Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,337
- 113,178
Wanabodi,
Lile Shirika letu la Ndege, ATCL, lililokuwa mkao wa kifo, baada ya kuwa hoi bin taaban huku jeneza la kuizika rasmi likiwa limeishaandaliwa, hatimaye sasa litafufuka, kwa kuibuka kisasa zaidi, kwa nguvu zaidi na kurejea katika utawala wa soko la biashara ya ndege nchini (regain the past glory) katika kipindi kifupi kijacho.
Hayo yamebainishwa leo asubuhi na Kaimu Mtendaji Mkuu wa ATCL, Bw. Paul Chizi, katika mahojiano ya kipindi cha Jambo Tanzania, kinachorushwa hewani na TBC.
Huku akihojiwa na Mtangazaji mahiri kabisa wa TBC, Marine Hassan Marine, Bw. Paul Chizi amesema, baada ya ATCL kupewa mtaji mpya na serikali, sasa itajitegemea yenyewe na kwa kuanzia, itaanza na ndege zake mbili, moja ambayo ilikuwa kwenye matengenezo makubwa sasa imeshapona na imesharejea, na ya pili inakwenda kwenye matengenezo.
Bw. Chizi alitoa historia fupi ya ATCL tangu shirika lilipoanzishwa baada ya kuvunjika kwa iliyokuwa Jumuiya ya Afrika Mashariki, mwaka 1977, ATC ilikuwa na ndege 7, zikiwemo ndege mbili alizozirithi toka EA Airways, mwaka 1978, ilinunua ndege zake 5.
Akielezea kilichoiua ATCL ni zoezi la ubinafsishaji kwa Shirika la Ndege la Afrika Kusini, SAA, ulioliacha shirika hilo na madeni makubwa.
Marine Hassan alimbana zaidi Bw. Chizi, kuwa hata mara baada ya ubia huo na SAA kuvunjwa, mbona ATCL ilizidi kuzama, bwana Chizi alijibu majibu ya kichekesho eti kuwa "ni kawaida kwa baadhi ya mashirika ya ndege kufa, na kutolea mfano shirika la ndege la Uswissi, Swissair na lile la Italia, Alitalia kuwa yamekufa, hivyo sio ajabu kwa ATCL kufa!.
Marine alimbana zaidi kuwa kwa vile mashirika hayo aliyoyataja yamekufa, hivyo ndio sababu kweli ya shirika letu kufa!?. Bwana Chizi alisisitiza ndio, kama mashirika haya makubwa yamekufa, hiyo ni sababu tosha kwa nini ATCL isife!.
Mtangazaji Marine akazidi kubanana na Chizi, kuwa Tanzania sasa tuna mashirika binafsi ya ndege yenye mafanikio makubwa, akauliza, iweje mashirika binafsi yaliyokuwa hayana kitu, yafanikiwe, na shirika la umma lenye kila kitu life?!. Bwana Chizi alijibu kuwa hayo mashirika yaliyofanikiwa, yameweza kufanikiwa tuu kwa vile ATCL ilikuwa imekufa, maadam sasa imefufuka, sasa ATCL itarejea kwenye hadhi yake ya zamani!.
Marine Hassan akamdodosa bwana Chizi, jee ATCL itaweza vipi kuwarejesha abiria wake iliyowapoteza. Bwana Chizi amesema anaamini Watanzania wanalipenda shirika lao, hivyo mara watakapo rejea hewani, Watanzania watawaunga mkono kama zamani.
Mtangazaji Marine ilizidi kumbana bwana Chizi kwa kumsukumiza kabisa kwenye kona, alipomuuliza kuwa kama ATCL itaweza kuhimili ushindani wa soko dhidi ya mashirika mengine ambayo tayari yameisha imarika, Bwana Chizi, sio tuu alitoa kichekesho kingine, bali piauvunjwaji wa sheria za biashara huria, alipojibu kuwa ATCL itaiomba serikali kutoa waraka maalum, utakaowalazimisha watumishi wote wa umma, ni lazima waitumie ATCL, na wataweza tuu kutumia ndege za mashirika mengine pale tuu ambapo ATCL haiendi!.
Hili pia lilimshtua Marine Hassan alipomuuliza, hili la waraka, jee, halitasababisha ukiukwaji wa misingi ya soko huria na ushindani wa haki?!. Bwana Chizi, akasisitiza, hizo ndizo mbinu zinazotumiwa na mataifa mbalimbali kuhakikisha mashirika yake ya ndege, yana survive na kutolea mfano Uingereza, kuwa watumishi wa umma wa Uingereza, lazima wazitumie ndege za British Airways kila wanaposafiri, na endapo watakosa nafasi, ndipo wanaweza kupanda ndege za mashirika mengine. Kipindi kikaisha!.
MY TAKE
Japo habari hizi za kufufuka kwa a national flag carrier ni good news kwa Wazalendo, lakini ni bad news kwa private flights operators wa sekta binafsi kama Precision Air, maana ATC ikiimarika ni kifo kwao!.
Ila kama Bw. Paul Chizi anayekaimu u-CEO wa ATCL ndiye huyu niliyemuona na kumsikia leo, na kama ndiye yeye anayesubiria kuidhinishwa na Bodi ya ATCL kuwa CEO kamili, then, ATCL ni Bye Bye jumla, kaburini kabisa!, hivyo Precision Air Air itaendelea kupumua.
Mungu Ibariki ATCL!
Mungu Ibariki Tanzania!
Pasco.
Lile Shirika letu la Ndege, ATCL, lililokuwa mkao wa kifo, baada ya kuwa hoi bin taaban huku jeneza la kuizika rasmi likiwa limeishaandaliwa, hatimaye sasa litafufuka, kwa kuibuka kisasa zaidi, kwa nguvu zaidi na kurejea katika utawala wa soko la biashara ya ndege nchini (regain the past glory) katika kipindi kifupi kijacho.
Hayo yamebainishwa leo asubuhi na Kaimu Mtendaji Mkuu wa ATCL, Bw. Paul Chizi, katika mahojiano ya kipindi cha Jambo Tanzania, kinachorushwa hewani na TBC.
Huku akihojiwa na Mtangazaji mahiri kabisa wa TBC, Marine Hassan Marine, Bw. Paul Chizi amesema, baada ya ATCL kupewa mtaji mpya na serikali, sasa itajitegemea yenyewe na kwa kuanzia, itaanza na ndege zake mbili, moja ambayo ilikuwa kwenye matengenezo makubwa sasa imeshapona na imesharejea, na ya pili inakwenda kwenye matengenezo.
Bw. Chizi alitoa historia fupi ya ATCL tangu shirika lilipoanzishwa baada ya kuvunjika kwa iliyokuwa Jumuiya ya Afrika Mashariki, mwaka 1977, ATC ilikuwa na ndege 7, zikiwemo ndege mbili alizozirithi toka EA Airways, mwaka 1978, ilinunua ndege zake 5.
Akielezea kilichoiua ATCL ni zoezi la ubinafsishaji kwa Shirika la Ndege la Afrika Kusini, SAA, ulioliacha shirika hilo na madeni makubwa.
Marine Hassan alimbana zaidi Bw. Chizi, kuwa hata mara baada ya ubia huo na SAA kuvunjwa, mbona ATCL ilizidi kuzama, bwana Chizi alijibu majibu ya kichekesho eti kuwa "ni kawaida kwa baadhi ya mashirika ya ndege kufa, na kutolea mfano shirika la ndege la Uswissi, Swissair na lile la Italia, Alitalia kuwa yamekufa, hivyo sio ajabu kwa ATCL kufa!.
Marine alimbana zaidi kuwa kwa vile mashirika hayo aliyoyataja yamekufa, hivyo ndio sababu kweli ya shirika letu kufa!?. Bwana Chizi alisisitiza ndio, kama mashirika haya makubwa yamekufa, hiyo ni sababu tosha kwa nini ATCL isife!.
Mtangazaji Marine akazidi kubanana na Chizi, kuwa Tanzania sasa tuna mashirika binafsi ya ndege yenye mafanikio makubwa, akauliza, iweje mashirika binafsi yaliyokuwa hayana kitu, yafanikiwe, na shirika la umma lenye kila kitu life?!. Bwana Chizi alijibu kuwa hayo mashirika yaliyofanikiwa, yameweza kufanikiwa tuu kwa vile ATCL ilikuwa imekufa, maadam sasa imefufuka, sasa ATCL itarejea kwenye hadhi yake ya zamani!.
Marine Hassan akamdodosa bwana Chizi, jee ATCL itaweza vipi kuwarejesha abiria wake iliyowapoteza. Bwana Chizi amesema anaamini Watanzania wanalipenda shirika lao, hivyo mara watakapo rejea hewani, Watanzania watawaunga mkono kama zamani.
Mtangazaji Marine ilizidi kumbana bwana Chizi kwa kumsukumiza kabisa kwenye kona, alipomuuliza kuwa kama ATCL itaweza kuhimili ushindani wa soko dhidi ya mashirika mengine ambayo tayari yameisha imarika, Bwana Chizi, sio tuu alitoa kichekesho kingine, bali piauvunjwaji wa sheria za biashara huria, alipojibu kuwa ATCL itaiomba serikali kutoa waraka maalum, utakaowalazimisha watumishi wote wa umma, ni lazima waitumie ATCL, na wataweza tuu kutumia ndege za mashirika mengine pale tuu ambapo ATCL haiendi!.
Hili pia lilimshtua Marine Hassan alipomuuliza, hili la waraka, jee, halitasababisha ukiukwaji wa misingi ya soko huria na ushindani wa haki?!. Bwana Chizi, akasisitiza, hizo ndizo mbinu zinazotumiwa na mataifa mbalimbali kuhakikisha mashirika yake ya ndege, yana survive na kutolea mfano Uingereza, kuwa watumishi wa umma wa Uingereza, lazima wazitumie ndege za British Airways kila wanaposafiri, na endapo watakosa nafasi, ndipo wanaweza kupanda ndege za mashirika mengine. Kipindi kikaisha!.
MY TAKE
Japo habari hizi za kufufuka kwa a national flag carrier ni good news kwa Wazalendo, lakini ni bad news kwa private flights operators wa sekta binafsi kama Precision Air, maana ATC ikiimarika ni kifo kwao!.
Ila kama Bw. Paul Chizi anayekaimu u-CEO wa ATCL ndiye huyu niliyemuona na kumsikia leo, na kama ndiye yeye anayesubiria kuidhinishwa na Bodi ya ATCL kuwa CEO kamili, then, ATCL ni Bye Bye jumla, kaburini kabisa!, hivyo Precision Air Air itaendelea kupumua.
Mungu Ibariki ATCL!
Mungu Ibariki Tanzania!
Pasco.