pingli-nywee
JF-Expert Member
- Sep 16, 2015
- 11,923
- 13,344
Matayarisho ya kukwapua medali na kuendeleza heshima ya Kenya kimataifa kwenye riadha yameanza kwa bashasha. Baada ya muda mrefu wa kimya kikubwa kwenye ulingo wa michuano ya riadha kimataifa, kisa athari za janga la COVID-19. Hii ni baada ya Athletics Kenya(AK) kutangaza rasmi wanariadha watakaojumuishwa kwenye #TeamKenya kwa kitengo cha marathon ndani ya mchuano wa Olympiki Tokyo 2021.
Mashindano hayo yataanza rasmi tarehe 23 Julai 2021 baada ya kuhairishwa kwa mwaka mzima. Kenya itawakilishwa kwenye marathon na mabingwa wanane(wanne kwa kina dada na hivyo hivyo kwa wanaume), wakiwemo mabingwa Eliud Kipchoge na Brigid Kosgei ambao wanashikilia rekodi za dunia kwenye mbio za wanaume na wanawake mtawalia.
AK ina matumaini ya mafanikio makubwa kule Tokyo na sio kwenye mbio za marathon tu. Ikizingatiwa kwamba wanariadha wa Kenya wamekuwa wakiendelea na mazoezi ya kujitayarisha kwa mashindano ya Olimpiki, bila kusitasita, kwa muda wote huo. Matayarisho yanaendelea kwa kina kwa michuano ya kufuzu kwa wanariadha wengine wa Kenya, kwenye mbio zingine zote ambazo watajitosa uwanjani na kushiriki kule Tokyo.
All the best to our beloved CHAMPIONS! Bendera mashuhuri ya Kenya lazima itapepea juu zaidi, bila shaka.
Athletics Kenya names Olympic marathon team - Canadian Running Magazine
Mashindano hayo yataanza rasmi tarehe 23 Julai 2021 baada ya kuhairishwa kwa mwaka mzima. Kenya itawakilishwa kwenye marathon na mabingwa wanane(wanne kwa kina dada na hivyo hivyo kwa wanaume), wakiwemo mabingwa Eliud Kipchoge na Brigid Kosgei ambao wanashikilia rekodi za dunia kwenye mbio za wanaume na wanawake mtawalia.
AK ina matumaini ya mafanikio makubwa kule Tokyo na sio kwenye mbio za marathon tu. Ikizingatiwa kwamba wanariadha wa Kenya wamekuwa wakiendelea na mazoezi ya kujitayarisha kwa mashindano ya Olimpiki, bila kusitasita, kwa muda wote huo. Matayarisho yanaendelea kwa kina kwa michuano ya kufuzu kwa wanariadha wengine wa Kenya, kwenye mbio zingine zote ambazo watajitosa uwanjani na kushiriki kule Tokyo.
All the best to our beloved CHAMPIONS! Bendera mashuhuri ya Kenya lazima itapepea juu zaidi, bila shaka.
Athletics Kenya names Olympic marathon team - Canadian Running Magazine