Tetesi: ATCL yashindwa kutua Comoro na kurudi Dar es Salaam kufuatia hali mbaya ya hewa

khumbu_peresa

Member
Feb 11, 2021
28
105
Habari wana Jamvi,

Mimi ni mfuatiliaji mzuri wa sekta au tasnia ya usafiri wa anga kwa ndani ya nchi na kimataifa.

Siku ya jana tarehe 21/04/2022 shirika la ndege la Tanzania lilikua na ndege yake Airbus namba TC 210 ambayo inatoka DAR-HAH (DAR-COMORO) ambayo iliruka saa 4 asubuhi kuelekea Visiwani Comoros.

Pia Precision Air walikua wana Charter Flight (Ndege imekodishwa)siku hiyo kutoka Dar kwenda visiwani humo.
Umbali wa kutoka Dar mpaka Comoro ni km 683 sawa na 424.

Precision Air wakitumia ndege yao yenye usajili wa 5H-PWG ambayo ni aina ya ATR 72 yenye uwezo wa kubeba Abiria 70 kwa mpigo na mizigo tani 2.5 waliruka kuelekea Visiwani humo.

Kwa habari toka ndani ya vyanzo vya mamlaka ya ndege vinasema Ndege ya Air Tanzania ilifika kwenye Anga la Comoro na kushindwa kutua kwa kile Captain alichokiita hali mbaya ya hewa na kulazika kurudi tena Dar es salaam.

Watoa habari wanasema hii ni mara ya tatu kwa Rubani wa Air Tanzania kurudisha ndege Dar kutoka comoro hata kwa kitu ambacho kinaweza kuvumilika.

Huku nyuma Captain wa Precision Air aliyejulikana kwa jina moja la Captain Salim aliweza kutua Katika uwanja wa ndege wa Comoro salama kabisa mbali na hali ya hewa kuwa sio nzuri.

Bravo sana kwa Captain huyu wa Precision air hii inaonesha kuwa shirika la ndege la Precision lina marubani wenye uzoefu mkubwa kwenye tasnia hii ya anga pia shirika lina uzoefu mkubwa kwenye usafirishaji wa watu na mizigo yao.

Precision air wamekua kwenye hii biashara toka mwak 1995 na uzoefu huu umewasaidia kuwa extraordinary mbali ya shirika letu la Tanzania lenye ndege za kisasa.

Hongereni sana Precision Air.
 
Hii ni hasara kubwa kwa Air Tanzania. Inabidi wasafiri waliorudishwa watagharamikiwa na ATCL.
 
Mkuu katika kanuni za Urubani na Usalama wa anga maruani wote wako sahihi. Aina ya ndege unazozungumzia ni tofauti na zinaendesha na watu tofauti. Bottom line ni kwamba ingetokea tatizo kwa Ndege ya Precision si ajabu ingeoneka na Negligence kwa sababu mwenzake aliacha kutua kwa sababu ya hali ya HEWA.

Kumbuka katika usafiri wa Anga USALAMA Ndio kitu cha kwanza na kitendo cha wewe kusema kwamba Precision Ilitua pamoja na Hali ya Hewa kuwa mbaya ina maana unasema kwamba Precision Air hawachukulii suala la usalama wa anga kwa uzito wake.

Nimemaliza. Ila Hongera kwake Captain Salim kwa kuweza kuhakikisha abiria wanakuwa salama ila next time msijivunie RISK za kijinga kama hizi.
 
Habari wana Jamvi,

Mimi ni mfuatiliaji mzuri wa sekta au tasnia ya usafiri wa anga kwa ndani ya nchi na kimataifa...
Asante kwa tangazo




Screenshot_2022_0422_103514.jpg
 
Mkuu jaribu kufuatilia YouTube 'mayday' jinsi msururu wa vijimakosa vidogo vidogo vya kupuuza vinavyopoteza uhai wa mamia ya watu. Sijawahi kupanda ndege lakini nachoelewa tasnia ya safari za anga inajali sana usalama wa abiria kuliko gharama za uendeshaji.

Usifikiri lingetokea jambo lingekuwa LA rubani peke yake yaani hapo amelinda ajira za watu pamoja na biashara zao.
 
Mkuu katika kanuni za Urubani na Usalama wa anga maruani wote wako sahihi. Aina ya ndege unazozungumzia ni tofauti na zinaendesha na watu tofauti...
Swali la ufahamu kama utakuwa una ufahamu wa haya mambo, hivi anaeamua ndege kutua ni nani kati ya rubani na mwongoza ndege maana hapo naona rubani mmoja katua na mwingine kasepa.

Ngoja nimwite na barafu pia
 
Habari wana Jamvi,

Mimi ni mfuatiliaji mzuri wa sekta au tasnia ya usafiri wa anga kwa ndani ya nchi na kimataifa...
Wewe ndio mmoja wa abiria wale wajinga wanao shangilia speed ili kufika haraka na kuto jali usalama wa maisha yenu na miili yenu . sijaona post ya kijinga kama hii.
 
Swali la ufahamu kama utakuwa una ufahamu wa haya mambo, hivi anaeamua ndege kutua ni nani kati ya rubani na mwongoza ndege maana hapo naona rubani mmoja katua na mwingine kasepa.

Ngoja nimwite na barafu pia
Ndege inapokuwa Angani,Captain in Command Ndie anayewajibika katika kila jambo na ndio mwenye uamuzi wa mwisho.Na uamuzi wake ni final and conclusive hata kama uko wrong atawajibika nao lakini haweza ambiwa na mtu aliyeko chini atue wakati yeye anaona hawezi kutua halafu atue.Ili yule wa chini anaweza mwambia kapteni usitue lakini kapteni kwa utashi na uwezo na taarifa alizonazo kwa wakati huo akaamua kutua kwa kutegemea judgement yake.
 
Majuzi hapa pale Uganda Rwandair ilipiga mieleka .sasa huyu.mtoa uzi anataka ambia nini watuuuu

Au yy ana amini marubani wanaopata ajali ni wasio na uzoefu ? Acha zengwee mtoa UZI

ATC imekuwanikiruka kwenda Comoro kwa zaidi ya Mwaka sasa na hujuwah sikia ajali wala kwere kwere wacha watu wafanye vitu kwa usahihi
 
Siku ya jana tarehe 21/04/2022 shirika la ndege la Tanzania lilikua na ndege yake Airbus namba TC 210 ambayo inatoka DAR-HAH (DAR-COMORO) ambayo iliruka saa 4 asubuhi kuelekea Visiwani Comoros...
Kuna mwaka ilitokea hivyo walirudi wakatua Mtwara na Boeing 737
 
Back
Top Bottom