Athumani iddi chuji

Swahilian

JF-Expert Member
Apr 28, 2009
591
66
CHUJI

Athumani Idi chuji, mwanasoka Tanzania.
Amejaliwa vipaji, nashindwa kuelezea.
Kakosa tu uchugaji,kondoo wangemezea.
Hiki kipaji cha chuji, ni matatizo makubwa.

Mpira kakomalia, shule hakupendelea.
Mama alikubalia,kandanda we endelea.
Wengi akawavutia ,nyotaye kuongelea.
Hiki kipaji cha soka,au cha kusingizia.

Ikawa chuji na Simba,wafurahi kidedea.
Ukuta kashika nyumba, msimbazi kupepea.
Sokani walikukumba, bado uliwachekea.
Hivi soka ikipanda , akili zenu huruka?

Mara ukaaanza kuponda, sekeseke za chakula.
Ugomvi na wako nyanda, kisa chenu ni Jamila.
Huna raha ukakonda, Simba ikawa madhila.
Hiki kipaji cha Idi, kina wingi wa vituko.

Usajili tafrani, hutaki tena nyumbani.
Wasema huna amani,wataka kwenda jangwani.
Wang’ang’ania benchini, nyumba mpya twigani.
Kipaji cha Brambati, sijaona duniani.

Kifungo kikawa mwisho, ukarudi uwanjani.
Tuliona zako jasho, ulijituma dimbani.
Walikwongeza na posho, washinda mwao vinywani.
Athumani wa kipaji, mwige nduguyo Pius

Taifa zima gumzo, madebe ukapigiwa.
Maximo akwite mwanzo, kiungo bora kaitwa.
Ukaanza zako bezo, dole kati likasutwa.
Chuji hiki kipaji, kutukana mashabiki?

Tamati yanigongea ,sifaze nisiandike.
Sisahau ya Songea, yachekesha ya Mwandike.
Soka hawakuchelea, miezi sita wamweke.
Idi kipaji tumia, u’huru sasa tulia.

 
Swahilian acha majungu tuletee tungo za kuamsha mioyo ya uzalendo kwa taifa letu linalodidimia, hicho si kitu muhimu ambacho watu tungependa kujishughulisha kufikiria kwa sasa
 
Pole sana Ndugu yangu!!1. jifunze kufikiri zaidi na ujue yapi majungu na zipi ni sifa na ipi ni hali halisi, je! haya hayatuhusu wanajamii,au weye si kati ya wanajamii? mie si mwanamajungu kama ufikiriavyo na hata siku moja sifundishi kuandika kama wewe usivyofundishwa kunishuku! amani iwe kwako, majibizano na ubishani ni hamasa kwa wasaka ukweli! japo si siku zote!! rudia tena na tena!!
 
CHUJI

Athumani Idi chuji, mwanasoka Tanzania.
Amejaliwa vipaji, nashindwa kuelezea.
Kakosa tu uchugaji,kondoo wangemezea.
Hiki kipaji cha chuji, ni matatizo makubwa.

Mpira kakomalia, shule hakupendelea.
Mama alikubalia,kandanda we endelea.
Wengi akawavutia ,nyotaye kuongelea.
Hiki kipaji cha soka,au cha kusingizia.

Ikawa chuji na Simba,wafurahi kidedea.
Ukuta kashika nyumba, msimbazi kupepea.
Sokani walikukumba, bado uliwachekea.
Hivi soka ikipanda , akili zenu huruka?

Mara ukaaanza kuponda, sekeseke za chakula.
Ugomvi na wako nyanda, kisa chenu ni Jamila.
Huna raha ukakonda, Simba ikawa madhila.
Hiki kipaji cha Idi, kina wingi wa vituko.

Usajili tafrani, hutaki tena nyumbani.
Wasema huna amani,wataka kwenda jangwani.
Wang’ang’ania benchini, nyumba mpya twigani.
Kipaji cha Brambati, sijaona duniani.

Kifungo kikawa mwisho, ukarudi uwanjani.
Tuliona zako jasho, ulijituma dimbani.
Walikwongeza na posho, washinda mwao vinywani.
Athumani wa kipaji, mwige nduguyo Pius

Taifa zima gumzo, madebe ukapigiwa.
Maximo akwite mwanzo, kiungo bora kaitwa.
Ukaanza zako bezo, dole kati likasutwa.
Chuji hiki kipaji, kutukana mashabiki?

Tamati yanigongea ,sifaze nisiandike.
Sisahau ya Songea, yachekesha ya Mwandike.
Soka hawakuchelea, miezi sita wamweke.
Idi kipaji tumia, u’huru sasa tulia.
stuing artism
kipaji kizuri endelea hivyohivyo na utunzni mzuri
mependa sana jinsi ulivyoweza kufikiria na kutunza ujumbe wako hasa kwa mtu kama chuji mwenye majimambo na kipaji
tuletee nyingine basi
Great
 
Ukuta kashika nyumba, yamaanisha sehemu ya ulinzi alikwepo Victor Costa a.k.a nyumba. Nafkiri umenipata hapo. Poa kakaa!
 
Back
Top Bottom