Athari ya demokrasia kupitia maandamano yasiyo na ukomo

Teroburu

Member
Aug 6, 2009
41
3
Uendeshaji wa vyama kupitia maandamano unaficha mambo mengi ambayo ni vyema watanzania tujiulize. Je miaka 2010 hadi 2015 tutegemee maandamano wa mji hadi mji? Ndio demokrasia ya vyama inavyojengwa? Je tunatoa nafasi kwa chama kilichoshinda kutekeleza mipango yake?


Je upinzani unapinga nafasi ya uwekezaji wa nje kama njia muhimu ya kujenga uchumi na kujenga nafasi mpya za ajira? Je, ni sera ya upinzani kuwa wawekazaji katika sera ya madini waondoke na upinzani unafahamu athari za utaifishaji?

Maandamano hayatoi nafasi ya kuwauliza viongozi wa “Vyama-maandamano” kama wangependa waliowekeza SONGAS waondoke sasa hivi. Je tunao uwezo wa kununua mitambo ya kuchimba madili na kuchota gesi asilia kutoka ardhini bila kutegemea uwekezaji kutoka nje?

Je “Vyama-maandamano” vitatumia mbinu gani kuwashawishi wawekezaji wawekeze fedha nyingi za kigeni lakini sisi ndio tuvune matunda yetu? Watanzania ni bora tukumbuke kuwa tuna rasilmali nyingi sana ardhini lakini hii rasilmali sio yetu peke yetu kwa kuwa hatuna uwezo wa kifedha, kuitaalamu na kiufundi wa kuivuna.

Utamu wa maandamano ni nafasi ya kulaumu na kuahidi watanzania kuwa hali ya maisha ya watanzania yatabadilika endapo walio upinzani watachukua dhamana ya kuongoza nchi.

Maandamano zenye ahadi tamu tamu hayatoi nafasi kwa wananchi kujiuliza msimamo wa vyama-maandamano kuhusu sera zao na watatoa wapi rasilmali ya kubadili maisha ya watanzania kwa muda mfupi kama wanavyoahidi.

Bei ya petrol, dizeli na vyakula huko Kenya ni kubwa zaidi ya Tanzania. Mtikisiko wa uchumi wa dunia ulipo sasa, machafuko katika nchi zinazozalisha mafuta na kadhalika haitokani na chama kilichopo madarakani Tanzania.

Mimi nafahamu kuwa wengi katika Jamii forum, hawapendi kuwauliza “Vyama-maandamano” maswali magumu. Wengi tunapenda kusikia maneno matamu ya kulaumu, na kutoa ahadi kuwa ufumbuzi wa matatizo ya Tanzania ni kupitia “maandamano.” Kwa bahati mbaya pia, wengi hatupendi kujitafutia taarifa sisi wenyewe. Tunasubiri kuwa Fulani tunayempenda akishasema sisi tunakubali na pia tunawazomea kwa nguvu sana wale ambao wataonyesha dalili za kupingana au kuhoji. Hiyo ndio demokrasia ijayo Tanzania. Mungu Ibariki Tanzania.
 
...Bei ya petrol, dizeli na vyakula huko Kenya ni kubwa zaidi ya Tanzania.
Mkuu, ina maana hapo nyumbani kwako ukiona jirani analala njaa, na wewe uridhike tu usifanye kazi eti kwa kuwa wapo wengine wana hali mbaya kama wewe? Hizi comparison na Kenya et al hazina maana turidhike, kila nchi imejaliwa kuwa na resources tofauti tofauti!
 
Haya maandamano sio siri yamekuwa kero sasa, naamini Dr Slaa angekuwa ni mbunge haya maandamano yasingekuwepo
 
Kichwa cha mada hii ni potofu. Maandamano yanafanyika kwa vile hakuna demokrasia ya kutosha.

Kungekuweko na demokrasia hatungehitaji kufanya maandamano kudai katiba ya watu (na sio ya kuandikwa na mkuu wa chama kimoja na marafiki zake kama wanavyotaka kufanya CCM).

Kungekuweko na demokrasia hayangehitajika maandamano ya kudai wezi wa mali ya uma washitakiwe. Hilo lingefanyika kama kitu cha kawaida.

Katika demokrasi hayahitajiki maandamano kuthibiti serikali isipandishe kodi za bidhaa muhimu kiholela. Bunge lingetosha.

Kungekuweko na demokrasia wala CCM haingekuweko madarakani sasa. Tunaandamana kudai demokrasia. Usijaribu kutukanganya na maandamano yetu. Hatuachi.
 
Uendeshaji wa vyama kupitia maandamano unaficha mambo mengi ambayo ni vyema watanzania tujiulize. Je miaka 2010 hadi 2015 tutegemee maandamano wa mji hadi mji? Ndio demokrasia ya vyama inavyojengwa? Je tunatoa nafasi kwa chama kilichoshinda kutekeleza mipango yake?


Je upinzani unapinga nafasi ya uwekezaji wa nje kama njia muhimu ya kujenga uchumi na kujenga nafasi mpya za ajira? Je, ni sera ya upinzani kuwa wawekazaji katika sera ya madini waondoke na upinzani unafahamu athari za utaifishaji?

Maandamano hayatoi nafasi ya kuwauliza viongozi wa “Vyama-maandamano” kama wangependa waliowekeza SONGAS waondoke sasa hivi. Je tunao uwezo wa kununua mitambo ya kuchimba madili na kuchota gesi asilia kutoka ardhini bila kutegemea uwekezaji kutoka nje?

Je “Vyama-maandamano” vitatumia mbinu gani kuwashawishi wawekezaji wawekeze fedha nyingi za kigeni lakini sisi ndio tuvune matunda yetu? Watanzania ni bora tukumbuke kuwa tuna rasilmali nyingi sana ardhini lakini hii rasilmali sio yetu peke yetu kwa kuwa hatuna uwezo wa kifedha, kuitaalamu na kiufundi wa kuivuna.

Utamu wa maandamano ni nafasi ya kulaumu na kuahidi watanzania kuwa hali ya maisha ya watanzania yatabadilika endapo walio upinzani watachukua dhamana ya kuongoza nchi.

Maandamano zenye ahadi tamu tamu hayatoi nafasi kwa wananchi kujiuliza msimamo wa vyama-maandamano kuhusu sera zao na watatoa wapi rasilmali ya kubadili maisha ya watanzania kwa muda mfupi kama wanavyoahidi.

Bei ya petrol, dizeli na vyakula huko Kenya ni kubwa zaidi ya Tanzania. Mtikisiko wa uchumi wa dunia ulipo sasa, machafuko katika nchi zinazozalisha mafuta na kadhalika haitokani na chama kilichopo madarakani Tanzania.

Mimi nafahamu kuwa wengi katika Jamii forum, hawapendi kuwauliza “Vyama-maandamano” maswali magumu. Wengi tunapenda kusikia maneno matamu ya kulaumu, na kutoa ahadi kuwa ufumbuzi wa matatizo ya Tanzania ni kupitia “maandamano.” Kwa bahati mbaya pia, wengi hatupendi kujitafutia taarifa sisi wenyewe. Tunasubiri kuwa Fulani tunayempenda akishasema sisi tunakubali na pia tunawazomea kwa nguvu sana wale ambao wataonyesha dalili za kupingana au kuhoji. Hiyo ndio demokrasia ijayo Tanzania. Mungu Ibariki Tanzania.

Ndugu yangu Teroburu,
Inaonekana na wewe ni sehemu ya Upunguani wa akili wa nchi hii. Nadhani hujawi kuhudhuria mkutano hata mmoja wa CHADEMA na kusikiliza kile kinachongelewa kwenye mikutano hiyo. Kinachofanywa na CHADEMA hivi sasa ni kuwafunda wananchi ukakamavu ili 2015 tutakapoibiwa tena kura za urais basi tuzidai kama wakenya walivyozidai 2007.

Baada ya hapo ndipo utajua kwamba maandamano yasiyo na ukomo hayana athari kwa demokrasia bali yanaikomaza na kuifanya kuwa ya maana kuliku ilivyo hivi sasa.
 
Aliekufundisha na aliekutuma wana uafadhali katika kutojua mambo. Wewe waamini wawekezaji toka nje ndo wamepanua ajira? Watu kama Bakheresa ndo wawekezaji.

Ulishaenda migodini kutathimini watanzania wangapi wameajiriwa ukalinganisha na wanachovuna waliokutuma kupitia jina la wawekezaji?

Hao SONGAS unaowatolea mfano si ndo wametuingiza kwenye mgao kila mara au waishi ikulu ambako hata mgawo wa umeme sidhani kama wanauelewa maana yake.

Ndugu yangu kama wewe wamwogopa mungu ama mtume mohamad omba radhi watesekao kwa sababu ya uwekezaji na watanzania kwa ujumla. Umenipa hofu sana kama wajua kusoma na kuandika halafu unatuandikia madudu kama haya. Juzi tu Tarime watu wameuawa wewe unashabikia uwekezaji? Kama polisi na serikali yatambua amani kwa nini wawekezaji nao wasipigwe kwa kutotimiza na kujali wazalendo?
 
Hata Misri na Tunisia marais wao na wapambe wao waliongea maneno sawa na hayo..ila kilichotokea wote tunakijua, sasa wewe subiri tu uone nguvu ya umma
 
Kichwa cha mada hii ni potofu. Maandamano yanafanyika kwa vile hakuna demokrasia ya kutosha.

Kungekuweko na demokrasia hatungehitaji kufanya maandamano kudai katiba ya watu (na sio ya kuandikwa na mkuu wa chama kimoja na marafiki zake kama wanavyotaka kufanya CCM).

Kungekuweko na demokrasia hayangehitajika maandamano ya kudai wezi wa mali ya uma washitakiwe. Hilo lingefanyika kama kitu cha kawaida.

Katika demokrasi hayahitajiki maandamano kuthibiti serikali isipandishe kodi za bidhaa muhimu kiholela. Bunge lingetosha.

Kungekuweko na demokrasia wala CCM haingekuweko madarakani sasa. Tunaandamana kudai demokrasia. Usijaribu kutukanganya na maandamano yetu. Hatuachi.

You said it all Dr. Moshi, katika nchi kama Tananzania ambayo demokrasia inaamuliwa na chama tawala, hamna jinsi nyine zaidi ya kuuwezesha umma utambua kuwa wenyewe ndo wenye nguvu kuliko dolla na chama tawala.

Kwa miaka mingi watanzania wamejengewa uoga ka kutishwa na hawkuwahi kujua kuwa wao ndo waajiri wa hawa wanao jifanya miungu watu.

Kasumba hii bado ipo mpka leo huko vijijini watanzania wengi huko wanajua serikali na ccm ndo top wao, wakiongea kitu wao ni kutii tu pasipo kuuliza why?.

Chadema wanafanya kazi kubwa ya kuufumbua umma macho kuwa wao ndo waajiri wa hawa miungu watu, kuwa wao ndo wenyemaamuzi ya matumizi ya rasilimali zao na siyo serikali. Wao ndo wanaamua nani awekeze wapi na kwa faida gani

Huyu anayetaka watu waendelee kukaa kimya wawaache ccm waendelee kutafuna rasilimali za nchi hii kwa ufisadi basi hatufai na anasitahili kufungiwa jiwe laa kusagia shingoni akatupwe baharini

Tanzania hatuna bunge kwa sasa hivi ni ujinga mtupu unaendelea ndani ya hili bunge ambalo ndiyo mwakilishi wa wananchi.
Bunge badala ya kuisimamia serkali linaitetea serikali kwa maovu yake.
Ni bora wananchi wachukue hatua wenyewe pamoja na wabunge wachache wenye nia njema na nchi hii.

Huyu ndugu yetu kama hajaelewa maana ya haya maandamano basi tunamwelewesha kuwa yanatokana na kushindwa kwa bunge kuwakilisha mawazo halisi ya wananchi na badala yake limekuwa kibaraka wa serikali inayowakandamiza wananchi.

Habari ndo hiyo akawaambie na wanamagamba kama na wao hawajajua kwanini chadema wanaandamana.
 
ni kweli maandamano sio sera inayowezwa kutekelezwa na vizara fulani ili kuboresha maisha ya watu .lkn kwa TZ ngoja maandamano yaendelee kidogo ili kuamsha utamu wa siasa za tanzania ILI KUWAFANYA WALIOPEWA MADARAKA YA KUUTUMIKIA UMMA KUTOKAA MAOFISINI KUSUBIRI KULETEWA RIPOT KAMA MKUU WA KAYA ALIVYOKEMEA WAKATI AKIFUNGA SEMINA KWA MAWAZIRI. NA UTAMBUE KUWA watu waliopiga kura kumchagua rais hawafiki 25% ya watu waliojiandikisha. hivyo basi hii ni fursa mbadala ya kueneza elimu ya uraia ili watu wengi zaidi wawe na mwamko wa kushiriki katika shughuli za kisiasa wanapotaka kujenga taifa lenye ustawi na kufanya maamuzi sahihi juu ya hatma ya nchi yao.
 
Maandamano haya yanayofanywa ina maanisha hakuna DEMOKRASIA YA KWELI na ya HAKI ndiyo maana wananchi wanatafuta hiyo haki,kwa hiyo mada ya ndiyo inayo potosha jamii.Au wewe ni msemaji wa SISIEMU
 
Kinachofanyika hapa ni moja ya kazi/jukumu muhimu sana la chama chochote cha siasa popote kilipo. Jukumu hilo ni 'kuizimua' na kufanya 'conscientization' katika jamii ambamo chama hiki kinaitumikia.
Pia tukumbuke kuwa maana ya chama cha siasa ni kikundi cha watu fulani kilichoundwa kisheria kikiwa na malengo na nia ya kuondoa serikali iliopo madarakani. Siyo 'kuipindua' bali 'kuiondoa' kwa njia halali zilizopo.
Kuisifu au kuipa njia mbadala serikali inayoongozwa na chama tawala si kazi ya chama cha 'upinzani'.
Maandamano ya CDM ni sehemu ya jukumu la chama kuifanya/kuifahamish jamii kuhusu yale yanayoendelea/yaliyotokea/yatakayotokea ya kijamii, kisiasa, kiuchumi n.k. Briefly ni kusema kuwa wanafanya kazi yao! CDM si chama cha 'uchaguzi'
 
Uendeshaji wa vyama kupitia maandamano unaficha mambo mengi ambayo ni vyema watanzania tujiulize. Je miaka 2010 hadi 2015 tutegemee maandamano wa mji hadi mji? Ndio demokrasia ya vyama inavyojengwa? Je tunatoa nafasi kwa chama kilichoshinda kutekeleza mipango yake?


Je upinzani unapinga nafasi ya uwekezaji wa nje kama njia muhimu ya kujenga uchumi na kujenga nafasi mpya za ajira? Je, ni sera ya upinzani kuwa wawekazaji katika sera ya madini waondoke na upinzani unafahamu athari za utaifishaji?

Maandamano hayatoi nafasi ya kuwauliza viongozi wa “Vyama-maandamano” kama wangependa waliowekeza SONGAS waondoke sasa hivi. Je tunao uwezo wa kununua mitambo ya kuchimba madili na kuchota gesi asilia kutoka ardhini bila kutegemea uwekezaji kutoka nje?

Je “Vyama-maandamano” vitatumia mbinu gani kuwashawishi wawekezaji wawekeze fedha nyingi za kigeni lakini sisi ndio tuvune matunda yetu? Watanzania ni bora tukumbuke kuwa tuna rasilmali nyingi sana ardhini lakini hii rasilmali sio yetu peke yetu kwa kuwa hatuna uwezo wa kifedha, kuitaalamu na kiufundi wa kuivuna.

Utamu wa maandamano ni nafasi ya kulaumu na kuahidi watanzania kuwa hali ya maisha ya watanzania yatabadilika endapo walio upinzani watachukua dhamana ya kuongoza nchi.

Maandamano zenye ahadi tamu tamu hayatoi nafasi kwa wananchi kujiuliza msimamo wa vyama-maandamano kuhusu sera zao na watatoa wapi rasilmali ya kubadili maisha ya watanzania kwa muda mfupi kama wanavyoahidi.

Bei ya petrol, dizeli na vyakula huko Kenya ni kubwa zaidi ya Tanzania. Mtikisiko wa uchumi wa dunia ulipo sasa, machafuko katika nchi zinazozalisha mafuta na kadhalika haitokani na chama kilichopo madarakani Tanzania.

Mimi nafahamu kuwa wengi katika Jamii forum, hawapendi kuwauliza “Vyama-maandamano” maswali magumu. Wengi tunapenda kusikia maneno matamu ya kulaumu, na kutoa ahadi kuwa ufumbuzi wa matatizo ya Tanzania ni kupitia “maandamano.” Kwa bahati mbaya pia, wengi hatupendi kujitafutia taarifa sisi wenyewe. Tunasubiri kuwa Fulani tunayempenda akishasema sisi tunakubali na pia tunawazomea kwa nguvu sana wale ambao wataonyesha dalili za kupingana au kuhoji. Hiyo ndio demokrasia ijayo Tanzania. Mungu Ibariki Tanzania.

Je serikali ya CCM haioni madhara yatakayotokanayo na kuongezeka kwa gap kati ya wasio nacho na walio nacho?
Je serikali ya CCM na viongozi wake haioni ubaya wowote kuwa madalali wa maliasili kwa wawekezaji ambao hawajali maslahi ya wenyeji wao wakishakula ten percent lolote ktk mikataba hewala, na mwishowe wanaofaidi na wageni na wananchi kunyanyaswa ktk nchi yao, Je CCM haioni madhara ya ten percent ktk rasilimali zetu?
Je CCM haioni aibu kwa ahadi na ilani zisizotekelezeka wananchi washachoka na ahadi lukuki huku zikiwa hazifanyiwi kazi kuanzia ahadi za kumaliza mgao wa umeme hadi za kuifanya kigoma Dubai je hamuoni ubaya wa ahadi hewa wananchi wamechoka kufanywa majuha
Je CCM hamuoni kuwa mnawaletea machungu wananchi pamoja na kudidimiza uchumi wa nchi kwa vitendo vikubwa vya rushwa na ufisadi wa wazi tena mwingine ukisimamiwa na chama eg EPA, Rada, Richmond, Iptl na mengine mengi bila kuelezea ufisadi na rushwa ktk ofisi za serikali.
Je watz wategemee nini kutoka kwenu ikiwa huduma za jamii kama mahospitali na elimu zinazidi kudidimia huku mkiendelea na ngonjera zenu za maboresho nadaharia bila vitendo huku nyie mkitibiwa ktk hospitali binafsi na nje kwa kodi zetu? Huku watoto wenu wakisoma private na nje ya nchi?
JeCCM mtaendelea hadi lini kutoheshimu na kupindisha sheria kwa faida yenu? Ikiwa ni pamoja na tabia ya vyombo vya dola kutumia nguvu kubwa kwa raia wasio na silaha? Je kwenu ni sawa kutokuheshimu maoni na maamuzi ya wananchi kupitia haki yao ya kuchagua na mkawawekea watu wasiowataka kwa kushirikiana na NEC ''uchakachuaji''
Je ni sawa kwa nyie kuendelea kuwalinda wezi wa mali ya umma huku mkiwalundikia vyeo lukuki huku wananchi wanaotafta hela ya mlo wa siku mkiwaua kwa risasi na kuwaita wavamizi ndani ya nchi yao? na wale wavuvi maskini wanaotumia nyenzo hafifu badala ya kuwawezesha mnawaita haramu?
Je suala la kuwajibika kwa ''watawala'' wa CCM coz sio viongozi halipo wanafanya upuuzi mwingi lakini hawataki kuwajibika mifano iko mingi kwa mawaziri wa awamu hii sina haja ya kuitaja. Na ni lini mtaacha kutafuta visingizio na kutatua mataizo yetu? Msipachike siasa kila mahali.
Je ni lini CCM itaacha ukiritimba na usultani au uongozi wa majina a.k.a kubebana bila kuangalia uwezo huku mkieneza siasa za majitaka kwa kushutumu vyama flani wkt nyie ni wabaya kuliko hao
Je hamuoni mnarudisha maendeleo nyuma kwa viongozi kulipana mishahara na posho kubwa kubwa na watoto wao wakijilimbikizia mali ilihali watendaji kama walimu, wauguzi, polisi na madaktari wakiugumia kwa maumivu ya mshahara mdogo?
Kwa leo naishia hapa ingawa maswali ya nyie kujitafakari ni mengi kiasi kwamba unaweza jaza kurasa na kurasa, kabla hujaanza kuhoji kuhusu maandamano ya CDM na mustakabali wake ni vizuri mjihoji je mnatimiza wajibu wenu? Au mko pale kulalamika na kuanza kushutumu watu wakijaribu kuwakosoa? Hivi tu mnaanza kutafuta mchawi na kulilia na bado hatujaanza kushika bakora na kuwatandika sita za nguvu coz ndo njia iliyobaki ili mjitambue
 
Uendeshaji wa vyama kupitia maandamano unaficha mambo mengi ambayo ni vyema watanzania tujiulize. Je miaka 2010 hadi 2015 tutegemee maandamano wa mji hadi mji? Ndio demokrasia ya vyama inavyojengwa? Je tunatoa nafasi kwa chama kilichoshinda kutekeleza mipango yake?


Je upinzani unapinga nafasi ya uwekezaji wa nje kama njia muhimu ya kujenga uchumi na kujenga nafasi mpya za ajira? Je, ni sera ya upinzani kuwa wawekazaji katika sera ya madini waondoke na upinzani unafahamu athari za utaifishaji?

Maandamano hayatoi nafasi ya kuwauliza viongozi wa "Vyama-maandamano" kama wangependa waliowekeza SONGAS waondoke sasa hivi. Je tunao uwezo wa kununua mitambo ya kuchimba madili na kuchota gesi asilia kutoka ardhini bila kutegemea uwekezaji kutoka nje?

Je "Vyama-maandamano" vitatumia mbinu gani kuwashawishi wawekezaji wawekeze fedha nyingi za kigeni lakini sisi ndio tuvune matunda yetu? Watanzania ni bora tukumbuke kuwa tuna rasilmali nyingi sana ardhini lakini hii rasilmali sio yetu peke yetu kwa kuwa hatuna uwezo wa kifedha, kuitaalamu na kiufundi wa kuivuna.

Utamu wa maandamano ni nafasi ya kulaumu na kuahidi watanzania kuwa hali ya maisha ya watanzania yatabadilika endapo walio upinzani watachukua dhamana ya kuongoza nchi.

Maandamano zenye ahadi tamu tamu hayatoi nafasi kwa wananchi kujiuliza msimamo wa vyama-maandamano kuhusu sera zao na watatoa wapi rasilmali ya kubadili maisha ya watanzania kwa muda mfupi kama wanavyoahidi.

Bei ya petrol, dizeli na vyakula huko Kenya ni kubwa zaidi ya Tanzania. Mtikisiko wa uchumi wa dunia ulipo sasa, machafuko katika nchi zinazozalisha mafuta na kadhalika haitokani na chama kilichopo madarakani Tanzania.

Mimi nafahamu kuwa wengi katika Jamii forum, hawapendi kuwauliza "Vyama-maandamano" maswali magumu. Wengi tunapenda kusikia maneno matamu ya kulaumu, na kutoa ahadi kuwa ufumbuzi wa matatizo ya Tanzania ni kupitia "maandamano." Kwa bahati mbaya pia, wengi hatupendi kujitafutia taarifa sisi wenyewe. Tunasubiri kuwa Fulani tunayempenda akishasema sisi tunakubali na pia tunawazomea kwa nguvu sana wale ambao wataonyesha dalili za kupingana au kuhoji. Hiyo ndio demokrasia ijayo Tanzania. Mungu Ibariki Tanzania.

Nimependa sana hapo nilipo RED.

Ndio maana wakaitwa WADANGANYIKA. kwa maana hawajui kusema sikutenda.

 
Lengo kuu la maandamano haya nikujiongezea wana chama
kwani wapo watu wanaofata mkumbo lakini ni lazima
katika mikutano yao watoe muda wakuulizwa maswali nawananchi
pia wabunge waeleze mpaka sasa wametekeleza nn kwy ahadi zao
 
Mkuu una uchungu kweli na nchi hii?
Mkuu kuna jukwaa la mahaba kule may be ungeenda kule, kwani naamini kuwa hakuhitaji sana kuwa na upeo mkubwa wa kufikiri kabla ya kuchangia mada na siyo jukwaa la siasa mkuu. Nadhani umepotea.
 
Back
Top Bottom