Fidel80
JF-Expert Member
- May 3, 2008
- 21,947
- 4,444
VIUNGO wazoefu wa ushambuliaji wa timu ya soka ya taifa 'Taifa Stars', Athuman Idd 'Chuji' na Haruna Moshi �Boban� wamejitoa katika kikosi hicho kinachofundishwa na kocha Mbrazili, Marcio Maximo.
Haruna kutoka Simba na Idd wa Yanga wamefikia hatua hiyo kutokana na kutoelewana na kocha huyo ambaye ameshindwa kuwapanga katika fainali za Mataifa ya Afrika kwa wachezaji wa ndani (CHAN) ukiondoa Haruna ambaye alicheza mechi ya kwanza dhidi ya Senegal kwa dakika zisizozidi thelathini.
Habari za uhakika ambazo Mwanaspoti imezipata jijini hapa zinasema wachezaji hao wamejitoa Stars katika kipindi chote ambacho itakuwa chini ya Mbrazili huyo kwa madai kuwa amewadhalilisha baada ya kuwaweka benchi huku akitangaza kwa wananchi kuwa ni wagonjwa wakati ni wazima wa afya njema.
"Chuji na Boban wanaonekana kama wakimbizi, wameamua kujitoa ingawa kuna wakati wamekuwa wakifikiria watu watawaelewa vibaya. Lakini jana (juzi Jumapili), wamekubaliana kuachana na Taifa Stars," alisema mchezaji wa karibu na wachezaji hao.
"Wameona wakiendelea kuwa chini ya Maximo kamwe hawawezi kuisaidia Stars na yataendelea kuwa malumbano kwa kuwa tayari ameonyesha kinyongo dhidi yao na amekuwa hataki kuwachezesha lakini kila anapoulizwa na waandishi wa habari anazungusha maneno kibao bila ya kusema ukweli.
"Boban na Chuji wamepanga kuwa wakifika Dar es Salaam walizungumzie suala hilo kwa undani, ndio maana unaona wamekuwa wakifanya mazoezi pekee yao baada ya Maximo kuwatenga. Unaona maisha yao kama juzi kawashusha kwenye basi tena mbele ya watu," alisema mchezaji huyo.
Jumamosi usiku baada ya Stars kuwasili kwenye hoteli ya The President mjini Yaomossokro ikitokea Bouake ambako walimaliza mechi yao ya mwisho dhidi ya Zambia kwa sare ya bao 1-1, Maximo aliwataka wachezaji waliocheza na wale waliokuwa kwenye benchi kubaki kwenye basi.
Bila ya kutaja majina alisema; �Wale waliocheza na waliokuwa kwenye benchi ndio wabaki kwenye basi tuzungumze."
Hali hiyo iliwafanya Chuji na Boban wateremke kimya kimya na kupitiliza hadi vyumbani kwenda kujifungia. Lakini baada ya dakika 15, Maximo alifanya mkutano na waandishi wa habari na alipoulizwa sababu ya kuteremka wachezaji hao alisema kauli tofauti.
"Unajua tumetoka sare, ambayo imetuathiri, huenda wachezaji wengine wana uchungu ndio maana wameshuka kwenye basi wanataka kujipumzisha, huwezi kuwakata na hakuna chochote kibaya," alijibu.
Mwanaspoti iliwasaka Boban na Chuji kila mtu kwa wakati wake na kukiri kwamba walishushwa kwenye basi na Maximo. "Alisema waliocheza na waliokuwa kwenye benchi ndio wabaki kwenye basi, sisi tulikuwa jukwaani wakati wa mechi. Hakutaja majina lakini mtu mzima unaelewa huhitaji kusukumwa," alisema Boban na alipoulizwa suala la kujitoa kwenye timu alisema.
"Nipo katika mazingira magumu sana, mimi huwa si mzungumzaji lakini wakati huu nitazungumza. Naomba unipe muda, kuna maamuzi ambayo nimefikia na nisingependa kuyaharakisha."
Lakini kwa upande wa Chuji ambaye pia alikiri kuteremshwa kwenye basi, kuhusu suala la kujitoa alisema; "Uamuzi huo ni mzito, kama utakuwa umefikiwa unataka busara na ushauri. Lakini kuna ambacho nimefikia hata kama kuna ambao hawatapenda lakini sipendi kuendelea kuumia kama nilivyoishi huku Ivory Coast. Nitasema kila kitu baada ya kufika Dar es Salaam, ni vizuri kuyamaliza haya tukiwa nyumbani.
"Unaniona niko huku, mimi ni kama askari ambaye nimekuja kutetea taifa langu. Lakini pamoja na kuwa na bunduki siruhusiwi kufyatua risasi wakati naona wenzangu wanashambuliwa. Inaniuma sana kweli, ila naomba uvumilie ikifika siku nitasema tu wacha nirudi nyumbani kwanza," alisema Chuji.
Maximo alikataa katakata kwa mara nyingine kwamba kuna ugomvi ndani ya timu hiyo na kusisitiza kuwa suala la nidhamu anaendelea kulipa nafasi na yoyote ambaye hatataka kulifuata basi hatapata nafasi katika kikosi chake.
Siku chache zilizopita alisema kikosi atakachochagua kwa mara nyingine kitajali damu mpya zaidi kwani amegundua majina hayana msaada.
Bado chanzo cha tafrani la Maximo, Boban na Chuji hakijajulikana vizuri ingawa kila upande unaushutumu mwingine kwa kutokuwa na nidhamu au kuwa na dharau kwa upande mwingine.
Wiki iliyopita Mbrazili huyo alitaka wachezaji hao warudishwe Dar es Salaam, lakini busara za Waziri, Seif Khatib ndio zilifanya wabaki baada ya kukataza mtu yoyote kurudishwa ingawa maamuzi ya mwisho ya kikao yalifikiwa kwamba kocha ndiye mwenye uamuzi wa mwisho kama ataamua kuwapanga au kutowapanga uwanjani.
Hii ni mara ya pili kwa Maximo kuingia kwenye tafrani kubwa na wachezaji mara ya kwanza ikiwa ni dhidi ya kipa Juma Kaseja ambaye amesusa kabisa kumuita katika kikosi chake huku akiwa hataki kutoa sababu za uhakika.
Pamoja na ubora wake katika ufundishaji, moja ya kasoro kubwa ya kocha huyo imekuwa ni suala la kukasirika mara kwa mara na pia kuweka visasi kitu ambacho wadau wamekuwa wakimuasa kuachana navyo kwa faida ya kikosi chake.
Habari za ndani zinasema kuwa Maximo amepanga kukivunja kikosi chake atakaporejea nchini na kwamba anataka kuunda kikosi kipya cha vijana wengi.
Source;Mwanaspoti
Haruna kutoka Simba na Idd wa Yanga wamefikia hatua hiyo kutokana na kutoelewana na kocha huyo ambaye ameshindwa kuwapanga katika fainali za Mataifa ya Afrika kwa wachezaji wa ndani (CHAN) ukiondoa Haruna ambaye alicheza mechi ya kwanza dhidi ya Senegal kwa dakika zisizozidi thelathini.
Habari za uhakika ambazo Mwanaspoti imezipata jijini hapa zinasema wachezaji hao wamejitoa Stars katika kipindi chote ambacho itakuwa chini ya Mbrazili huyo kwa madai kuwa amewadhalilisha baada ya kuwaweka benchi huku akitangaza kwa wananchi kuwa ni wagonjwa wakati ni wazima wa afya njema.
"Chuji na Boban wanaonekana kama wakimbizi, wameamua kujitoa ingawa kuna wakati wamekuwa wakifikiria watu watawaelewa vibaya. Lakini jana (juzi Jumapili), wamekubaliana kuachana na Taifa Stars," alisema mchezaji wa karibu na wachezaji hao.
"Wameona wakiendelea kuwa chini ya Maximo kamwe hawawezi kuisaidia Stars na yataendelea kuwa malumbano kwa kuwa tayari ameonyesha kinyongo dhidi yao na amekuwa hataki kuwachezesha lakini kila anapoulizwa na waandishi wa habari anazungusha maneno kibao bila ya kusema ukweli.
"Boban na Chuji wamepanga kuwa wakifika Dar es Salaam walizungumzie suala hilo kwa undani, ndio maana unaona wamekuwa wakifanya mazoezi pekee yao baada ya Maximo kuwatenga. Unaona maisha yao kama juzi kawashusha kwenye basi tena mbele ya watu," alisema mchezaji huyo.
Jumamosi usiku baada ya Stars kuwasili kwenye hoteli ya The President mjini Yaomossokro ikitokea Bouake ambako walimaliza mechi yao ya mwisho dhidi ya Zambia kwa sare ya bao 1-1, Maximo aliwataka wachezaji waliocheza na wale waliokuwa kwenye benchi kubaki kwenye basi.
Bila ya kutaja majina alisema; �Wale waliocheza na waliokuwa kwenye benchi ndio wabaki kwenye basi tuzungumze."
Hali hiyo iliwafanya Chuji na Boban wateremke kimya kimya na kupitiliza hadi vyumbani kwenda kujifungia. Lakini baada ya dakika 15, Maximo alifanya mkutano na waandishi wa habari na alipoulizwa sababu ya kuteremka wachezaji hao alisema kauli tofauti.
"Unajua tumetoka sare, ambayo imetuathiri, huenda wachezaji wengine wana uchungu ndio maana wameshuka kwenye basi wanataka kujipumzisha, huwezi kuwakata na hakuna chochote kibaya," alijibu.
Mwanaspoti iliwasaka Boban na Chuji kila mtu kwa wakati wake na kukiri kwamba walishushwa kwenye basi na Maximo. "Alisema waliocheza na waliokuwa kwenye benchi ndio wabaki kwenye basi, sisi tulikuwa jukwaani wakati wa mechi. Hakutaja majina lakini mtu mzima unaelewa huhitaji kusukumwa," alisema Boban na alipoulizwa suala la kujitoa kwenye timu alisema.
"Nipo katika mazingira magumu sana, mimi huwa si mzungumzaji lakini wakati huu nitazungumza. Naomba unipe muda, kuna maamuzi ambayo nimefikia na nisingependa kuyaharakisha."
Lakini kwa upande wa Chuji ambaye pia alikiri kuteremshwa kwenye basi, kuhusu suala la kujitoa alisema; "Uamuzi huo ni mzito, kama utakuwa umefikiwa unataka busara na ushauri. Lakini kuna ambacho nimefikia hata kama kuna ambao hawatapenda lakini sipendi kuendelea kuumia kama nilivyoishi huku Ivory Coast. Nitasema kila kitu baada ya kufika Dar es Salaam, ni vizuri kuyamaliza haya tukiwa nyumbani.
"Unaniona niko huku, mimi ni kama askari ambaye nimekuja kutetea taifa langu. Lakini pamoja na kuwa na bunduki siruhusiwi kufyatua risasi wakati naona wenzangu wanashambuliwa. Inaniuma sana kweli, ila naomba uvumilie ikifika siku nitasema tu wacha nirudi nyumbani kwanza," alisema Chuji.
Maximo alikataa katakata kwa mara nyingine kwamba kuna ugomvi ndani ya timu hiyo na kusisitiza kuwa suala la nidhamu anaendelea kulipa nafasi na yoyote ambaye hatataka kulifuata basi hatapata nafasi katika kikosi chake.
Siku chache zilizopita alisema kikosi atakachochagua kwa mara nyingine kitajali damu mpya zaidi kwani amegundua majina hayana msaada.
Bado chanzo cha tafrani la Maximo, Boban na Chuji hakijajulikana vizuri ingawa kila upande unaushutumu mwingine kwa kutokuwa na nidhamu au kuwa na dharau kwa upande mwingine.
Wiki iliyopita Mbrazili huyo alitaka wachezaji hao warudishwe Dar es Salaam, lakini busara za Waziri, Seif Khatib ndio zilifanya wabaki baada ya kukataza mtu yoyote kurudishwa ingawa maamuzi ya mwisho ya kikao yalifikiwa kwamba kocha ndiye mwenye uamuzi wa mwisho kama ataamua kuwapanga au kutowapanga uwanjani.
Hii ni mara ya pili kwa Maximo kuingia kwenye tafrani kubwa na wachezaji mara ya kwanza ikiwa ni dhidi ya kipa Juma Kaseja ambaye amesusa kabisa kumuita katika kikosi chake huku akiwa hataki kutoa sababu za uhakika.
Pamoja na ubora wake katika ufundishaji, moja ya kasoro kubwa ya kocha huyo imekuwa ni suala la kukasirika mara kwa mara na pia kuweka visasi kitu ambacho wadau wamekuwa wakimuasa kuachana navyo kwa faida ya kikosi chake.
Habari za ndani zinasema kuwa Maximo amepanga kukivunja kikosi chake atakaporejea nchini na kwamba anataka kuunda kikosi kipya cha vijana wengi.
Source;Mwanaspoti