tukio hilo la kijiografia kwa kutumia mbinu za kiuhandisi basi anaweza unganisha Ulaya na Afrika kuwa bara moja lenye nguvu na tishio kuliko yote.

Kiini cha mradi ingekua pale Gilbraltar ambapo ungejengwa bwawa la kufua umeme kubwa katika historia ya dunia ambalo lingefua megawatt elfu 50. Lingekua na urefu wa mzunguko km 34 na msingi wenye urefu wa km 2.5 kwenda chini ndani ya maji na 300 m juu ya maji.

Mpango ulikuwa, angeziba bahari ya Atlantic na mito inayozunguka kma Dardenelles kuleta maji kwenye bahari ya Mediterranean ili kupunguza kina cha maji hadi kufika Mt 200 magharibi na Mt 100 mashariki.

Bwawa hili lingezuia (Divert) maji kuingia bahari ya Mediterranean hivyo kina cha maji kingepungua kwa zaidi ya mita 200. Na maji mengine yangetumika kwenye kuzalisha umeme, mradi mkubwa wa kurutubisha jangwa la sahara kwa ajili ya kilimo cha kisasa pamoja na kutenga ardhi mpya ambayo ingeunganisha mabara ya Afrika na Ulaya ili kumaliza changamoto ya udogo wa ardhi.

View attachment 1301279
Atlantropa ikikamilika mabara yangeungana hivi kwa nchi kavu

Mafanikio aliyotarajia
1.Kuwepo bara lenye nguvu kuweza kuchallenge nguvu ya America na Asia kama zingekuja kuwa tishio kiuchumi/Kisiasa.

2.Kumaliza tatizo la ajira ulaya maana wangetapakaa Huku Afrika kutafuta fursa mpya kma kilimo,madini n.k

3.Kungemaliza tatizo la ardhi ulaya maana aliona vita nyingi zilikua kugombania ardhi. Ulaya ingekua extended mpaka kusini mwa Afrika hivyo ardhi ingekua zaidi ya mahitaji.

4.Chakula kisingepungua maana ardhi mpya ingetumika kwa ajili ya kilimo na jangwa la sahara lingerutubishwa kwa mradi mkubwa wa umwagiliaji hivyo ardhi yake ingeanza kuwa na rutuba ya kukuza mimea. Yangejengwa mashamba makubwa kabisa ya kilimo cha kisasa hivyo chakula kisingewahi isha ulaya.

5.Nishati ingekuwa ya kutosha mfano huo mradi wote wa mabwawa ya umeme takribani 8 ungezalisha megawatts zaidi ya Laki moja hivyo umeme ungekuwa wa uhakika Atlantropa nzima hivyo kupunguza vita za kugombea nishati ndogo iliyobaki mfano mafuta na makaa ya mawe n.k

6.Mradi huu ungeunganisha mataifa yote ya Ulaya yaliyokua kwenye vuguvugu la vita kuu za dunia maana mradi ungehitaji ushirikiano wa mataifa yote kwenye utekelezaji na ukikamilika wangeishi kama familia moja na hivyo kusahau tofauti zao maana nishati ipo,chakula kipo,ardhi ya kumwaga!! Mpigane kwa lipi tena??!!

Utekelezaji Afrika
View attachment 1301283

Afrika ingejengwa maziwa makuu mapya mawili pale DRC kwenye mto congo na ziwa Chad lingetanuliwa kina. Hapa pia yangejengwa mabwawa makubwa ya kufua umeme kulisha Afrika nzima. Maziwa haya yangefanya eneo lote la sahara ambalo ni jangwa kuwa sehemu ya kilimo maana yangeathiri uoto kutokana na unyevu unaoletwa. Pia hali ya hewa ingebadilika ambapo joto lingepungua na kufanya eneo kuwa zuri kwa makazi ya wazungu pia.

Gilbraltar na sicily pia kungewekwa daraja la magari na treni kuunganisha mabara haya mawili na watu wangevuka kwa urahisi tu kupitia Tunisia na Morocco. Kiufupi mabara yangeunganishwa na kuifanya ulaya nzima kuhamia Afrika na viceversa ili kupata bara moja lenye nguvu na maisha mazuri.

Aliamini kuwa amani ingeletwa sio kwa mitutu na kelele za wanasiasa majukwaani ila kwa teknolojia ambayo ingeleta maisha bora kwa watu wote hivyo amani ingepatikana. Alipanga mataifa yote Atlantropa yaunganishwe na hiyo "gridi ya taifa" ili akitokea mkorofi mmoja kutaka kuleta vita basi anazimiwa umeme ili kumdhoofisha so ingeleta discipline kwa mataifa yote ya ulaya na Afrika.

Matokeo
Mradi huu licha ya kupata support ya baadhi ya wahandisi na viongozi wa kisiasa ila mataifa ya ulaya hayakuutilia maanani. Alitumia nguvu kubwa hata ya kumshawishi Hitler kuutimiza ili agenda yake ya kutawala dunia itimie ila pamoja na udikteta wake bado aliikataa sababu mradi unawaza kuleta amani wakati ambao ujerumani ulihubiri vita ndio suluhu ya kuwakomboa watu wake kutoka mikono ya ''wazungu''. Mpaka anafariki mwaka 1952 mradi wake haukuwahi anza utekelezaji wake na toka azikwe hajapatikana bado mtu wa kuendeleza ndoto yake hiyo ya bara kuu.

Swali langu kwa Great thinkers humu
1. Je kwanini wazungu hawakusupport mradi huu??
2. Je nini hatma ya Afrika kujikomboa kwenye ukoloni huu??
3. Je mradi huu ungefanikiwa?
4. Nini madhara ya kimazingira?
5. Na je malengo kamili ya mradi huu kuleta amani ya milele ingetimia??

Naomba kuwasilisha

View attachment 1301281
IKO WAZI WAZUNGU WENGI WALIKUWA WANA TUCHUKIA ;MIAKA HIYO ILA KWA SASA WANA TUTAFUTA SANA MAANA WANAJUA WENGI WETU TUNA HUGECOCK.
WANATUSUMBUA NATUNAWAOA TU MIAKA KAMA 20 MBELENI UBAGUZI UTAISHA KABISA.... ILA KAMA TUTAPATA PESA TUKAWAGEGEDE UKO KWAO TUWAPUNGUZIE GHARAMA ZAKUJA HUKU
 
Ulaya na Afrika ni jamii mbili zilizo mbali mbali kiuelewa na elimu ya mambo.

Mfumo wa hizi jamii bara la Ulaya na la Afrika ni mbali mbali.

Ukitumia akili kuchunguza Ulaya na Afrika unagundua tofauti kubwa ya maliasili kwa Afrika ukilinganisha na ulaya, na uelewa na elimu ya mambo na mfumo kwa Ulaya ukilinganisha na Afrika.

Nyakati zetu hatuoni teknolojia yoyote Afrika. Kadhalika uzalishaji wa uchumi.
Kwa maoni yako huu mradi ungeleta faida kwa waafrika?? Je unadhani amani ya kweli afrika na ulaya ingepatikana baada ya kuungana kuwa bara moja?
 
Mwanadamu kwa haiba yake akiwa kwenye changamoto ndio anapata wasaa mzuri wa kuchakata akili yake ili kupata suluhisho la matatizo yanayomzunguka. Na hili ndio lilimkuta Msanifu majengo na mhandisi wa kijerumani Herman Sorgel kuja kubuni mradi wenye maono makubwa uliohitaji wafanyakazi zaidi ya million moja na kukamilika baada ya miaka 150!!
View attachment 1301280

Prologue
Herman Sorgel alikua msanifu majengo (Architect) aliyezaliwa mji wa Bavaria,ujerumani mnamo 1885 na kufariki mwaka 1952. Baada ya kushuhudia vita kuu mbili za dunia zikileta madhara makubwa na migogoro isiyoisha, mhandisi huyu ikabidi abuni mradi ambao ungeiunganisha ulaya kuwa kitu kimoja na kuepusha vita ya tatu ya dunia huku dunia nzima ikihakikishiwa amani milele sio kwa kutumia bunduki au siasa za majukwaani bali teknolojia.

Mpango wa Mradi:
View attachment 1301391
Strait of Gilbraltar
Ningependa wasomaji mfahamu kuwa umbali kati ya ulaya na Afrika ni km 14 pekee kiufupi ukiwa morocco unaiona Hispania kabisa na katika historia kuna tukio linaitwa Messinian Salinic Crisis ambapo eneo hilo la ulaya lilishikamana na eneo la Afrika hivyo bahari ya Mediterranean ikazibwa jambo lililofanya maji yasiingie kutoka Bahari ya Atlantic. Ilichukua takribani miaka kadhaa kina cha maji kilipungua sana na bara la Afrika na ulaya yaligusana kabisa kwa nchi kavu. However mafuriko makubwa yalitokea huko mbeleni na kurudisha bahari hiyo mahala pake mpaka leo hii.

Dhana hii ilimfikirisha sana Mhandisi Sorgel kwamba kma ataweza kurudia tukio hilo la kijiografia kwa kutumia mbinu za kiuhandisi basi anaweza unganisha Ulaya na Afrika kuwa bara moja lenye nguvu na tishio kuliko yote.

Kiini cha mradi ingekua pale Gilbraltar ambapo ungejengwa bwawa la kufua umeme kubwa katika historia ya dunia ambalo lingefua megawatt elfu 50. Lingekua na urefu wa mzunguko km 34 na msingi wenye urefu wa km 2.5 kwenda chini ndani ya maji na 300 m juu ya maji.

Mpango ulikuwa, angeziba bahari ya Atlantic na mito inayozunguka kma Dardenelles kuleta maji kwenye bahari ya Mediterranean ili kupunguza kina cha maji hadi kufika Mt 200 magharibi na Mt 100 mashariki.

Bwawa hili lingezuia (Divert) maji kuingia bahari ya Mediterranean hivyo kina cha maji kingepungua kwa zaidi ya mita 200. Na maji mengine yangetumika kwenye kuzalisha umeme, mradi mkubwa wa kurutubisha jangwa la sahara kwa ajili ya kilimo cha kisasa pamoja na kutenga ardhi mpya ambayo ingeunganisha mabara ya Afrika na Ulaya ili kumaliza changamoto ya udogo wa ardhi.

View attachment 1301279
Atlantropa ikikamilika mabara yangeungana hivi kwa nchi kavu

Mafanikio aliyotarajia
1.Kuwepo bara lenye nguvu kuweza kuchallenge nguvu ya America na Asia kama zingekuja kuwa tishio kiuchumi/Kisiasa.

2.Kumaliza tatizo la ajira ulaya maana wangetapakaa Huku Afrika kutafuta fursa mpya kma kilimo,madini n.k

3.Kungemaliza tatizo la ardhi ulaya maana aliona vita nyingi zilikua kugombania ardhi. Ulaya ingekua extended mpaka kusini mwa Afrika hivyo ardhi ingekua zaidi ya mahitaji.

4.Chakula kisingepungua maana ardhi mpya ingetumika kwa ajili ya kilimo na jangwa la sahara lingerutubishwa kwa mradi mkubwa wa umwagiliaji hivyo ardhi yake ingeanza kuwa na rutuba ya kukuza mimea. Yangejengwa mashamba makubwa kabisa ya kilimo cha kisasa hivyo chakula kisingewahi isha ulaya.

5.Nishati ingekuwa ya kutosha mfano huo mradi wote wa mabwawa ya umeme takribani 8 ungezalisha megawatts zaidi ya Laki moja hivyo umeme ungekuwa wa uhakika Atlantropa nzima hivyo kupunguza vita za kugombea nishati ndogo iliyobaki mfano mafuta na makaa ya mawe n.k

6.Mradi huu ungeunganisha mataifa yote ya Ulaya yaliyokua kwenye vuguvugu la vita kuu za dunia maana mradi ungehitaji ushirikiano wa mataifa yote kwenye utekelezaji na ukikamilika wangeishi kama familia moja na hivyo kusahau tofauti zao maana nishati ipo,chakula kipo,ardhi ya kumwaga!! Mpigane kwa lipi tena??!!

Utekelezaji Afrika
View attachment 1301283

Afrika ingejengwa maziwa makuu mapya mawili pale DRC kwenye mto congo na ziwa Chad lingetanuliwa kina. Hapa pia yangejengwa mabwawa makubwa ya kufua umeme kulisha Afrika nzima. Maziwa haya yangefanya eneo lote la sahara ambalo ni jangwa kuwa sehemu ya kilimo maana yangeathiri uoto kutokana na unyevu unaoletwa. Pia hali ya hewa ingebadilika ambapo joto lingepungua na kufanya eneo kuwa zuri kwa makazi ya wazungu pia.

Gilbraltar na sicily pia kungewekwa daraja la magari na treni kuunganisha mabara haya mawili na watu wangevuka kwa urahisi tu kupitia Tunisia na Morocco. Kiufupi mabara yangeunganishwa na kuifanya ulaya nzima kuhamia Afrika na viceversa ili kupata bara moja lenye nguvu na maisha mazuri.

Aliamini kuwa amani ingeletwa sio kwa mitutu na kelele za wanasiasa majukwaani ila kwa teknolojia ambayo ingeleta maisha bora kwa watu wote hivyo amani ingepatikana. Alipanga mataifa yote Atlantropa yaunganishwe na hiyo "gridi ya taifa" ili akitokea mkorofi mmoja kutaka kuleta vita basi anazimiwa umeme ili kumdhoofisha so ingeleta discipline kwa mataifa yote ya ulaya na Afrika.

Matokeo
Mradi huu licha ya kupata support ya baadhi ya wahandisi na viongozi wa kisiasa ila mataifa ya ulaya hayakuutilia maanani. Alitumia nguvu kubwa hata ya kumshawishi Hitler kuutimiza ili agenda yake ya kutawala dunia itimie ila pamoja na udikteta wake bado aliikataa sababu mradi unawaza kuleta amani wakati ambao ujerumani ulihubiri vita ndio suluhu ya kuwakomboa watu wake kutoka mikono ya ''wazungu''. Mpaka anafariki mwaka 1952 mradi wake haukuwahi anza utekelezaji wake na toka azikwe hajapatikana bado mtu wa kuendeleza ndoto yake hiyo ya bara kuu.

Swali langu kwa Great thinkers humu
1. Je kwanini wazungu hawakusupport mradi huu??
2. Je nini hatma ya Afrika kujikomboa kwenye ukoloni huu??
3. Je mradi huu ungefanikiwa?
4. Nini madhara ya kimazingira?
5. Na je malengo kamili ya mradi huu kuleta amani ya milele ingetimia??

Naomba kuwasilisha

View attachment 1301281
PILI HUU MRADI ULIANGUKIA KIPINDI KIBAYA ULAYA KULIKUWA NA UTENGANO SANA
 
A
Je unadhani amani ya kweli afrika na ulaya ingepatikana baada ya kuungana kuwa bara moja?
Amani haipatikani katika vitu au miradi au maendeleo ya uchumi.

Maendeleo au uchumi mzuri ni mambo ya msingi sana kwa jamii. Yakikosekana ni tatizo kubwa sana.

Lakini haya hayawezi kufikiriwa kama kwa kuwa nayo huleta amani.

Kinachowaunganisha watu sio miradi, sio hali nzuri ya uchumi au maendeleo.

Kwasababu haya yote ukiyatafiti utaona ni matokeo yanayokuja kufuatia kutekeleza vema nyajibu.
 
Waafrka hatujawahi kuwa na akili ya kutakiana mema!

Hatutaepuka kutawaliwa, wameacha physically.

Wenzetu wazungu wako kwenye AI tech, sisi huku tunapambana kunyamazishana.
 
Back
Top Bottom