Tuko
JF-Expert Member
- Jul 29, 2010
- 11,178
- 7,319
Ni bayana kuwa katika kipindi cha takribani mwaka mmoja viongozi wa baraza kuu la waislamu Tanzania BAKWATA pamoja na viongozi wengine wa taasisi za kiislamu, wamekuwa kwa namna tofauti, na wakati tofauti wakichochea chuki kwa waislamu dhidi ya CHADEMA.
Sio lengo la makala yangu kueleza chimbuko ama namna ambavyo viongozi hawa wamekuwa wakijenga uhasama huo kwani naamini wananchi wengi hayo wanayajua. Naomba nieleze kwa maoni yangu na kwa kuzingatia yale ninayoyaona athari za hatua hii inayochukuliwa na viongozi wa waislamu.
Naamini kama watu wenye akili timamu wanazo sababu zao za kujenga mazingira ya kuikosashe CHADEMA nafasi za kuongoza wananchi. Hilo sina tatizo nalo, ila wasiwasi wangu ni yatokanayo na hatua hizi walizochukua ndugu zetu. Sio sahihi kusema Tanzania hatujawahi kuwa na chembechembe za chuki za kidini, zimekuwepo lakini katika level ndogo isiyo na madhara makubwa (naamini kuna watu wenye maoni tofauti katika hili, nayaheshimu). Hata hivyo katika miaka ya karibuni, kwa kiasi kikubwa watanzania tulikuwa tunaaminiana licha ya kuwa na dini tofauti.
Ni jambo la kusikitisha kuwa chuki iliyojengwa na viongozi wa kiislamu dhidi ya CHADEMA imeanza, tena kwa kasi ya kutisha kurudisha chokochoko na chuki za kidini. Ingawa sio rahisi sana kuligundua hili, lakini siku hizi katika makundi ya watu, tayari kuna asilimia kubwa ambao wanaamini mtu anayeitwa Abdalah ni lazima atakuwa anashabikia chama fulani, na mtu anayeitwa Peter, anashabikia chama fulani. Kwa bahati mbaya zaidi kumekuwa na asilimia inayoongezeka kila kukicha ya watu ambao wanawa-treat watanzania wenzao kwa kuzingatia itikadi zao za kisiasa, ambazo 'wanazijua' kutokana na dini ya mtu. Miaka michache iliyopita ilikuwa ni nadra sana mtu kupewa au kunyimwa ajira, kwa sababu wa dini yake. Amini msiamini, kwa kipindi cha mwaka mmoja tu tangu viongozi wa waislamu walipoanza kuhubiri chuki dhidi ya CHADEMA, ubaguzi wa kidini umeshaanza kurudi tena kwa kasi ya ajabu.
Kwa mfano zipo taarifa za uhakika kuwa siku hizi kuna wahadhiri wa vyuo ambao mwanafunzi mwenye jina linaloashiria dini fulani hawezi kupata A kwenye somo lake. Mbaya zaidi wapo wengine wanadiriki kujitahidi kuwafelisha wanafunzi wanaodhaniwa kuwa wafuasi wazuri wa dini zao ama kwa mavazi wanayovaa, au matendo mengine. Wapo mabosi wengi ambao kama upo uwezekano, basi watajitahidi kwa nguvu zote kuhakikisha kuwa mtu mwenye jina linaloashiria dini fulani hatakuwa mfanyakazi wake. Mnaweza mkadhani kuwa naongeza chumvi katika hili lakini kama unaweza kusoma 'mioyo' ya watu, yapo maeneo mengine hata ile kusalimiana kwa 'moyo', kushirikiana kaitka mambo ya kijamii na kadhalika kumeshaathiriwa vibaya sana na itikadi za kisiasa, zinazotokana na udini. Ubaguzi umeshaanza kuota mizizi mahospitalini, mashuleni, wapo wanaoamini hata selection ya wanafunzi inaangalia dini, selection ya wanaokopeshwa kusoma vyuo vikuu inaangalia dini n.k, kisa kwa sababu dini yako ndiyo imefanya mbunge niliyemtaka asichaguliwe na mambo kama hayo.
Tunaweza tusikatane kwa mapanga kwa sasa, lakini athari za tatizo hili endapo likiendelea kufumbiwa macho na viongozi wetu wa dini na siasa, kama ilivyo sasa zitakuwa kubwa zaidi ya kukatana mapanga. Sitaki kuamini hivyo, lakini kama ni kweli kuna kundi moja la dini lililo na nafasi zaidi katika huduma za jamii, basi ni dhahiri kuwa kundi jingine lenye nafasi ndogo katika huduma za jamii litaumia. Kama walimu wakiamua kupendelea wanafunzi kwa imani zao, kama madaktari wakiamua kupendelea huduma kwa waumini wenzao, kama wahadhiri wakiamua kufaulisha au kufelisha wanafunzi kulingana na dini zao, kama waajiri wakiamua kuajiri watu waumini wenzao, mwisho wa siku viongozi wa dini au viongozi wa siasa hawataumia moja kwa moja, bali wananchi na waumini wa kawaida ndio watakaoumia.
Najua waislamu wamekuwa na madai kadhaa wanayotaka serikali iwatekelezee kama waislamu. Sioni namna yeyote ambayo madai hayo yatatekelezwa kwa kuwachukia CHADEMA, japo kwa maoni yangu. Siku zote nimekuwa nikiamini katika diplomasia na mazungumzo. Ni matumaini yangu kuwa ili mengi ya madai ya waislamu yaweze kutekelezwa, yatahitaji kuridhiwa katika vyombo vya maamuzi vya nchi hii, ambavyo bila shaka vinaundwa na watu wenye itikadi tofauti za kisiasa. Sioni sababu yeyote ya waislamu kukata tamaa ya kushawishi na kuamua kutumia mbinu ya kuwagawa watoa maamuzi kwa itikadi ya dini.
Nini kifanyike...
Naamini katika mazungumzo. Hakuna njia ya mkato zaidi ya viongozi wetu wa kiislamu kuamua kuacha kujenga chuki za kisiasa. Lakini pia nadhani viongozi wa CHADEMA wana jukumu la kufanya katika hili zaidi ya kupuuzia. Ni kweli kuwa CHADEMA kinaweza kutimiza malengo yake ya kuchaguliwa kuongoza nchi 'katikati' ya juhudi hizi za kuipaka matope lakini, kwa maoni yangu haitakuwa na maana hata kama wakiingia madarani. Viongozi wa CHADEMA wanatakiwa 'KUWAONYESHA' waislamu kwa maneno na vitendo kuwa sio chama chenye dhamira yeyote mbaya kwa maslahi halali ya waislamu. Simaanishi kuwa kwa sasa CHADEMA inaonyesha kinyume chake, bali nadhani kwa kuna wanachama na wafuasi wa CHADEMA ambao wapo njia panda kutokana na kupewa 'maagizo' au kushawishiwa na viongozi wao kuwa CHADEMA hakifai. Najua ni vigumu kuwaondoa watu katika imani zao ndiyo maana inabidi CHADEMA ikubali kubeba vyote, watu, itikadi zao za kisiasa na imani zao.
Upo umuhimu wa viongozi wa CHADEMA kuonyesha 'heshima' kwa viongozi wa waislamu, sio tu kuwarudhisha viongozi hao, bali pia kutoa ujumbe kwa wanachama na wafuasi wao kuwa CHADEMA kinatambua na kuheshimu imani zao. Viongozi wa CHADEMA wamekuwa 'kimya' au wamekuwa nao wakijibu katika vyombo vya habari baadhi ya shutuma na lawama za viongozi wa waislamu. Sio vibaya, lakini kwa namna fulani inajenga picha ya 'bifu' ambayo madhara yake ndiyo hayo watu kuchotwa kisiasa, kwa imani za dini zao.
Naomba niishie hapa, nikiamini kuwa katika mazingira ambayo tumeshaanza kujengewa, michango 'negative' dhidi ya maoni na mapendekezo ya makala hii yatakuwepo. yapo mengi ya kujadili na kuelezana ili Tanzania iweze kuwa mahali pa amani...
Sio lengo la makala yangu kueleza chimbuko ama namna ambavyo viongozi hawa wamekuwa wakijenga uhasama huo kwani naamini wananchi wengi hayo wanayajua. Naomba nieleze kwa maoni yangu na kwa kuzingatia yale ninayoyaona athari za hatua hii inayochukuliwa na viongozi wa waislamu.
Naamini kama watu wenye akili timamu wanazo sababu zao za kujenga mazingira ya kuikosashe CHADEMA nafasi za kuongoza wananchi. Hilo sina tatizo nalo, ila wasiwasi wangu ni yatokanayo na hatua hizi walizochukua ndugu zetu. Sio sahihi kusema Tanzania hatujawahi kuwa na chembechembe za chuki za kidini, zimekuwepo lakini katika level ndogo isiyo na madhara makubwa (naamini kuna watu wenye maoni tofauti katika hili, nayaheshimu). Hata hivyo katika miaka ya karibuni, kwa kiasi kikubwa watanzania tulikuwa tunaaminiana licha ya kuwa na dini tofauti.
Ni jambo la kusikitisha kuwa chuki iliyojengwa na viongozi wa kiislamu dhidi ya CHADEMA imeanza, tena kwa kasi ya kutisha kurudisha chokochoko na chuki za kidini. Ingawa sio rahisi sana kuligundua hili, lakini siku hizi katika makundi ya watu, tayari kuna asilimia kubwa ambao wanaamini mtu anayeitwa Abdalah ni lazima atakuwa anashabikia chama fulani, na mtu anayeitwa Peter, anashabikia chama fulani. Kwa bahati mbaya zaidi kumekuwa na asilimia inayoongezeka kila kukicha ya watu ambao wanawa-treat watanzania wenzao kwa kuzingatia itikadi zao za kisiasa, ambazo 'wanazijua' kutokana na dini ya mtu. Miaka michache iliyopita ilikuwa ni nadra sana mtu kupewa au kunyimwa ajira, kwa sababu wa dini yake. Amini msiamini, kwa kipindi cha mwaka mmoja tu tangu viongozi wa waislamu walipoanza kuhubiri chuki dhidi ya CHADEMA, ubaguzi wa kidini umeshaanza kurudi tena kwa kasi ya ajabu.
Kwa mfano zipo taarifa za uhakika kuwa siku hizi kuna wahadhiri wa vyuo ambao mwanafunzi mwenye jina linaloashiria dini fulani hawezi kupata A kwenye somo lake. Mbaya zaidi wapo wengine wanadiriki kujitahidi kuwafelisha wanafunzi wanaodhaniwa kuwa wafuasi wazuri wa dini zao ama kwa mavazi wanayovaa, au matendo mengine. Wapo mabosi wengi ambao kama upo uwezekano, basi watajitahidi kwa nguvu zote kuhakikisha kuwa mtu mwenye jina linaloashiria dini fulani hatakuwa mfanyakazi wake. Mnaweza mkadhani kuwa naongeza chumvi katika hili lakini kama unaweza kusoma 'mioyo' ya watu, yapo maeneo mengine hata ile kusalimiana kwa 'moyo', kushirikiana kaitka mambo ya kijamii na kadhalika kumeshaathiriwa vibaya sana na itikadi za kisiasa, zinazotokana na udini. Ubaguzi umeshaanza kuota mizizi mahospitalini, mashuleni, wapo wanaoamini hata selection ya wanafunzi inaangalia dini, selection ya wanaokopeshwa kusoma vyuo vikuu inaangalia dini n.k, kisa kwa sababu dini yako ndiyo imefanya mbunge niliyemtaka asichaguliwe na mambo kama hayo.
Tunaweza tusikatane kwa mapanga kwa sasa, lakini athari za tatizo hili endapo likiendelea kufumbiwa macho na viongozi wetu wa dini na siasa, kama ilivyo sasa zitakuwa kubwa zaidi ya kukatana mapanga. Sitaki kuamini hivyo, lakini kama ni kweli kuna kundi moja la dini lililo na nafasi zaidi katika huduma za jamii, basi ni dhahiri kuwa kundi jingine lenye nafasi ndogo katika huduma za jamii litaumia. Kama walimu wakiamua kupendelea wanafunzi kwa imani zao, kama madaktari wakiamua kupendelea huduma kwa waumini wenzao, kama wahadhiri wakiamua kufaulisha au kufelisha wanafunzi kulingana na dini zao, kama waajiri wakiamua kuajiri watu waumini wenzao, mwisho wa siku viongozi wa dini au viongozi wa siasa hawataumia moja kwa moja, bali wananchi na waumini wa kawaida ndio watakaoumia.
Najua waislamu wamekuwa na madai kadhaa wanayotaka serikali iwatekelezee kama waislamu. Sioni namna yeyote ambayo madai hayo yatatekelezwa kwa kuwachukia CHADEMA, japo kwa maoni yangu. Siku zote nimekuwa nikiamini katika diplomasia na mazungumzo. Ni matumaini yangu kuwa ili mengi ya madai ya waislamu yaweze kutekelezwa, yatahitaji kuridhiwa katika vyombo vya maamuzi vya nchi hii, ambavyo bila shaka vinaundwa na watu wenye itikadi tofauti za kisiasa. Sioni sababu yeyote ya waislamu kukata tamaa ya kushawishi na kuamua kutumia mbinu ya kuwagawa watoa maamuzi kwa itikadi ya dini.
Nini kifanyike...
Naamini katika mazungumzo. Hakuna njia ya mkato zaidi ya viongozi wetu wa kiislamu kuamua kuacha kujenga chuki za kisiasa. Lakini pia nadhani viongozi wa CHADEMA wana jukumu la kufanya katika hili zaidi ya kupuuzia. Ni kweli kuwa CHADEMA kinaweza kutimiza malengo yake ya kuchaguliwa kuongoza nchi 'katikati' ya juhudi hizi za kuipaka matope lakini, kwa maoni yangu haitakuwa na maana hata kama wakiingia madarani. Viongozi wa CHADEMA wanatakiwa 'KUWAONYESHA' waislamu kwa maneno na vitendo kuwa sio chama chenye dhamira yeyote mbaya kwa maslahi halali ya waislamu. Simaanishi kuwa kwa sasa CHADEMA inaonyesha kinyume chake, bali nadhani kwa kuna wanachama na wafuasi wa CHADEMA ambao wapo njia panda kutokana na kupewa 'maagizo' au kushawishiwa na viongozi wao kuwa CHADEMA hakifai. Najua ni vigumu kuwaondoa watu katika imani zao ndiyo maana inabidi CHADEMA ikubali kubeba vyote, watu, itikadi zao za kisiasa na imani zao.
Upo umuhimu wa viongozi wa CHADEMA kuonyesha 'heshima' kwa viongozi wa waislamu, sio tu kuwarudhisha viongozi hao, bali pia kutoa ujumbe kwa wanachama na wafuasi wao kuwa CHADEMA kinatambua na kuheshimu imani zao. Viongozi wa CHADEMA wamekuwa 'kimya' au wamekuwa nao wakijibu katika vyombo vya habari baadhi ya shutuma na lawama za viongozi wa waislamu. Sio vibaya, lakini kwa namna fulani inajenga picha ya 'bifu' ambayo madhara yake ndiyo hayo watu kuchotwa kisiasa, kwa imani za dini zao.
Naomba niishie hapa, nikiamini kuwa katika mazingira ambayo tumeshaanza kujengewa, michango 'negative' dhidi ya maoni na mapendekezo ya makala hii yatakuwepo. yapo mengi ya kujadili na kuelezana ili Tanzania iweze kuwa mahali pa amani...