Ighombe
JF-Expert Member
- Feb 12, 2014
- 1,173
- 652
Hapo mi nakuelewa mzee .Ni noma kujificha kwenye mgongo wa kiswahili kwa kushindwa kingereza kwa kutumia meno uzalendo.Tatizo ni uongozi mbovu. Mzee wangu aliishia darasa la sita lakini alikuwa anaandika na kuongea kiingereza na watu wa mataifa mengine bila taabu.
Baada ya kuharibu elimu kiasi kikubwa wamefanya kuwa suala la kisiasa. Eti Kiswahili pekee ni kipimo cha uzalendo. Na Kiswahili chenyewe hakifundishwi vizuri. Kimeharibika sana. Matumizi ya l, r, tabu. “Hana” inaandikwa “ana”! Halafu wamefundishwa dawa ni “kujiamini”; yaani kuwa wabishi kufa wakikosolewa. Kujitetea na “uzalendo” bila kujali kuwa wanaangamizwa kwa kukosa fursa.
Kujua lugha nyingi za kimataifa ni faida. Kuna watu toka DR Congo wana nyadhfa katika serikali za Afrika ya Kusini, US, Uingereza. Walisoma shule kwa kifaransa lakini wana kiingereza cha uhakika na Kiswahili pia.
Tanzania hatuna teknolojia wala utajiri wa machapisho ya taaluma kwa Kiswahili. Hatulingani na wachina, wafaransa, wajerumani, warusi. Na hao wengi wanajua lugha za kimataifa zaidi ya moja. Wengi kiingereza wanacho ingawa sio lugha yao ya kujifunzia. Wanakitumia inapobidi.